Saturday, December 11, 2010

WANYANG'ANYWA ARDHI YAO HUKO BABATI BILA YA KUPATIWA FIDIA YOYOTE.



WAADHIMIA KUFANYA MAANDAMANO BAADA YA KUNYANG'ANYWA ARDHI YAO BILA FIDIA BABATI
.


BAADHI ya wakazi wa mtaa wa Bagara ziwani wilayani Babati wameazimia kufanya maandamano ya amani hadi kwa Mkuu wa mkoa wa Manyara,Henry Shekifu kutokana na kilio chao cha muda mrefu cha kunyang'anywa ardhi yao bila fidia ya maana.

Wakizungumza na waandishi wa habari juzi mjini Babati huku wakiwa na masikitiko makubwa wakazi hao zaidi ya 48 walidai kuwa wataandamana hadi kwa Mkuu huyo wa Mkoa na endapo kilio chao hakitasikilizwa watakwenda kulalamika kwa waziri mwenye dhamana ya ardhi.

Mmoja kati ya wakazi hao Athumani Omary alisema kuwa wamemiliki ardhi hiyo kwa zaidi ya miaka 40 lakini serikali inataka kuwahamisha bila kuwafidia na kuwapa eneo jingine.

Omary alisema katika ardhi hiyo yapo makaburi ya wazazi wao waliofariki na kuzikwa hapo pia kuna watu waliozaliwa kwenye ardhi hiyo hivyo hawatakubali waporwe ardhi yao kwa urahisi.

Naye Sakwara Muna alisema japo Babati ni makao makuu ya mkoa wa Manyara hawapingi eneo lao kutumika kwa ajili ya kupatikana maendeleo lakini wanapaswa wapatiwe eneo mbadala la kuhamia.

Muna alisema kama Serikali imeamua eneo la Bagara ziwani ni la kujengea majengo mapya ya taasisi mbalimbali za kibinafsi na serikali inatakiwa kuwajali wale wanaoishi kwenye eneo hilo.

Mkazi mwingine Tatu Sakwara alisema baadhi ya viongozi wa ardhi wilayani Babati wamekuwa wakitoa fidia ambayo hailingani na thamani ya ardhi kwani familia yenye makaburi na ardhi ya eka 10 huwezi kuwapa sh 200,000 kwa kila eka.

Sakwara alisema kuwa hivi karibuni Jeshi la polisi mkoani humo lilijenga makazi ya polisi baada ya kununua eneo kwa sh 78 milioni lakini hawajaambulia chochote kwenye fedha hizo.

Hata hivyo Mwenyekiti wa mtaa huo,Juma Akedai alikiri kufahamu mgogoro huo na kudai kuwa wakazi hao wananyanyaswa kutokana na kutotendewa haki na Serikali.

Wednesday, December 8, 2010

KANISA KATOLIKI JIMBO LA NJOMBE KUTOA HUDUMA YA UMEME KWA BEI NAFUU.

KANISA LAWAKUMBUKA WAUMINI WAKE NA KUAMUA KUTOA HUDUMA YA UMEME KWA WANANCHI NJOMBE.


Wakati Wananchi wakipata Hadha kubwa kutokana na Kukatizwa Katizwa kwa Huduma ya Umeme Mara kwa Mara Sasa Hali hio huenda Ikawa Historia Baada ya Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe Kuanza Kutoa Huduma ya Umeme kwa Bei Nafuu Tofauti na Ile inayotozwa na Shirika la Ugavi Tanzania TANESCO

Katika Kutatua Kero kwa Njia Iliosahihi Zaidi ya Wakazi 250 Wameripotiwa kuanza kunufaika na Huduma hiyo ambayo pia itawaunganisha Wakazi wa Ludewa.

Askofu wa jimbo hilo Mhashamu Alfred Maluma amesema lengo la mradi huo ni kuwapa nyenzo ya kuondokana na umasikini kutokana na maeneo ya vijiji ambavyo viko katika mazingira magumu ya kufikiwa na maendeleo yanayofanywa na Serikali.

Akizungumzia Mradi Huo wa umeme wa Mawengi wilayani Ludewa unaoendeshwa na kanisa Katoliki Jimbo la Njombe Askofu huyo Amesema Mradi huo pia umeanza kusambaza umeme kwa wananchi kwa bei nafuu kuliko inayotozwa na Shirika la Umeme (Tanesco).

Askofu Maluma alikuwa akizungumza na kundi la wanahabari waliotembelea mradi huo ambao umejengwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la ACRA chini ya ufadhili wa Serikali ya Italia.

Kwa mujibu wa Katibu wa Huduma za jamii na Maendeleo wa kanisa Katoliki jimbo la Njombe, Padri Evodius Msigwa wananchi ambao wameunganishiwa umeme hadi sasa wanafikia 250 na juhudi zinaendelea kuwaunganishia wengine.

Padri Msigwa ambaye ni Paroko wa kanisa Katoliki parokia ya Njombe alisema kutokana na wananchi wengi kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za kuunganisha umeme, jumuiya ya Lumama inawatoza asilimia 20 ya maunganisho na asilimia 80 wanalipa kidogo kidogo ndani ya mwaka mmoja.

Umeme huo unaozalishwa kwa kutumia maporomoko ya maji kama ilivyo kwa vyanzo vingine vya Tanesco, unahudumia vijiji vitatu vya Mawengi, Lupande na Madunda na una uwezo wa kuzalisha kilowati 150 kwa siku.

Askofu huyo alisema ili umeme huo uweze kuwafikia watu wengi katika vijijini vingine, ni lazima Serikali ishirikiane kwa karibu na kanisa hilo, wahisani pamoja na Wakala wa Umeme Vijijini (Rea) ili kuusambaza kwa wananchi wengi zaidi kutokana na miundombinu yake kuwa aghali.

HOSPITALI YA WILAYA NJOMBE (KIBENA) YAKOSA HUDUMA YA X-RAY.

MWEZI WA SABA SASA HOSPITALI YA WILAYA NJOMBE (KIBENA) YAKOSA HUDUMA YA X-RAY.



Zoezi la Kutambua na Upimaji Wagonjwa wa Fistula Wilayani Njombe limeshindwa kufanyika kama ilivyokusudiwa kufuatia Idadi ndogo ya Wananchi waliojitokeza katika Hospitali ya Mji wa Njombe Kibena

Hadi Kufikia jana wakati wa Kufunga Zoezi hilo ni Mwanamke Mmoja Tu aliejitokeza kupimwa na kugundulika kuwa na Ugonjwa huo ambae Tayari amepelekwa katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa kwa ajili ya Matibabu Zaidi

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mji wa Njombe Kibena Daktari Evarest Mtitu Amesema idadi hio ndogo ya Wananchi waliojitokeza Imetokana na Kuchelewa kufika kwa Taarifa kwa Wananchi juu ya Uendeshwaji wa Zoezi hilo ambalo liliendeshwa kwa siku mbili

Amesema kutokana na Ufinyu wa Bajeti katika Sekta ya Afya Wilayani Njombe Umechangia kutokufanikiwa kwa

Kwa Mwezi wa Saba Sasa Hospitali ya Kibena Wilayani Njombe imeshindwa kutoa Huduma ya Upigaji Picha za X-Ray Kutokana na Kukosa Mtaalamu wa Fani hio

Hali hio imetokana na Mtaalamu Aliekuwepo Awali kupata Nafasi ya Masomo na Kwenda Kusoma Katika Tume ya Taifa ya Mionzi hali ambayo Imesababisha Huduma Hio Kusitishwa

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Kibena Daktari James Ligwa Amesema kutokana na Kukosekana kwa Huduma Hio katika Hospitali hio imesababisha Wananchi kulazimika kwenda katika Vituo na Zahanati Binafsi ili kuweza kupata Huduma Hizo Hatua Ambayo Imewasababishia Kuongeza Ugumu wa Maisha Kutokana na Gharama Kubwa katika Vituo Hivyo

Amesema Hospitali ya TANWART na IKONDA zimekuwa Zikitumiwa na Hospitali hio Kama Njia Mbadala ya kusaidia Wagonjwa wanaofikia katika Kituoi Hicho Kwa ajili ya Kuhitaji Huduma Hizo

Akizungumza na mtandao huu Hospitalini hapo Mganga Mfawidhi wa Hospitali hio Daktari Evarest Mtitu Amesema Tayari Wamewasiliana na Serikali kwa ajili ya kuomba Kuajiri Mtaalamu Mwingine ambapo kwa sasa Wanasubiri majibu kulingana na Taratibu za Ajira

BEI KUBWA YA MBOLEA YAWA KIKWAZO KWA WAKULIMA WILAYA YA NJOMBE

MBOLEA ZAWA KIKWAZO KWA WAKULIMA ,NJOMBE.

Wananchi Wilayani Njombe Wameendelea kulalamikia Bei Kubwa ya Mbolea licha ya serikali kutangaza kuwa Zingeuzwa kwa punguzo kufuatia kuwepo kwa Utaratibu wa Malipo ya Ruzuku

Katika Vijiji vya Lupembe,Tarafa za Makamabako na Maeneo ya Ilembula Wananchi Wamelalamikia Kuuziwa Mbolea Hizo kwa bei ya juu Zaii Toafuti na Walivyoelekezwa hapo Awali

Wakiongea na mtandao huu baadhi ya wananchi wamesema mbolea aina ya DAP kwa madukani inauzwa 65 elfu kwa ruzuku wananunua kwa shilingi 39 elfu ambapo serikali inakua imelipia kiasi cha 26 elfu.Kwa upande wa mbegu,wamesema kwa kilo 10 ya luzuku inauzwa 20 elfu na madukani inauzwa 40 elfu.

Hali Hio Imewafanya Wananchi hao Wasione Umuhimu wa kuwepo kwa Ruzuku hio kwani Bei Inayouzwa Madukani Wamedai kutotofautiana na Bei inayouzwa na Mawakala wa Ruzuku

Licha ya Malalamiko hayo lakini Bado Wananchi hao Wameelezea jinsi Zoezi hilo linavyoendeshwa kwa madai ya kuendeshwa katika hali ya Taratibu hali ambayo inawachelewesha kuanza Msimu Mpya wa Kilimo Ambao Unakaribia kuanza

Mmoja wa Mawakala wa mbolea CLEA MGINA, amesema sababu za kuchelewa kumaliza zoezi hilo ni Kutokana na gharama kubwa za Ununuzi wa Mbolea Hizo hivyo wananchi wanashindwa kulipia kwa Wakati gharama hizo.

Thursday, December 2, 2010

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI 1 DISEMBA 2010


HOTUBA YA MKUU WA WILAYA YA NJOMBE MH.SARA DUMBA KATIKA SIKU YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI 1 DISEMBA 2010.

Waheshimiwa Viongozi wa Wilaya, Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa Idara, Maafisa Tarafa, Maafisa Watendaji wa kata, Viongozi wa Madhehebu ya Dini, Wazee wetu na Ndugu wananchi wa Tarafa ya Makambako,
KAMWENE,
BWANA YESU ASIFIWE
TUMSIFU YESU KRISTU,
SALAAM ALEIKUM!!!

Ndugu Wananchi,

Awali ya yote, napenda kuchukua fursa hii ya pekee kuwashukuru viongozi wote Tarafa ya Makambako , Kata ya Igongolo, Kijiji cha Kichiwa kwa kunialika kuja kujumuika nanyi katika siku hii muhimu ya maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani na kunipa nafasi ya pekee ya kuwa mgeni rasmi.

Siku ya leo ya Tarehe 1 Disemba 2010 tumekusanyika hapa kwa lengo la kuadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani inayoadhimishwa Duniani kote katika kuhamasisha jamii katika mapambano dhidi ya UKIMWI na kutafakari madhara yanayotokana na janga hili la UKIMWI, vile vile kuikumbusha jamii kuweka mikakati ya kupambana na UKIMWI kwa dhati. Ujumbe wa mwaka huu ni “MWANGA KWA HAKI” Wadau wote kutoa na kutetea upatikanaji wa huduma na haki za binadamu kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI.

Ndugu Wananchi,

Tangu UKIMWI ulipogundulika Nchini mwaka 1983 Serikali imeweka mipango mbalimbali ya Mapambano dhidi ya UKIMWI ikiwa ni pamoja na kuadhimisha Siku hii ya tarehe Mosi Disemba inayoendana na upimaji wa hiari wa virusi vya ukimwi.



Ndugu wananchi,

Njombe kama zilivyo wilaya nyingi nchini ni miongoni mwa Wilaya zinazokabiliwa na ongezeko kubwa la maambukizi ya virusi vya Ukimwi miongoni mwa Wananchi.

Ndugu wananchi,

Unyanyapaa unasababisha maambukizi yazidi kuongezeka kwa kuwa watu wanaficha hali zao na kufanya ngono zisizo salama na wengine kutojitokeza kupima.

Ndugu wananchi,

Ni ukweli usiopingika kuwa Elimu juu ya Ukweli kuhusu UKIMWI imetolewa nchini na kwa wilaya yetu kwa kiwango kikubwa lakini bado idadi ya watu wanaojitokeza kupima ni ndogo sana na kwa wakati huohuo hali ya maambukizi imefikia Asilimia 25.4% kwa waliopimwa katika Vituo vya Ushauri Nasaha kuanzia Januari hadi Septemba, 2010.

UPIMAJI WA HIARI WA VIRUSI VYA UKIMWI

Ndugu wananchi,

Tangu Ukimwi ulipogundulika nchini Tanzania mwaka 1983 maambukizi ya UKIMWI yameendelea kuongezeka na kusambaa kwenye Mikoa na Wilaya zote.

Katika Wilaya yetu ya Njombe, wagonjwa wa kwanza Watatu(3) waligundulika katika Hospitali ya Ilembula mwaka 1986 ambako upimaji wa Virusi vya UKIMWI ulianza kufanyika. Na hali ya maambukizi mapya imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.

Watu waliojitokeza kupima tangu Julai 2005 hadi Septemba 2010 ni 80,415 kati yao 41,204 ni Wanaume na 59,577 ni Wanawake. Waliogunduliwa kuwa na Virusi vya UKIMWI ni 17,093 ambapo kati yao Wanaume ni 6,538 na Wanawake ni 10,555 Hivyo kiwango cha maambukizi ya UKIMWI kufuatia upimaji huu ni 19.2%.kama jedwali Na. 1 hapa chini linavyoonyesha takwimu ya Upimaji kwa ufupi tangu mwaka 2005/06 hadi Septemba 2010

Jedwali na 1: Upimaji wa virusi vya UKIMWI

Idadi ya waliopima Wenye Virusi
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
2005/06 2,725 2,262 4,987 372 540 912 18.2%
2006/07 4,029 4,315 8,345 600 890 1,490 17.9%
2007/08 23,779 37,323 61,102 3,089 5,491 8,580 14.0%
2008/09 6,110 6,757 12,867 1,070 1,605 2,675 20.7%
Jan – Sept
2010 4,561 8,920 13,481 1,407 2,029 3,436 25.4%

JUMLA 41,204 59,577 80,415 6,538 10,555 17,093 19.2%
Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii



Ndugu wananchi,

Hali ni mbaya zaidi kwa kuwa inaonyesha watu wengi wanazidi kupata maambukizi ya magonjwa ya ngono kwani kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2010 hadi Septemba, 2010 kati ya wagonjwa waliofika hospitali ya Wilaya ya Njombe kutibiwa magonjwa mbalimbali , jumla ya watu ..... waligundulika kuwa na magonjwa ya ngono wakiwemo wanaume .... na wanawake .... , idadi hii ni kubwa kwani magonjwa ya ngono ni moja ya viashiria vya ukubwa wa maambukizi ya UKIMWI kwani tafiti nyingi zinadhihirisha kuwa asilimia ........ya watu wanaougua magonjwa ya ngono huwa na maambukizi ya UKIMWI.



Ndugu Wananchi,

Suala la hofu ya kupima na kubainika kuwa na maambukizi inabidi mlipinge vikali kwani baada ya mtu kugundulika ameambukizwa Ukimwi ataweza kupata huduma za dawa ya kupunguza makali ya Ukimwi katika sehemu mbalimbali mfano Hospitali ya Njombe TANWAT na Ilembula na kupata ushauri nasaha na hivyo kumuwezesha kuendelea na maisha yake kama kawaida.Mtu ukipima na kujua hali yako utajua ni namna gani uishi na hivyo utajiongezea muda mrefu wa kuishi.

Kadhalika Wilaya imeweka mpango wa kuanzisha vituo vingine vya kutoa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi katika Zahanati ya Kipengere,Kituo cha Afya cha Makambako na Lupembe ili kuwapunguzia gharama za Usafiri wa kufuata huduma hizo Wilayani.

Ndugu Wananchi,
Napenda kuwashukuru sana wale wote waliojitokeza kupima UKIMWI kwa hiari, na kwa wale ambao hawakujitokeza basi nawaomba waende wakapime ili kwa pamoja tuweze kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI wilayani Njombe.
Pia sote tutambue kuwa tunawajibu wa kuwasaidia Watoto yatima na Waathirika wa ukimwi.

TAARIFA YA HALI YA UKIMWI KATIKA WILAYA YA NJOMBE

TAARIFA YA HALI YA UKIMWI KATIKA WILAYA YA NJOMBE SIKU YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI DISEMBA MOSI 2010 KATIKA KIJIJI CHA KICHIWA KATA YA IGONGOLO.

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Leo ni mara ya Tano tangu mwaka 2006 kwa kufanya maadhimisho rasmi ya Kitaifa ya Siku ya UKIMWI Duniani katika Wilaya ya Njombe.

Mwaka huu 2010 Kitaifa maadhimisho ya Siku hii yatafanyika katika Manispaa ya Morogoro uwanja wa Nane Nane.

Ujumbe wa Mwaka 2010 ni “MWANGA KWA HAKI”
…..Wadau Wote wanatakiwa kutoa na kutetea upatikanaji wa huduma na haki za binadamu kwa watu Wanaoishi na Virusi Vya UKIMWI….


Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Kimsingi wakati tunatafakari ujumbe huu katika maadhimisho haya nia kubwa ni kuihamasisha jamii iweze kutambua kuwa hali ya UKIMWI Wilayani Njombe ina athari kubwa na kuwa janga la UKIMWI linaathiri mtu binafsi,familia,jamii,Wilaya,Mkoa na Kitaifa.

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Ifahamike wazi kuwa madhara yanayotokana na maambukizi ya UKIMWI ni makubwa kwa kila mwananchi,jitihada kubwa zinafanyika kitaifa na Kiwilaya za kukabiliana na UKIMWI kwa kutoa elimu na huduma za kuzuia maambukizi mapya,tiba na huduma kwa watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI hata hivyo bado changamoto ni nyingi sana katika Wilaya yetu.

Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ni:
i.Ongezeko la huduma za utoaji dawa za tiba endelevu katika Vituo vya Vijijini mfano Kidugala,Lupembe na Makambako ili kusogeza huduma karibu na Wananchi
ii.Kuendelea kupokea fedha toka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania ambapo kwa Mwaka 2009/10 Wilaya imepokea jumla ya Tsh.114,974,000 kati ya fedha hizo Tsh.77,259,000 zimepokelewa na Halamshauri ya Wilaya ya Njombe na Sh.37,715,000 zimepokelewa na Halamsahuri ya Mji wa Njombe kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ya Kudihibiti UKIMWI ikiwemo ya kuhudumia watoto Yatima,Watu Wanaoishi na VVU pia kutoa elimu ya mapambano dhidi ya UKIMWI kwa makundi mbambali.

iii.Wilaya imeendelea kupata misaada na huduma kutoka kwa Wadau kama TUNAJALI,JPIEGO,fhi-ROADS Project,Asasi za Kidini na Kiraia na Wanachi kwa ajili ya mapambano dhidi ya UKIMWI



HALI YA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Katika kipindi cha Januari hadi Septemba, 2010 jumla ya Watu 13,481 walijitokeza kupima VVU kati yao Wanaume 4,561 na Wanawake 8,920 ambapo waliogundulika kuwa na VVU ni 3,436 kati yao Wanaume 1,407 na Wanawake 2,029 Sawa na asilimia 25.4 hii ni kutokana na idadi ndogo ya Watu waliojitokeza kupima katika kipindi husika.
Watu walipima kwa hiari(VCT) ni 4,235 kati yao wanawake 3047 na Wanaume 1,188 walipima VVU na Wanawake 8,920.

Wanawake wajawazito 4,918 na Wenza 2,671 walipima VVU kati yao Wajawazito 557 na Wenza 338 waligundulika kuwa na VVU
Huduma ya kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto ni mojawapo ya njia inayotumika hapa wilayani. Huduma hii ni njia ya uhakika zaidi ya kujua hali ya maambukizi ya UKIMWI katika jamii na pia husaidia kuzuia maambukizi kwa watoto wanaozaliwa na wazazi wenye virusi vya UKIMWI kwani hupatiwa dawa husika.



Pia Jumla ya Watu 1,657 kati yao Wanaume 702 na Wanawake 955 walipatiwa huduma ya maalum ya Unasihi na upimaji VV (PITC) ambapo wenye VVU ni 605 kati yao Wanaume ni 245 na Wanawake ni 360

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Viashiria vya kiwango cha kuenea kwa kasi kwa UKIMWI vinaoneshwa pia na hali ya maambukizi ya magonjwa ya ngono.

Katika wilaya ya Njombe hali ya maambukizi ya Magonjwa ya ngono imekuwa ikiongezeka kwa kasi kubwa toka wananchi 2,247 waliotibiwa mwaka 1994 hadi wananchi 15,208 kwa mwaka 2006.

Kwa kipindi cha Januari –Septemba, 2010 Jumla ya Watu 2,507 walitibiwa magonjwa ya ngono kati yao Wanaume ni 957 na Wanawake ni 1550

Idadi kubwa ya watu wanaojitokeza kutibiwa Magonjwa mbalimbali yakiwemo ya Ngono inatokana na wananchi kuzingatia elimu inayotolewa kwa jamii. Hata hivyo hali hii inadhihirisha kuwa watu wengi bado hawajabadili tabia ya kufanya ngono isiyo salama, hii inatokana aidha na uelewa mdogo wa matumizi sahihi ya kondomu, upuuziaji, kutopatikana au kutokuwa na uwezo wa kununua kondomu au makusudi ya kutotumia kondomu.



Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Hali ya maambukizi ya Ukimwi ni kubwa katika Kata za Njombe Mjini, Makambako, Imalinyi, Ilembula, Mtwango, Mdandu, Lupembe na Kidegembye. Hali hii inadhihirishwa na kuwepo kwa wagonjwa wengii wa muda mref, watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI,Idadi kubwa ya watu wanaogundulikwa kuwa na Virusi vya UKIMWI na ongezeko kubwa la Watoto Yatima

Mheshimiwa Mgeni rasmi,
Sababu za Kata husika kuwa na maambukizi makubwa ya virusi vya UKIMWI ni;
Muingiliano wa Wageni wanaofuata huduma mbalimbali kama hospitali ya Ilembula, Biashara ya mbao, viazi, makampuni/mashamba ya chai katika miji na Vijiji vya Makambako,Ilembula,Lupembe nakadhalika.
Shughuli za kibiashara na ajira za kuhamahama kama mashamba ya chai, upasuaji mbao na viazi.
Baadhi ya Waganga wa Jadi wanawadanganya wananchi kuwa wanaouwezo wa tiba ya UKIMWI.
Imani za kishirikina za korogwa na baadhi ya wagonjwa wanaorudishwa nyumbani kutoka Miji mingine.
Kukosekana kwa uelewa sahihi wa UKIMWI miongoni mwa Jamii (Kuhudumia wagonjwa, kutobadili tabia juu ya ngono salama.
Mila na desturi ya Kutotahiri wanaume.




Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Huduma kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI :

Kwa mwaka 2009/2010 Halmashuri ya Wilaya ya Njombe imewezesha fedha Tsh.Milioni Tano kwa ajili ya mitaji ya miradi ya kiuchumi kwa Vikundi 10 vya WAVIU yaani Tumaini-Kidugala,Amani–Itunduma,Upendo-Ukalawa,PIUTA-Ulembwe,Twendepamoja-Ihang’ana,SemaUmasikiniBasi(SEUBA)-Makambako,Ngalinjele-Luduga,Tunajua-Iyayi na MaishaBora-Wangama.

ATHARI ZA UKIMWI WILAYANI NJOMBE

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Kutokana na athari za UKIMWI,
Wilaya ya Njombe inakabiliwa na ongezeko kubwa la Watoto Yatima wanaokadiriwa kufikia 12,000 katika Wilaya.

Jitihada za Wilaya kwa kushirikiana na wadau hususani Mradi wa Tunajali
(FHI) imefanya Utambuzi unaoshirikisha jamii wa Watoto wanaoishi katika Mazingira Hatarishi zaidi(WWMHZ) ambao umefanyika katika Wilaya kati ya Mwaka 2007-2010 umefanikisha kuwatambua Watoto Yatima na Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi zaidi ni kama ifuatavyo:


Mwaka H/W ya Njombe H/ Mji wa Njombe Jumla Kiwilaya
2009/10 Wav Was Jml Wav Was Jml Wav Was Jumla
2,521 2,341 4,862 1,920 2,116 4,036 4,441 4,457 8,898

Hadi sasa utambuzi wa Watoto Yatima na Wanaoishi katika Mazingira hatarishi Zaidi umefanyika katika Kata 13 za Halmashauri ya Mji na Halmashauri ya Wilaya ni Kata 10 tu kati ya Kata 36 umefanyika bado Kata 26 katika H/Wilaya ya Njombe ambapo Jitihada kwa kuwasilisha maombi ya fedha zinaendelea na kushirikisha Wadau wa ndani na nje yaani Mashirika yasiyo ya Kiserikali,Wizara za Afya na Ustawi wa Jamii na Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto ili kufanikisha utambuzi wa Watoto wote Wanaoishi katika Mazingira hatarishi wilayani Njombe.


Watoto yatima waliopata huduma Mwaka 2009/10 ni kama ifuatavyo:

Kwa mwaka 2009/10 Halmashauri ya Wilaya imetoa fedha Jumla ya Tshs. 16,200,000/= kwa ajili ya Watoto Yatima 324 kwa ajili ya mahitaji ya elimu katika Shule za Sekondari na Jumla ya Watoto 262(Wav. 132 na Wasichana 130) Wanaolelewa katika Vituo vya Ilembula ELCT,Kipengere RC,Kituo cha Tumaini-Ilunda ,Upendo Nyombo na Jumuiya ya Orphans Education Centre –Makambako wamepatiwa Jumla ya Shs.5.000,000/=(Milioni Tano)kwa ajili mahitaji ya kielimu na tiba kutokana na fedha toka Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania.

Pia Halmashauri ya Wilaya imeandaa gunia 5 za Mchele ,katoni 20 na mafuta ya kupikia ndoo 5 vyenye thamani ya Jumla Sh.1,025,000/=kwa Vituo vya Kulelea Watoto Yatima husika ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha jamii kutoa misaada kwa Watoto yatima wakiwemo wanaolelewa katika Vituo vya Watoto yatima.

Kadhalika kwa Mwaka 2009/10 Mashirika ya NDO-RC (Njombe Development Organisation) imetoa misaada ya vifaa vya elimu,afya na mahitaji muhimu kwa Watoto Yatima Jumla 6,074 yenye thamani ya Sh.228,054,750 na Shirika la TUNAJALI(FHI) limetoa msaada wa Jumla ya Watoto Yatima 2,463 na Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wamepatiwa misaada ya thamani Jumla Tsh.121,509,000

Pia Mradi wa ROADS –Makambako umetoa msaada kwa Watoto Yatima 1,738 kati yao Wavulana 798 kwa fedha Tsh 49,678,600/= na Wasichana 830 kwa kuwahudumia fedha za mahitaji ya shule,chakula,tiba, malazi na msaada wa kiasaikolojia na WAVIU 1,320 kati yao Wanaume 480 na Wanawake 840 kwa ajili ya huduma za chakula,matibabu na vifaa vya nyumbani vya thamani ya Sh 37,993,140/=

Jamii inapaswa kuhakikisha inawasaidia Watoto yatima na kuwahudumia Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na kwa kuanzisha mifuko maalum kila Kijiji mfano wa Mtaa wa Ubena Kata ya Ubena-Makambako kimeanzisha mfuko wa Yatima ambapo wananchi wamechangia Sh.Milioni Moja nab ado michango inaendelea hivyo kila Kijiji kinapaswa kuiga mfano huo.

Athari nyingine ni:
Kupungua kwa nguvu kazi na kupungua uwezo wa kiuchumi wa familia kutokana na wanafamilia kuuguza wagonjwa kwa muda mrefu.
Gharama kubwa kwa Serikali na jamii katika kuhudumia Watoto Yatima na Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
Mifarakano katika Familia na jamii kutokana na unyanyapaa.


CHANGAMOTO KATIKA KUPAMBANA NA JANGA LA UKIMWI.

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Serikali na Halmashauri kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali inafanya jitihada kubwa sana katika mapambano dhidi ya janga la UKIMWI hata hivyo tanakabiliwa na changamoto zifuatazo:-
Uchache wa vituo vya ushauri nasaha na upimaji wa VVU hususani maeneo ya Vijijini.
Uchache wa vituo vya huduma na kutoa tiba kwa Wagonjwa na Wato wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kutokana na ongezeko na muingiliano wa watu na ukubwa wa Wilaya.
Upungufu wa vifaa,dawa na vitendanishi (reagents) kwa ajili ya upimaji wa VVU
Upungufu wa watumishi hususani wa maabara katika vituo vya afya ambao wangesaidia upimaji wa VVU.
Ongezeko la wagonjwa wa UKIMWI kutokana na kushamiri kwa biashara mbalimbali katika Wilaya yetu sambamba na kuendelea kwa Mila na desturi potofu za ukeketaji wasichana, kutotahiri wavulana na wasichana wanaotarajia kuolewa kufanya ngono na watu wazima kwa nia ya kufungua njia ya uzazi.


MIKAKATI YA KUPAMBANA NA UKIMWI

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,

Halmashauri ina mikakati ifuatayo katika kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI:-
Kuongeza vituo vya ushauri nasaha,tiba endelevu na upimaji VVU hususani Vijijini ili kusogeza huduma hii muhimu karibu zaidi na Wananchi.
Kushirikiana na wadau mbalimbali waliopo Wilayani zikiwemo asasi zisizo za kiserikali kwa mfano AMREF, FHI-PROGRAMU YA TUNAJALI , SHIPO, GROWOYODA, Benjamin Mkapa Foundation,ENGENDER HEALTH, (JohnHopkins University)JPIEGO,SPW, PSI, CUAMM, NJODINGO , PADA, TY-SEDA nk. katika juhudi za kupambana na UKIMWI.
Kuendelea na juhudi za Kuhamasisha akinamama wajawazito na Wenzi wilayani kuhusu umuhimu wa kuanza kliniki mapema na kupimwa Virusi vya UKIMWI kama wana maambukizi ili wapatiwe dawa ya kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.
Kuendelea kutoa dawa za kupunguza makali ya VVU.
Kuhamasisha jamii katika Kata zote ili kuchukua jukumu la kutunza watoto yatima na watoto waishio katika mazingira magumu na hatarishi.
Kuendelea kuelimisha jamii njia ya kupambana na ugonjwa wa UKIMWI kwa kuimarisha kamati za Ukimwi za Wilaya, kata, vijiji na vitongoji vyake.
Kusimamia na kuendeleza mpango wa wilaya wa mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.
Kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS katika juhudi za kupambana na UKIMWI.
Kuhamasisha jamii kuacha mila za ukeketaji sambamba na kuhimiza wavulana/Waname kutahiri na watu wote kujitokeza kupima afya kwa hiari na kukomesha unyanyapaa katika Jamii