Wednesday, December 18, 2013

Anusurika kuuawa na majambazi wilayani kilosa

Mkazi wa manispaa ya wilaya ya kilosa mkoani morogoro,costa mwamba amenusurika kuuawa baada ya kushambuliwa kwa mapanga na watu wanaosadikiwa ni majambazi.


Akizungumzia tukio hilo mtendaji wa kijiji cha munisagara Donald mgulambwa amesema kuwa tukio hilo limetokea dec 17 mwaka huu majira ya saa nane usiku ambapo watu hao walifika nyumbani kwa bwana mwamba na kuvunja mrango kwa jiwe maarufu kama jiwe Fatuma.,
Amesema kuwa majambazi hao ambao wanasadikiwa kuwa ni wane baada ya kufanikiwa kuvunja mlango huo waliingia ndani na ndipo walipoanza kumcharanga kwa mapanga bwana mwamba pamoja na mkewe Chiku Salumu na kasha kufanikiwa kuchukua kiasi cha pesa shilingi laki nane.

Mgulambwa amesema kuwa baada ya majambazi kufanya uhalifu huo majeruhi hao walipiga kelele za kuomba msaada kwa majirani ndipo majambazi hao wakatokomea kusiko julikana.

Majirani wa eneo hilo walimkimbiza bwana Mwamba katika hospitari ya wilaya ya kilosa kutokana na majeruhi makubwa aliyoyapata huku mkewe akipelekwa katika katika zahanati ya kijiji hicho.

Tukio kama hili ni la pili kutokea katika kijiji cha munisagara ambapo viongozi wa kijiji viongozi wametoa taarifa katika kituo cha polisi wilani kilosa kwa uchungzi zaidi.

Thursday, December 12, 2013

VIKUNDI VYA POLISI JAMII VYAPEWA VITAMBULISHO WILAYANI KILOSA


Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya kilosa peter nsato [SP]Dec 12 ametoa vitambulisho kwa vikundi vya polisi jamii wilayani kilosa.

 Mgeni rasmi SP Peter Nsato akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa vikundi vya polisi jamii Wilayani Kilosa.
Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya kilosa peter nsato [SP] amevitaka vikundi vya polisi jamii wilayani humo kutenda kazi kwa uadilifu na kuwataka kufichua uhalifu punde unapotokea,Pia katika kuwapatia vitambulisho  wanavikundi hao wamepewa mavazi ya kujitambulisha kuwa askari [reflector]pindi wawapo kazini.
 Matanda Ally matanda akipokea mavazi ya polisi jamii kutoka kwa SP Peter Nsato mara baada ya kupokea kitambulisho

 Aidha mkuu wa kituo cha polisi wilaya ya kilosa [ASP]Antony mkwawa amesema kuwa jeshi la polisi limeamua kuanzisha uhamasishaji wa polisi jamii na ulinzi shilikishi lengo likiwa ni kupungunza uhalifu unaotokea katika jamii na kulinda mali za wananchi,Na kuongeza kuwa jeshi la polisi linauhaba wa polisi na kuwataka wananchi kushirikiana vizuri na polisi jamii hao ili kumaliza kabisa matukio ya kiharifu yanayotokea katika jamii.            
 
       
 Aliyesimama ni mkuu wa kituo cha polisi wilaya ya kilosa ASP Antony mkwawa na wapili Kushoto kwake ni SP  Peter Nsato.

Aidha katika risala iliyoandaliwa katika vikundi hivyo ambavyo ni UKOMBOZI ULINZI SHIRIKISHI Kutoka kata ya kasiki,MALIWASO ULINZI SHIRIKISHI kata ya mbumi na MTENDENI B ULINZI SHIRIKISHI,Wamelipongeza jeshi la polisi kwa kuwashirikisha wanajamii kwani imesaidia kuvumbua matatizo yaliyopo kwenye jamii.
                 Hata hivyo wamesema kuwa wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa vifaa vya kufanyia kazi kama vile tochi,usafiri,makoti kwa ajili ya mvua na kuliomba jeshi la polisi tarafa ya kilosa liendelee kuwahamasisha wadau mbalimbali katika maeneo yao kuvisaidia vikundi hivyo vya ulinzi shirikishi.

Monday, September 30, 2013

BREKING NEWS: MSANII MACK 2 B WA KUNDI LA WATEULE AMEFARIKI DUNIA


Breekking news ilitufikia mida hii ni kwamba Msanii Na Producer Wa Music Wa BongoFleva Na Reggae Mack Malik Simba Amefariki Dunia Dakika 50 Zilizopita. Kaka Wa Marehemu Msafiri Masharubu amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa Na Kuvimba Kwa Miguu Sana. Amefia Nyumbani Kwao Yombo. 
 
Mack Alikuwa Member wa Kundi la wateule na producer kwenye studio za Enrico Pale Sound Crafters.Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema, Amina!!!!!!!!!!!.
 

Saturday, September 7, 2013

MBUNGE WA MOROGORO MJINI MHESHIMIWA ABDUL AZIZ ABOUD AWATAKA WANAVYUO KUSHIRIKI MICHEZO MBALIMBALI NA KUEPUKANA NA TABIA HATARISHI



MBUNGE WA MOROGORO MJINI MHESHIMIWA ABDUL AZIZ ABOUD AWATAKA WANAVYUO KUSHIRIKI MICHEZO MBALIMBALI NA KUEPUKANA NA TABIA HATARISHI

Mbunge wa morogoro mjini mheshimiwa Abdul Aziz Aboud amewataka vijana na wanavyuo waliopo vyuoni kujishughulisha katika michezo ikiwa ni sehemu  mojawapo katika afya ya mwanadamu.

Akizungumza kwa niaba ya mbunge huyo katibu wake Bwana Mourice Masala  amesema kuwa michezo ni muhimu kwa vijana na hasa kwa wale waliopo vyuoni kwani huwafanya kuchangamsha miili yao na kuepukana na kujiingiza katika vitendo viovu mara baada ya masomo yao.

Masala ameyasema hayo wakati akifunga bonanza la michezo lililovishirikisha vyuo vya Mtakatifu Joseph na Chuo cha uandishi wa habari MSJ vyote vya mkoani Morogoro.

Pia amewahasa vijana wanachuo hao waliopo mafunzoni kuzingatia kwa makini mafunzo yao ili waweze kuyahitimu kwa ufanisi na kuachana na tabia mbaya ambazo zimekuwa zikifanywa na baadhi ya vijana ikiwemo kujjiingiza katika kutumia madawa ya kulevya.
Nao wanachuo hao walionesha ushiriki wao kikamilifu katika kushiriki kwao katika kufanya michezo mbali mbali ambayo baadhi yake ilishirikisha wakufunzi kutoka katika vyuo hivyo.

Na Beatrice Majaliwa
Morogoro

CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.



CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.

Chuo cha mtakatifu Joseph kilichopo mkoani Morogoro leo  kimefanya tamasha la michezo katika viwanja vya michezo vya chuo cha kilimo (Sua) kwa lengo la kuboresha michezo na afya za wananchuo kupitia michezo .

Michezo hiyo iliyoanza nyakati za asubuhi na kuhitimishwa saa kumi jioni ilihusisha pia wanachuo kutoka katika chuo cha  Morogoro school of journalism (MSJ) ambapo michezo ya mpira wa miguu,mpira wa pete,kuvuta kamba ,kukimbiza kuku,na mbio za mita mia nne kwa upande wa wanafunzi na wakufunzi wao kutoa katika vyuo vyote viwili.

Mechi ya mpira wa miguu kati ya timu ya St Joseph Morogoro na Chuo cha habari morogoro(MSJ) Iliyoisha kwa ushindi wa goli 3(MSJ)  kwa 1 St Josep (Picha na Beatrice Majaliwa) 


Tamasha hilo lilokuwa na lengo la kuwaweka wanafunzi katika hali nzuri kiafya ,kufahamiana na kuweka mahusiano na ushirikiano baina ya vyuo shiriki.

Akisoma hutuba kwa mgeni rasmi Rais wa wanachuo  kutoka katika chuo cha Mtakatifu Joseph bwana Emanuel  Kabakeza amesema miongoni mwa chanagamoto wanazokutana nazo katika michezo ni pamoja na upungufu wa vifaa vya michezo ambavyo huwafanya kushindwa kufanya michezo yao kikamilifu.

Akijibu risala hiyo wakati wa kufunga bonanza hilo  mwakilishi wa mbunge wa Morogoro mjini ,katibu wa mbunge huyo bwana Mourice Masala  amesema kwa upande wake amefurahishwa na tamasha hilo lilioandaliwa na chuo hicho na kusema kwa sasa chuo kimekuwa na umuhimu mkubwa katika manispaa ya morogoro.

Masala  amesema kuwa kwa sasa chuo cha mtakatifu Joseph kimekuwa mkombozi kwa vijana wengi  katika mkoa wa morogoro na mikoa mingine kwa ujumla ikiwa ni sehemu mojawapo ya kupata taaluma katika fani mbalimbali.

Katika kupunguza adha ya ukosefu wa vifaa vya michezo ofisi ya mbunge imetoa seti moja ya jezi ya mchezo wa mpira wa miguu na mpira mmoja wa mchezp wa pete kwa wasichana ili kuongeza ari ya michezo kwa wanachuo hao.

Thursday, September 5, 2013

CHEKA AKARIBISHWA KWA VURUGU BUNGENI,NGUMI ZACHAPWA.

 
Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.

VURUGU ZA BUNGE LA TANZANIA ZAWAKERA WANANCHI.

 
 
Baada ya kuibuka mvutano mkali bungeni jana, kati ya Naibu Spika, Job Ndugai na wabunge wa Kambi ya Upinzani, wasomi, wanaharakati, Chama cha Madaktari Tanzania (Mat), Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), vimesema kinachoendelea sasa ndani ya Bunge ni masilahi ya vyama vya siasa siyo taifa.

Tuesday, September 3, 2013

SERIKALI YAJIBU MAPIGO KWA MTANDAO WA KENYA ULIOANZA KUICHOKONOA TANZANIA


 
 Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari- (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza  na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam  kuhusu  mtandao wa kijamii wa nchini Kenya ulioituhumu  Serikali ya Tanzania.

Tuesday, April 16, 2013

NMB KANDA YA MASHARIKI YATOA MSAADA WA MADAWATI 38 YENYE THAMANI YA TSH MIL 2.5 KATIKA SHULE YA MSINGI MTYANGIMBOLE WILAYANI KILOMBERO

Zaidi ya
wanafunzi 80 wa darasa la nne na la
tano wa shule ya msingi ya
Mtyangimbole
iliyopo kijiji cha Ikule kata ya
Mngeta wilayani
Kilombero,wanasomea kwenye
banda la nyasi huku wakiwa
wamekaa chini.

HabariKwanza Blog imeshuhudia hali hiyo
wakati wa makabidhiano wa msaada
wa madawati
38 yenye thamani ya shilingi milioni
mbili na laki tano uliotolewa na
Benki ya
Nmb Kanda ya mashariki shuleni
hapo.

Akizungumzia
hali hiyo Mwalimu Mkuu wa shule
hiyo bwana Emanuely Njavike amesema
kuwa wamelazimka
kufanya hivyo kutokana na shule
hiyo kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa
kwani vyumba
vilivyopo kwa sasa ni
viwili ambavyo vinatumiwa kwa
kupokezana kwa darasa la kwanza,la
pili,la tatu
na la sita.

Mwalimu Njavike
amesema kuwa hali hiyo
imewafanya
wanafunzi kutohudhuria masomo
kikamilifu kutokana na miundombinu
ya shule hiyo
kuwa mibovu hususan kipindi hiki
cha masika ambapo maji hujaa
katika vyumba hivyo na kuwafanya
wanafunzi hao kusoma katika
mazingira magumu na hatarishi.

Naye mwenyekiti wa kitongoji cha
Mtyangimbole Bwana Sangalufu John
Kibonde amesema
kuwa wananchi wa kitongoji hicho
walijenga maboma mawili mara
mbili na
yakabomoka kutokana na mvua za
masika
zinazoendelea kunyesha baada ya
serikali
kuchelewa kumalizia maboma hayo
hali inayowakatisha tamaa wananchi
kuchangia
ujenzi wa shule hiyo.
Shule ya
Mtyangimbole yenye wanafunzi 195
kuanzia
darasa la kwanza hadi la sita
inakabiliwa na upungufu wa vyumba
vitano vya madarasa na matundu
nane ya vyoo.

Hata hivyo maafisa wa benki ya NMB na Mbunge wa viti maalumu kupitia
Chama cha demokrasia
na maendeleo chadema Mheshimiwa
Suzan Kiwanga wamesikitishwa na
hali hiyo na
kusema kuwa shule hiyo inahitaji
msaada wa hali na mali ili
kuwanusuru watoto
hao wanaosoma katika mazingira
magumu na hatarishi

Monday, April 15, 2013

AJINYONGA KUEPUKA MADENI

MTU mmoja aliyejulikana kwa jina la
Karimu Kamwenda(41) mkazi wa
Kitongoji
cha Michenga A kijiji cha Michenga wilayani Kilombero
amejinyonga usiku wa kuamkia
leo kwa kile kinachodaiwa ni kukwepa madeni.

Kwa mujibu Mwenyekiti wa Kijiji cha Michenga
Bwana Iddi Kamila ameiambia
habarikwanza
kuwa kwa maelezo ya Kaka wa
Marehemu huyo, kuwa Marehemu amejinyonga
kwa
kinachosadikiwa kuwa ni kuwa na
madeni mengi aliyokuwa akidaiwa na watu mbalimbali.

Jeshi la polisi Wilayani Kilombero
limethibitisha kuwepo kwa taarifa za
mkazi huyo kujinyonga.

Wakati huo huo kijiji hicho cha
Michenga kinataraji kusoma mapato
na matumizi
ya kijiji mwishoni mwa wiki hii kwa
muujibu wa Mwenyekiti wa kijiji hocho Bwana
Idi Kamila.

Bwana Kamila ameuambia mtandaao
huu kuwa vikao vya ndani
vitakapokamilika
hiii leo taarifa itawekwa hadharani
siku ya kusoma mapato na matumizi
hayo.

KINANA KUONGEA NA WAKAZI WA IFAKARA KESHO

Katibu Mkuu wa Chama cha
Mapinduzi Taifa Bwana
Abdurahaman Kinana kesho
anataji kufanya ziara ya siku moja
Wilayani Kilombero na kuzungumza
na
Wananchi katika eneo la stendi ya
Kwa Makali.

Katibu wa siasa na uenezi CCM
Wilaya ya Kilombero Bwana
Pellegrine Kifyoga
ameiambia Habarikwanza kuwa
lengo la ziara hiyo ni
kuhamasisha ,kuangalia
utekelezaji wa ilani ya chama hicho
na kukagua uhai wa chama na
jumuiya
zake.

Bwana Kifyoga amesema kuwa
Bwana Kinana atafungua mashina ya
wakereketwa
na miradi ya kijamii na baada ya
hapo atazungumza na wananchi
pamoja na
wanachama wa CCM katika mkutano
wa hadhara utakaofanyika saa tisa
alasiri
katika Eneo la Stendi ya Kwa makali
Ifakara Mjini.

Katika Ziara ya Katibu huyo wa CCM
atambatana na Viongozi wa CCM
TAIFA, Katibu
wa NEC Itikadi na uenezi Bwana
Nape Nnauye na Katibu wa Nec
Oganaizesheni
Taifa Bwana Mohamed Seif  Khatib.

Amewataka wanachama na wananchi
kwa ujumla kujitokeza kwa wingi
kuwasikiliza
viongozi hao na kupokea maelekezo
yatakayotolewa na viongozi hao
katika
mkutano huo ili waweze kuyafanyia
kazi zaidi

Friday, April 5, 2013

SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO

SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO .

JUMLA ya Fedha shilingi Bilioni 3 Milioni 396 na Laki 9 na Elfu 9 Mia 2 na Tano zitatumika kama Gharama ya Ujenzi wa  Skimu ya Umwagiliaji katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa Wilayani Kilombero.

Kwa muujibu wa Taarifa ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero juu ya Mradi wa Ujenzi wa  Banio na Mfereji wa Umwagiliaji imeeleza  kuwa fedha zilizopatikana mpaka sasa ni Milioni 510 Laki 2 na Elfu 61 Mia 3 na Sabini na Tano Huku fedha zinazohitajika kukamilisha Ujenzi wa Skimu zikiwa ni Bilioni 2 milioni mia 916 Laki 6 na Elfu Arobaini na Saba Mia 8 na Thelathini na Tatu.

Taarifa imefafanua kuwa kati ya fedha hizo shilingi Milioni 416 na Laki 4 Elfu Sitini na Saba na Mia 3 Sabini na moja zimetumika katika Ujenzi wa Miundombinu Mfereji Mkuu Mita 900, Mifereji ya Kati 3 Mita 925 na Maumbo mbalimbali 12.

 Sehemu ya ujenzi wa mladi wa umwagiliaji wilayani kilombero  
(picha na Henry Bernard Mwakifuna.)
Mradi huo utakaosaidia upatikanaji wa uhakika wa Chakula na ongezeko la Kipato kuondokana na Kilimo cha kutegemea Mvua utasaidia Kaya 1204.

Mradi huo wenye eneo la Ukubwa wa Hekta 675 umepitia hatua mbalimbali tangu  Mwaka 1975 ukiwa chini ya Wachina walioanzisha Kituo cha Mafunzo ya kilimo ukipitia hatua mbalimbali unataraji kukabidhiwa Mwishoni mwa Mwezi ujao.

Sunday, March 17, 2013

TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI KUIWINDA MOROCCO

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 17, 2013

TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI KUIWINDA MOROCCO

Taifa Stars imeanza kambi jana jioni (Machi 16 mwaka huu) ambapo wachezaji 14 kati ya 23 walioitwa wameripoti na kufanya mazoezi leo asubuhi chini ya Kocha Kim Poulsen.

Wachezaji walioripoti ni nahodha Juma Kaseja kutoka Simba na msaidizi wake Aggrey Morris wa Azam, Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba), Shomari Kapombe (Simba) na Salum Abubakar (Azam).

Wengine ni Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mrisho Ngasa (Simba) na Simon Msuva (Yanga).

Wachezaji Hussein Shariff, Issa Rashid na Shabani Nditi ambao timu yao ya Mtibwa Sugar jana ilicheza mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) mjini Turiani wataripoti kambini leo jioni.

Kikosi hicho kitakamilika Jumanne asubuhi baada ya wachezaji walio katika kikosi cha Azam nchini Liberia kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho kurejea nchini. Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemorasi ya Congo (DRC) wanatarajiwa kutua nchini kesho usiku.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/-

MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/-

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Ruvu Shooting na Yanga iliyochezwa jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 62,228,000 kutokana na watazamaji 10,929.

Viingilio katika mechi hiyo namba 146 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,336,764.95 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,492,406.78.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,289,880.48, tiketi sh. 4,136,390, gharama za mechi sh. 4,373,928.29, Kamati ya Ligi sh. 4,373,928.29, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,186,964.14, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 850,486.06 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 850,486.06.

WAANGOLA KUCHEZESHA MECHI YA STARS

WAANGOLA KUCHEZESHA MECHI YA STARS

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Angola kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Morocco (Lions of the Atlas).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ivory Coast ndiyo inayoongoza kundi hilo ikiwa na pointi nne na kufuatiwa na Taifa Stars yenye pointi tatu.

Mwamuzi wa mechi hiyo ni Helder Martins de Carvalho wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Inacio Manuel Candido huku Ricardo Daniel Cachicumi akiwa mwamuzi msaidizi namba mbili. Mwamuzi wa mezani (fourth official) ni Antonio Muachihuissa Caxala.

Waamuzi hao watawasili nchini saa 1.20 usiku Machi 22 mwaka huu kwa ndege ya Kenya Airways wakitokea Luanda, Angola kupitia Nairobi, Kenya.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa David Fani kutoka Botswana anatarajiwa kuwasili Machi 22 mwaka huu saa 1.45 usiku kwa ndege ya South African Airways.

Naye mtathmini wa waamuzi (referee assessor) Neermal Boodhoo kutoka Afrika Kusini atawasili nchini Machi 22 mwaka huu 1.45 usiku kwa ndege ya South African Airways.

Saturday, March 16, 2013

WATOTO WALEMAVU WA KITUO CHA BETHELEHEMU WILAYANI KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA

WATOTO WA KITUO CHA BETHELEHEMU KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA.

Wanawake wa kata ya Kibaoni Wilayani Kilombero wametoa msaada wa mbuzi wawili kwa ajili ya sikukuu ya pasaka kwa watoto walemavu wa akili wa kituo cha bethelehemu unaogharimu jumla ya shilingi 180,000.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo Mratibu wa kamati ya sherehe ya siku ya mwanamke duniani Bi Sophia Msiku amesema kuwa msaaada huo umepatikana baada ya wanawake hao kufanya harambee katika sherehe ya siku ya wanawake duniani.

Bi Msiku amesema kuwa katika kusherekea siku ya mwanamke duniani walipanga kushiriki na watoto hao lakini kutokana na mambo kuingiliana walishindwa kufanya hivyo na badala yake walipanga siku ya kupeleka msaada huo.

Akizungumza wakati akipokea msaada huo mlezi mkuu wa kituo hicho Sister Maria Dorothea Lyimo amewashukuru akina mama hao na amewataka watu wengine kuiga mfano huo kwa kutoa msaada huo kwa watoto hao .

Tuesday, March 12, 2013

WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU

WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU .

Wakulima wa vitongoji vya lipangalala,lihami,kwa mkuya na kiyongwile kata ya Ifakara Wilayani Kilombero wamelalamikia kucheleweshwa mbolea ya ruzuku  ambayo ilitakiwa kufika tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana.

Wakizungumza na Mtandao huu wa habarikwanza Baadhi ya wakulima wamesema kuwa pembejeo katika maeneo hayo zimechelewa kufika hali ambayo imewafanya wakulima hao kushindwa kuzitumia hasa zile za kupandia kutokana na muda kupita.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya kugawa vocha za pembejeo katika maeneo hayo Bwana Paulo Magehema amekiri malalamiko ya wakulima hao ambapo amesema kuwa mbolea hiyo ilitakiwa ifike mwaka jana lakini imefika mwezi machi mwaka huu  huku  mimea ikiwa imeshaota na kukua hivyo kwa upande wa mbolea ya kupandia haitafanya kazi yoyote.

Hata hivyo amesema pamoja na kucheleweshwa kwa mbolea hizo wakulima 300 watanufaika na mbolea hizo ambazo zimefika  chache ambazo hazitakidhi idadi ya wakulima waliotuma maombi ya kupatiwa mbolea hizo




WANAFUNZI WILAYANI KILOMBERO WAHIMIZWA KUONGEZA BIDII KATIKA MASOMO YAO KUEPUKA AIBU YA MATOKEO KATIKA MITIHANI YAO YA KUHITIMU

WANAFUNZI WILAYANI KILOMBERO WAHIMIZWA KUONGEZA BIDII KATIKA MASOMO YAO

Wanafunzi wilayani Kilombero wamehimizwa kuongeza bidii katika masomo ili wafanye  vizuri katika mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne na kuondokana na aibu ambayo taifa imepata  kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha nne  kwa mwaka 2012 kufeli.

Hayo yameelezwa leo na mbunge wa jimbo la Kilombero Mheshimiwa Abdul Mteketa wakati akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kata ya Kibaoni alipokuwa akitoa msaada wa vitabu 100 vya masomo ya hesabu,jiografia,kemia,fizikia na bailojia katika shule hiyo.

Mh,Mteketa amesema kuwa kufeli kwa wanafunzi wengi inatokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa vitabu ,walimu na baadhi ya wanafunzi kutokuwa na nidhamu hivyo amewataka   wazazi ,walezi na walimu kushirikiana  kikamilifu ili kuinua kiwango cha taaluma shuleni hapo .

Kuhusu baadhi ya wanafunzi kutokuwa na nidhamu kwa walimu na utoro,amesema suala la nidhamu kwa mwanafunzi ni ushirikiano kati ya wazazi na walimu na hivyo amewataka wazazi kuwa wakali kwa watoto wao pindi wanapokosea  badala ya kuwatetea , hali hiyo inasababisha wanafunzi wengi kutokuwa na nidhamu pindi wanapoona wanatetewa na wazazi wao.

Awali akizungumza wakati akipokea msaada huo kwa niaba ya shule mkuu wa shule hiyo  Bwana Zakaria Kalinga amemshukuru Mh Mteketa  kwa msaada wa vitabu 100 na amemuomba asichoke kuitembelea shule hiyo na kutatua changamoto zinazowakabili ili kuinua kiwango cha taaluma shuleni hapo.

Bwana Kalinga amesema shle hiyo inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vitabu,uchache wa samani za ofisi,uhaba wa walimu hasa wa masomo ya sayansi,ukosefu wa nyumba za walimu,ukosefu wa hostel na ukosefu wa vifaa vya michezo na fedha kwa ajili ya matengenezo ya uwanja .

Kuhusu vifaa vya michezo na matengenezo ya uwanja mbunge huyo  amewaahidi atahakikisha anatekeleza ahadi hiyo.

Monday, March 11, 2013

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA MSAADA WA VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA  VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE

MBUNGE wa Jimbo la Kilombero Mheshimikwa Abdul Mteketa ametoa msaada wa Vitabu 200 vya Masomo mbalimbali kwa Shule ya Sekondari ya Kiyongwile iliyopo Kata ya Ifakara.

Akizungumza na Wanafunzi na Walimu wa Shule  hiyo Wakati akikabidhi msaada huo Mheshimiwa Mteketa amewaeleza kuwa  Lengo  la msaada huo ni kuinua Taaluma na kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi  wa shule hiyo na pia ni moja ya kutekeleza ahadi ya kuboresha Elimu kwa shule za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Kilombero.

Amewataka Wanafunzi na Walimu kuvitunza Vitabu hivyo ili Viwasaidie wanafunzi waliopo kwa sasa na watakaokuja baadaye.
Msaada uliotolewa ni Vitabu vya Masomo ya Fizikia, Kemia, Jiografia, Baiolojia na Hisabati.

Mbali na Msaada huo Mbunge huyo ametoa Msaada wa Kalamu za Wino na Mkaa zenye Thamani ya Shilingi Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000/=)kwa shule ya Msingi ya Lipangalala huku akiwaahidi kujenga Vyoo na kuweka Maji katika Shule hiyo.

Mheshimiwa Mteketa ametoa ahadi hiyo baada ya uongozi wa shule hiyo kumweleza matatizo hayo likiwemo  na tatizo la Ukosefu wa Umeme shuleni hapo.










KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA MSAADA WA PIKIPIKI KWA JESHI LA POLIS WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75

KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA  PIKIPIKI KWA JESHI LA POLISI WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75 
 
Kituo Kidogo cha Polisi cha Mngeta kilichopo wilayani Kilombero kimepatiwa msaada wa pikipipiki moja aina ya bajaji Boxer yenye thamani ya shilingi 1,750,000 kutoka kampuni ya Kilombero Plantation Limited KPL.

Meneja Rasilimali watu wa kampuni hiyo Bwana David Lukindo amesema kuwa msaada huo umekabidhiwa hivi karibuni na mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bwana Cater Coleman.

Bwana Lukindo amesema kuwa kampuni imetoa msaada huo baada ya kutambua kituo hicho kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa usafiri na msaada huo na anaamini kwa kiasi kidogo watakuwa wamesaidia katika kuimarisha ulinzi katika tarafa ya mngeta.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa msaada wa pikipiki hiyo Mkuu wa kituo hicho Mkaguzi msaidizi wa Polisi Joseph Elias,ameishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na anawaomba wadau wengine kuiga mfano wa KPL.

Bwana Elias amesema kuwa jeshi la polisi linakabiliwa na changamoto nyingi hususan usafiri hali inayowafanya kushindwa kuwafikia wananchi katika maeneo mengi hivyo kupatikana kwa  usafiri huo utasaidia jeshi hilo kupambana na wahalifu kwa kuwafikia wananchi wengi ,ili kupunguza vitendo vya uhalifu katika tarafa ya mngeta.