Monday, September 30, 2013

BREKING NEWS: MSANII MACK 2 B WA KUNDI LA WATEULE AMEFARIKI DUNIA


Breekking news ilitufikia mida hii ni kwamba Msanii Na Producer Wa Music Wa BongoFleva Na Reggae Mack Malik Simba Amefariki Dunia Dakika 50 Zilizopita. Kaka Wa Marehemu Msafiri Masharubu amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa Na Kuvimba Kwa Miguu Sana. Amefia Nyumbani Kwao Yombo. 
 
Mack Alikuwa Member wa Kundi la wateule na producer kwenye studio za Enrico Pale Sound Crafters.Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema, Amina!!!!!!!!!!!.
 

Saturday, September 7, 2013

MBUNGE WA MOROGORO MJINI MHESHIMIWA ABDUL AZIZ ABOUD AWATAKA WANAVYUO KUSHIRIKI MICHEZO MBALIMBALI NA KUEPUKANA NA TABIA HATARISHI



MBUNGE WA MOROGORO MJINI MHESHIMIWA ABDUL AZIZ ABOUD AWATAKA WANAVYUO KUSHIRIKI MICHEZO MBALIMBALI NA KUEPUKANA NA TABIA HATARISHI

Mbunge wa morogoro mjini mheshimiwa Abdul Aziz Aboud amewataka vijana na wanavyuo waliopo vyuoni kujishughulisha katika michezo ikiwa ni sehemu  mojawapo katika afya ya mwanadamu.

Akizungumza kwa niaba ya mbunge huyo katibu wake Bwana Mourice Masala  amesema kuwa michezo ni muhimu kwa vijana na hasa kwa wale waliopo vyuoni kwani huwafanya kuchangamsha miili yao na kuepukana na kujiingiza katika vitendo viovu mara baada ya masomo yao.

Masala ameyasema hayo wakati akifunga bonanza la michezo lililovishirikisha vyuo vya Mtakatifu Joseph na Chuo cha uandishi wa habari MSJ vyote vya mkoani Morogoro.

Pia amewahasa vijana wanachuo hao waliopo mafunzoni kuzingatia kwa makini mafunzo yao ili waweze kuyahitimu kwa ufanisi na kuachana na tabia mbaya ambazo zimekuwa zikifanywa na baadhi ya vijana ikiwemo kujjiingiza katika kutumia madawa ya kulevya.
Nao wanachuo hao walionesha ushiriki wao kikamilifu katika kushiriki kwao katika kufanya michezo mbali mbali ambayo baadhi yake ilishirikisha wakufunzi kutoka katika vyuo hivyo.

Na Beatrice Majaliwa
Morogoro

CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.



CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.

Chuo cha mtakatifu Joseph kilichopo mkoani Morogoro leo  kimefanya tamasha la michezo katika viwanja vya michezo vya chuo cha kilimo (Sua) kwa lengo la kuboresha michezo na afya za wananchuo kupitia michezo .

Michezo hiyo iliyoanza nyakati za asubuhi na kuhitimishwa saa kumi jioni ilihusisha pia wanachuo kutoka katika chuo cha  Morogoro school of journalism (MSJ) ambapo michezo ya mpira wa miguu,mpira wa pete,kuvuta kamba ,kukimbiza kuku,na mbio za mita mia nne kwa upande wa wanafunzi na wakufunzi wao kutoa katika vyuo vyote viwili.

Mechi ya mpira wa miguu kati ya timu ya St Joseph Morogoro na Chuo cha habari morogoro(MSJ) Iliyoisha kwa ushindi wa goli 3(MSJ)  kwa 1 St Josep (Picha na Beatrice Majaliwa) 


Tamasha hilo lilokuwa na lengo la kuwaweka wanafunzi katika hali nzuri kiafya ,kufahamiana na kuweka mahusiano na ushirikiano baina ya vyuo shiriki.

Akisoma hutuba kwa mgeni rasmi Rais wa wanachuo  kutoka katika chuo cha Mtakatifu Joseph bwana Emanuel  Kabakeza amesema miongoni mwa chanagamoto wanazokutana nazo katika michezo ni pamoja na upungufu wa vifaa vya michezo ambavyo huwafanya kushindwa kufanya michezo yao kikamilifu.

Akijibu risala hiyo wakati wa kufunga bonanza hilo  mwakilishi wa mbunge wa Morogoro mjini ,katibu wa mbunge huyo bwana Mourice Masala  amesema kwa upande wake amefurahishwa na tamasha hilo lilioandaliwa na chuo hicho na kusema kwa sasa chuo kimekuwa na umuhimu mkubwa katika manispaa ya morogoro.

Masala  amesema kuwa kwa sasa chuo cha mtakatifu Joseph kimekuwa mkombozi kwa vijana wengi  katika mkoa wa morogoro na mikoa mingine kwa ujumla ikiwa ni sehemu mojawapo ya kupata taaluma katika fani mbalimbali.

Katika kupunguza adha ya ukosefu wa vifaa vya michezo ofisi ya mbunge imetoa seti moja ya jezi ya mchezo wa mpira wa miguu na mpira mmoja wa mchezp wa pete kwa wasichana ili kuongeza ari ya michezo kwa wanachuo hao.

Thursday, September 5, 2013

CHEKA AKARIBISHWA KWA VURUGU BUNGENI,NGUMI ZACHAPWA.

 
Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.

VURUGU ZA BUNGE LA TANZANIA ZAWAKERA WANANCHI.

 
 
Baada ya kuibuka mvutano mkali bungeni jana, kati ya Naibu Spika, Job Ndugai na wabunge wa Kambi ya Upinzani, wasomi, wanaharakati, Chama cha Madaktari Tanzania (Mat), Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), vimesema kinachoendelea sasa ndani ya Bunge ni masilahi ya vyama vya siasa siyo taifa.

Tuesday, September 3, 2013

SERIKALI YAJIBU MAPIGO KWA MTANDAO WA KENYA ULIOANZA KUICHOKONOA TANZANIA


 
 Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari- (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza  na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam  kuhusu  mtandao wa kijamii wa nchini Kenya ulioituhumu  Serikali ya Tanzania.