Monday, December 8, 2014

WANANCHI WA WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WATAKIWA KUWA MAKINI KWA KIPINDI HIKI CHA KUELEKEA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA KIJIJI KWA KUCHAGUA KIONGOZI ATAKAYEJALI MASLAHI YA WANANCHI



Mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amewataka wananchi wa wilayani kilosa kuwa makini kwa kipindi hiki cha kampeni kwa kuwachagua viongozi watakaojali maslahi yao. 
                                   Mkuu wa wilaya ya Kilosa Elias Tarimo akiwa ofisini kwake.

Ameyasema hayo December 8 mwaka huu wakati akizungumza na HABARIKWANZA  ofisini kwake kuhusiana na hali ya kampeni inavyoendelea wilayani kilosa na ameeleza kuwa hali ya kampeni inaendelea vizuri na kwa amani.
Mh:Mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo akiwa anaongea na HABARIKWANZA ofisini kwake

Aidha amewataka viongozi wanaofanya kampeni kutumia lugha nzuri zisizo za matusi kwani siasi haiendeshwi kwa matusi na amesema kuwa mwanasiasa anayetumia lugha chafu za matusi huyo hajakomaa kisiasa na hana sera ya kuwaambia wananchi ili wamchague.

Pia Tarimo amewataka wananchi kusoma katiba mpya ambayo inatakiwa kupigiwa kura na amewataka wananchi kuwa makini pindi zitakaposambazwa kwa kuweza kuipigia kura pasipo kushawishiwa na mtu au kikundi cha watu kitu  ambacho kitamfanya mwananchi kuipigia kura pasipo ridhaa yake (kushawishiwa) na amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuipigia kura katiba hiyo pindi muda wake utakapofika.

Monday, October 27, 2014

UJENZI WA MAABARA WAPAMBA MOTO



Diwani wa kata ya Ulaya Wilayani kilosa mkoani Morogoro Raimond Chengula amewataka wananchi kuendelea kuchangia ujenzi  wa maabara katika shule ya sekondari Ukwiva.
Wakwanza kushoto ni Diwani wa kata ya Ulaya Raimond Chengula wakatikati ni Afisa mifugo kijiji cha Mhenda piua ni mhasibu wa ujenzi wa maabara na wa mwisho ni Katibu Tarafa wa Tarafa ya Ulaya Raphael Mvurungu.

Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wananchi walipokuwa wanasomewa mapato na matumizi kuhusu ujenzi wa maabara ambao kwa sasa umefikia hatua ya msingi ambapo Mhasibu wa kamati ya ujenzi Juma Khassim amewasomea mapato na matumizi ya michango waliyoitoa  na kusema kuwa ujenzi huo ulitakiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 180 na baada ya wao kupiga mahesabu wameona  gharama hiyo imepungua na kufikia kiasi cha shilingi milioni 140 kutokana na kupungua kwa gharama mbalimbali za ujenzi ikiwemo matofari kupatikana kiurahisi.
Wananchi wakiwa wanapewa maelekezo na viongozi wao kuhusu ujenzi wa maabara unavyoendelea katika shule ya sekondari Ukwiva.

Naye katibu Tarafa wa Tarafa hiyo ya Ulaya Raphael Mvurungu amesema kuwa jambo la ujenzi wa maabara ni la kila mwananchi na ni manufaa ya kila mwananchi kwani kwa kufanya hivyo hadi kufikia miaka ya mbele kutakuwa na wataalamu wa sayansi wa kutosha na amechukua hatua hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungabo wa Tanzania Jakaya Kikwete kwa kuamua kujenga maabara kwa shule za sekondari.
                               wananchi wa kata ya ulaya wakiwa wanaangalia msingi wa maabara

Kwa upande wao baadhi ya wananchi waliokusanyika katika kikao hicho cha kusomewa mapato na matumizi Augustino Kikoti,Elia Dunia ,Asha Salehe na Abdallah Nassoro wameipongeza kamati ya ujenzi  kwa juhudi walizozifanya  hadi sasa na kutiwa moyo kwa kusomewa mapato na matumizi ambayo inaonyesha hali halisi ya fedha zao zilivyotumika na wameahidi kuendelea kuchangia ujenzi huo wa maabara hadi pale utakapokamilika
                                   kokoto ikiwa imekusanywa kwa ajili ya ujewnzi wa maabara

Wednesday, October 1, 2014

KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU CHA SIMAMA IMARA KWA KUPATIKANA KWA HAKI KWA KILA MWANANCHI



Kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC mwishoni mwa wiki iliyopita kimetimiza umri miaka 19 toka kuanzishwa kwake.
 Baadhi ya wasaidizi wa kisheria waliohudhulia katika sherehe za kutimiza miaka 19 ya kituuo cha kutetea haki za Binadamu LHRC Jijini Dar es salaam.
Katika sherehe hiyo ya kusheherehekea miaka 19 toka kuanzishwa kwake yaliyohudhuliwa na mgeni Rasmi Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania Jaji Joseph Walioba pamoja na viongozi mbalimbali kwa ngazi za kisiasa na kiserikali.
Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko Jaji Joseph Warioba akiongea wakati wa maazimisho hayo ya 19 ya kituo cha wasaidizi wa kisheria.

Katika sherehe hiyo ya kutimiza miaka 19 toka lianzishwe shirika hilo la kutetea haki za binadamu Walioba ameliomba shirika hilo kusimama imara kwa kuhakikisha kila Mtanzania anapata haki yake stahiki hasa

                 Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za Binadamu Bi,Helen Kijobi Simba
 kipindi hiki cha mchakato wa kupata katiba mpya amesema kuwa wananchi wanapaswa kutambua katiba ili inapofika wakati wa kuipigia kura wajue wanaipigia kura katiba ipi.
Wakwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Waroba akifuatiwa na Mkurugenzi wa kituo cha usaidizi wa kisheria Bi,Helen Kijobi Simba akifuatiwa na Askofu

Aidha Warioba amewataka wasaidizi wa kisheria kuwapa elimu wananchi waliopo vijijini na mjini ili kuhakikisha wananchi walio wengi wanajitambuana kutambua umuhimu wao katika jamii na Taifa kiujumla.
 Baadhi ya wasaidizi wa kisheria kutoka wilayani Serengeti wakipokea zawadi baada ya utendaji mzuri wa kazi zao
Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika hilo la kutetea haki za binadamu nchini Tanzania LHRC Helen Kijobi Simba amesema kuwa katika utendaji wao wa kazi wakiwa wasaidizi wa kisheria wanakumbana na changamoto nyingi ikiwemo wanasiasa kuingilia katika utendaji wao wa kazi na kuonekana wasaidizi wa 

Mwenyekiti wa chama cha CUF Prof;Ibrahim Lipumba[kushoto] akiwa na mmoja na wajumbe katika Tamasha la miaka 19 ya kituo cha sheria na haki za binadamu.


kisheria kama wapinga maendeleo na kuwa kikwazo jambo ambalo Bi,Simba amesema ni kikwazo kikubwa kwao katika ufanyaji wa kazi.
Inayoonekana kwa mbele ni keki iliyoandaliwa katika tamasha la kituo cha sheria na haki za binadamu. 

Aidha Bi,Simba amewataka wasaidizi wa kisheria kutokata tamaa katika kutetea haki za wananchi ambao hawajui hata pakuanzia.



KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO ASEMA UJENZI WA MAABARA UTAONDOKA NA MTU MADARAKANI.



Viongozi wa vijiji na kata wametakiwa kusimamia kwa juhudi ujenzi wa maabara tatu za sayansi katika shule za sekondari.
Katibu mkuu wa mkoa wa morogoro aliyevaa suti ya kijivu Elias Ntandu  akitoa maelekezo ya ujenzi wa maabara katika shule ya sekondari kutukutuakiwa pamoja na viongozi alioambatana nao katika ziara ya ujenzi wa maabara.

Hayo yamesemwa na Katibu tawala mkoa wa morogoro Elias Ntandu mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa ziara yake ya kutembelea shule 39 za sekondari katika wilaya ya kilosa ambapo amekagua ujenzi wa maabara katika shule hizo na kujionea hali halisi ambapo amesema kuwa shule nyingi  za sekondari 

              Viongozi wakiwa wanakagua maabara katika shule ya sekondari Mazinyungu iliyopo wilayani kilosa
hazijakamilisha ujenzi huo wa maabara ambalo ni tamko la mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete na kuongeza kuwa hadi kufikia mwezi wa kumi na moja 2014 maabara hizo 
Maabara ya Fizikia ambayo inatumika ya shule ya sekondari Mazinyungu iliyopo wilayani kilosa mkoani morogoro.

zinatakiwa kukamilika na kwa viongozi wa kijiji na kata wanatakiwa kukamilisha ujenzi huo mapema ya mwezi wa kumi 2014.
Diwani wa kata ya Mbumi Mama mbaruku akitoa maelekezo kwa viongozi kuhusu ujenzi wa maabara katika shule ya sekondari Mbumi iliyopo katika eneo lake la kiutawala.

Katika ziara hiyo ya kukagua ujenzi wa maabara iliyoambatana na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya kilosa Elias Tarimo,Katibu tawala wilaya Hilary Sagala Afisa mipango wilaya Lwidin Ngakoka 
 Baadhi ya viongozi wakiwa katika shule shule ya sekondari Mvumi kabla ya kwenda kukagua ujenzi wa maabara.
Afisa elimu sekondari wilayani kilosa Jonas Ntigoza pamoja na Afisa elimu Taaluma mkoa Raphael Pagala na 
viongozi wengine kutoka wilayani kilosa ambapo Mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amewataka 
Katibu Tawala mkoa wa Morogoro Elias Ntandu akiwa na mkuu wa Wilaya ya Kilosa Elias Tarimo wakiwa wanajumuika katika kuchimba shimo ambalo litatumika pindi maabara itakapokuwa tayari.

viongozi kupiga mahesabu vizuri kughusu ujenzi huo wa maabara ili pindi wanapotoa gharama ya uchangiaji kwa kila mwananchi kusiwe na utata  kwani ujenzi wa maabara unategemea nguvu ya wananchi.
Afisa elimu sekondari Jonas Ntigonza akiwa anaangalia ujenziwa maabara katika shule ya sekondari Gongwe iliyopo mvumi wilayani kilosa.

Aidha Tarimo amewataka viongozi wa kisiasa kuacha kuingilia shughuli za ujenzi wa maabara kisiasa kwani

                     Maabara ya shule ya sekondari Ludewa iliyokuwa hatua za mwisho za umaliziaji.
 jambo hilo la ujenzi si swala la kisiasa na kuwataka wananchi kujitoa kwa hali na mali ili kukamilisha ujenzi 
huo wa maabara kwa kila shule ya sekondari mapema ya mwezi wa kumi 2014.
Ujenzi wa maabara ukiwa katika ngazi ya uchimbaji wa msingi katika shule ya sekondari Mkulo Iliyopo wilayani kilosa mkoani Morogoro na viongozi wakiwa wanakagua ujenzi huo.


Mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo akiwa katika uwajibikaji kwa vitendo kwa kuchimba  msingi katika shule ya sekondari Kutukutu.