Wednesday, March 26, 2014

WILAYA YA KILOSA YANUFAIKA NA MRADI WA MKUHUMI KUHUSU KUPAMBANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA



Watafiti  kutoka chuo kikuu cha Sokoine SUA wamefanya utafiti Wilayani Kilosa katika mpango wa kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayetokana na ukataji miti ovyo na uhalibifu wa misitu (MKUHUMI) katika vijiji vitano vinavyotekeleza  mradi huo wilayani Kilosa.

Akizungumza katika mkutano wa wadau wa misitu wilayani Kilosa march 24 mwaka huu na wawakilishi wa vijiji hivyo mfadhili wa chuo kikuu cha Sokoine SUA Santos  Silayo amesema kuwa wameanzisha mradi huo kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya hali ya nchi  na mradi huo umeanzisha katika wilaya tatu ambazo ni Kilosa , Rungwe na Kondoa  lengo likiwa ni kuwaelimisha wananchi  juu ya matumizi bora ya ardhi

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Elias Tarimo amewaomba wahadhiri  na wasimamizi wa mradi huo wa MKUHUMI kuwaelimisha wananchi juu ya changamoto wa uharibifu wa misitu kwa kusema kuwa imeshamili maeneo mbalimbali ya wilaya ya Kilosa ambapo watu wanaharibu misitu hiyo na kutochukuliwa hatua kupitia sheria za hifadhi ya misitu katika vijiji hivyo na kuendelea na uharibifu wa misitu hiyo.

Aidha kwa upande wake Diwani kata ya Lumbiji  Herman Msafiri ameupongeza mradi huo wa MKUHUMI kwani wameweza kupata elimu kuhusu matumizi bora ya ardhi . Pia amesema kuwa wanaushukuru mradi huo kwa kuwaelimisha juu ya shughuli za mashambani kupewa elimu ya shamba darasa kwa kufundishwa mbinu za kilimo hifadhi na kilimo rafiki.

Monday, March 24, 2014

MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 11 ALAWITIWA WILAYA MVOMERO MKOA MOROGORO



Kijana mwenye umri wa miaka 21 Mkude Kulubuko anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 11 anayesoma darasa la tatu katika shule ya msingi tangini.Tukio hilo limetokea katika kijiji cha tangeni kata ya mzumbe, tarafa ya mlali , wilaya ya mvomero mkoani morogoro ambapo mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa hilo march 21 mwaka huu.
Akielezea tukio hilo babu wa mtoto aliye lawitiwa Charles Golaga amesema kuwa march 21 mwaka huu mjukuu wake alikuwa akicheza na watoto wenzake ndipo mtuhumiwa alipomrubuni na kwenda kumfanyia mnyama huo vichakani .
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha tangeni Joseph Peter ameeleza kuwa amedhibitisha kuwa mtoto huyo amelawitiwa baada ya kumpelekwa hospitalini na daktari kuweleza kuwa mtoto huyo amearibika sehemu zake za haja kubwa na anamatatizo ya kujisaidia ovyo.
Aidha  baba wa mtoto huyo John Kesi Gabriel amekili kwa kutokea kwa tukio hilo ambaye amesema mwanae anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa wa morogoro na hali yake anaendelea vizuri.
Aidha kwa upande wa Kamanda wa Polisi mkoa  Morogoro Faustine Shilogile alipotafutwa kulizungumzia tukio hilo amesema kuwa hana taarifa zozote kwani yupo kikazi nje ya mkoa morogoro.

Tuesday, March 18, 2014

SHULE ZA MSINGI WILAYANI KILOSA ZANUFAIKA NA MPANGO WA MATOKEO MAKUBWA SASA[BRN]



Mkuu wa shule ya msingi kilosa town wilayani kilosa mkoani morogoro mwalimu Edna Dungumaro ameupongeza mradi wa matokeo makubwa sasa [BRN]Kwa kuweza kuinua kiwango cha ufaulu katika sekta ya elimu.

Hayo ameyasema march 18 alipotembelewa na habarikwanza shuleni hapo na kusema kuwa kwa upande wa shule yake kwa mwaka jana 2013 matokeo yalikuwa mazuri kwa kufaulisha wanafunzi 67 kati ya wanafunzi 71 wa darasa la saba na kueleza kuwa changamoto inayomkabili katika shule hiyo ni wanafunzi kuwa watoro,Pia amesema kuwa shule yake imeshika nafasi ya kumi [10]kiwilaya.

Aidha Navy kareen Ndoeka ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika shule hiyo ya kilosa town ameushukuru mpango huo wa matokeo makubwa sasa [BRN]Kwani wameweza kupata elimu kwa kiasi kikubwa.

Naye Jaspine mswaki mwanafunzi wa darasa la saba katika shule hiyo ya kilosa town ameupongeza mpango huo mwa matokeo makubwa sasa [BRN]Pia amewaomba walimu kuendelea kuwafundisha kwa moyo ili wapate elimu iliyo bora.

Monday, March 17, 2014

MAFURIKO YAENDELEA KUWATESA WAKAZI WA KILOSA



Wakazi wapatao 228 wa kata ya magomeni kitongoji cha manzese wilayani kilosa wameathiliwa na mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali.

Akithibitisha kutokea kwa mafuriko hayo mwenyekiti wa kitongoji cha masanze Abdul Bona amesema kuwa mafuriko hayo yameingia siku ya jumamosi  ya tarehe 15 march mchana na kusema kuwa wakazi wa eneo hilo wameathiliwa sana kwa mafuriko hayo kwa baadhi ya nyumba kubomoka na nyingine kuingiliwa na maji,Pia amesema kuwa tofauti na maji kuingia kwenye makazi ya watu mafuriko hayo yameathiri mazao pamoja na mashamba.

Aidha mmoja kati ya waathilika wa mafuriko hayo Said mandundu amesema kuwa nyumba zilizobomoka ni nyumba za udongo ambaye naye ni mmoja wao aliyekosa mahali pa kuishi na kwa sasa akiwa amehifadhiwa na jirani yake.

Kwa upande wake mzee kambi kamtande ambaya naye ameathiliwa na mafuriko hayo amesema kuwa chanzo cha mafuriko hayo ni kutokana na mto mkondoa kutokuwa na muelekeo maalum na baadhi ya wakulima kulima pembezoni mwa mto huo.Pia amesema kuwa mafuriko hayo yameharibu mazao pamoja na mashamba kuingiliwa na mchanga ambao haufai kwa kilimo.

Thursday, March 13, 2014

WILAYA YA KILOSA KUNUFAIKA NA MLADI WA MAJI VIJIJINI.


Wakazi wa wilaya kilosa mkoani morogoro watanufaika na mradi wa maji safi na salama ifikapo june 2014 chini ya benk kuu katika vijiji kumi wilayani kilosa. 

 Mradi huo unagharimu takribani milioni 801 ukiwa na lengo la kuboresha maji vijijini ambapo kwa wilaya ya kilosa mradi huo utanufaisha vijiji vya tundu,msowero,iwemba,mabwegele,dumila,zombo lumbo,lumango,kifinga na mikumi.

Akizungumza na wanakijiji wa mabwelebwele march 13 mhandisi wa maji wilayani kilosa Hosea Mwingizi  amewataka wanakijiji kutoa ushirikiano katika ujenzi wa mradi huo na kuwafafanulia mambo mbalimbali juu ya mradi huo ambapo kwa kijiji cha mabwegele kuna ujenzi wa visima viwili 

Aidha katibu  katika kijiji cha mabwegele SOLOMON Ibrahimu ameupongeza mradi huo kwa kuwapatia fursa hiyo ya kuwapatia maji na kusema kuwa kijiji chao chenye wanakijiji 4600 hakina bomba hata moja na kuushukuru sana mradi wa benk ya dunia
Aidha mwandishi msimamizi wa mradi huo Leornad Msenyele amewaelimisha wanakijiji wa mabwegele juu ya mpango wa mradi huo wa maji katika ujenzi wake hadi utakapo kamilika 

Pia mhandisi wa maji wilayani kilosa Mwingizi amewataka wananchi hao kutumia vyanzo hivyo vya maji vizuri pindi utakapokamilika.