Wednesday, April 30, 2014

SERIKALI YATOA TANI 160 ZA CHAKULA NA SHILINGI MILIONI 60 KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO MULEBA MKOANI BUKOBA.


MBUNGE WA MULEBA KASKAZINI MHESHIMIWA MWIJAGE KUWASAIDIA WAPIGA KURA WAKE 

Serikali imetoa jumla ya tani 160 za chakula na fedha taslimu shilingi milioni sitini zimetolewa na Waziri mkuu Mizengo Peter  Pinda  kwa  waathirika wa mafuriko  yaliyotokea march 28  katika vijiji vya kata ya Ibuga Wilaya ya Muleba  Mkoani  Bukoba.

Vijiji vilivyoathiriwa na maafa  hayo makubwa ambayo yamesababisha nyumba takribani  150 kuezuliwa na upepo  na watu kukosa makazi na mazao kuharibika ingawa hakuna aliyekufa na kujeruhiwa  katika tukio hilo      

Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika ziara yake Mbunge wa Jimbo  la Muleba kaskazini mheshimiwa Mwijage amesema amesikitishwa sana baada ya kupata habari hizo kwani ni mara ya pili kutokea kwa maafa hayo,  kwa kuwa maafa kama hayo yalishawahi kutokea mwaka 2012 hivyo amewapa pole wanakijiji hao na kuwataka kutokata  tama kwa hali hiyo.    

Mheshimiwa Mwijage amesema baada ya kutembelea vijiji hivyo amebaini karibu nyumba 150 zimeezuliwa na upepo  na  baadhi familia kukosa makazi pamoja na mazao kuharibiwa vibaya hivyo ametoa bahasha kwa kila muathirika akidai kuwa ina misumari ndani yake na kuwakilisha msaada uliotolewa na serikali ikiwa ni tani 160 za chakula na msaada kutoka kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda na milioni 60 alizotoa kwa ajili ya kununua maharage kwa wanakijiji hao.    

Mwijage pia amewaahidi wanakijiji hao kuwa wataletewa mahindi ambayo  watauziwa kwa bei ya shilingi hamsini kwa kilo lakini pia ametoa misaada ya papo hapo kama fedha tasilimu kwa ajili ya malipo ya ada kwa wanafunzi walioshindwa kwenda shule kutokana na hali hiyo.Baadhi ya misaada mingine ni sare za shule,mabati kwa bahadhi ya wanakijiji ,na  kutoa tamko kwa wakuu wote wa shule kutokudai ada kwa wanavijiji hivyo mpaka itakapofika mwezi  November  mwaka huu na amechukua jukumu la kuwasomesha watoto wote waliofanya vizuri katika masomo yao ya kidato cha nne mwaka huu  .   
  
Akitoa angalizo kwa  wale ambao wamekuwa wakitumia maafa hayo kwa manufaa yao binafsi kwa kuomba misaada toka sehemu mbalimbali kwa kutumia jina la kijiji cha Buhembo bila kupata kibali maalumu kutoka katika uongozi maalumu  na kusema kuwa huo ni wizi na wenye tabia hiyo waache na kufuata utaratibu   unaohusika  
Wakipokea misaada hiyo nao wanakijiji wa vijiji vya kata ya Ibuga wamesema wanaishukuru  serikali kwa kuwapa misaada hiyo kwani wamekuwa katika hali ngumu sana na kumshukuru mbunge wa jimbo hilo kwa kuchukua jukumu la kuwasomesha watoto wao

Sunday, April 27, 2014

FUVU LA KICHWA CHA BINADAMU NA MIKONO YAMEONEKANA APRIL 26 KWENYE MTO WAMI WILAYANI KILOSA



Mabaki ya mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari kilosa aliyefahamika kwa jina la Protas masinde yameonekana April 26 katika mto wami rudewa
.
Akizungumzia tukio hilo mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amesema kuwa mtoto huyo amepotea tangu April10 ya mwaka 2014 na juhudi za kumtafuta hazikuzaa matunda.
Aidha Tarimo ametoa wito kwa wanafunzi kufuata maelekezo pindi wawapo shuleni kwa kueleza kuwa marehemu na weenzake wawili walitumwa kuchota maji iliyo salama lakini wao walienda sehemu nyingine na kusababisha madhara hayo.Pia ameongeza kwa kusema kuwa kutokana na miundombinu ya maji kuharibiwa na mto shuleni hapo na kuwalazimu wanafunzi kwenda kuchota maji mtoni kwa ajili ya shughuli mbalimbali pia Halmashauri ya wilaya ya kilosa imejipanga kukarabati miundombinu hiyo ili kuepusha usumbufu na upatikanaji wa maji shuleni hapo.

Pia Baba mkubwa wa mototo Raimond Tangaraza amesema wamesikitishwa sana na taarifa hiyo lakini amesema kuwa kazi ya mungu haina makosa na licha majonzi hayo anawashukuru viongozi,wananchi na majirani kwa msaada wao waliouonyesha katika utafutaji wa mwili huo wa mototo wao.

Aidha mwalimu mkuu wa shule hiyo Erasto Lulandara amesema kuwa mwanafunzi huyo amepatwa na umauti huo alipoenda kuchota maji akiwa na wenzake sehemu ambayo maji yanachemka na amesema kuwa ni sehemu yenye kina kirefu ndipo Protas alipotumbukiza ndooyake kwa ajili ya kuchota maji ndipo ndoo ikamtereza na na alipojaribu kuidaka ndipo alopotereza na kuzama majini.

Kwa upande wake shuhuda wa tukio hilo Saidi Ally amesema kuwa wamekuta mwili wa marehemu ukiwa ni vipandevipande abavyo ni fuvu la kichwa,mikono na sehemu ya mwili na kusema kuwa chanzo cha kugunduliwa kwa mwili huo watoto waliokuwa wanavua samaki katika mto huo ndipo walipounasa mkono wa marehemu na kuongeza kuwa wameukuta mwili huo ukiwa katika hali mbaya.

Naye mganga mkuu wa hospitari ya wilaya ya kilosa John Nkinda amethibitisha kuwa ameupokea mwili huo ukiwa katika hali ya vipandevipande majira ya saa 8 mchana ya April 26 na kueleza kuwa wameuhifadhi chumba cha kuifadhia maiti na wanawasubiri  ndugu wa motto huyo kuja kuchukua mabaki ya mwiliwa marehemukwa ajili ya shughuli za mazishi.

Aidha kamanda wa polisi mkoa wa morogoro Paulo Leornad amesema kuwa amepokea taarifa hizo april 27 na kuahidi kutolea maelezo April 28 mwaka huu.

MASHINDANO YA MAIMOSI MKOANI MOROGORO KITAIFA KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI MOHAMED ABDULWAKILY AWAPONGEZA FABIAN NA MARIAM KWA USHINDI WA MBIO NDEFU KATIKA MAIMOSI KITAIFA MKOANI MOROGORO (CROSS COUTRY)

MASHINDANO  YA  MAIMOSI  MKOANI  MOROGORO  KITAIFA:

Na Jonathan  Tossi - Jeshi  La  Polisi.

Katibu  mkuu wa  wizara  ya  mambo  ya  ndani  nchini  Mohamed  Abdulluwakily   amewapongeza  wanamichezo wa  wizara  hiyo  na kuwaaasa kuwa   michezo  nisehemu  ya   kazi  hivyo  waendelea  kushiriki  michezo  hiyo  kwa  hali na  mali. Pia  amesema  kinachoitajika  sasa  ni kuunda  timu moja kutoka idara  za  wizara  ya  mambo  ya  ndani  ya  nchi   na kuwa  na   timu  moja  ya  wizara.

Saturday, April 26, 2014

WANANCHI WATAKIWA KUTUNZA MISITU WILAYANI KILOSA



Afisa Misitu wa Wilaya ya Kilosa Othman Haule ameitaka Serikali kuwekeza  katika sekta ya mali asili na misitu kwani ni sekta nyeti nchini.

Ameyesema hayo ofisini kwake wakati akizungumzia jinsi misitu inavyoathiliwa na wananchi kwa matumizi ya Kila siku na kusema kuwa chanzo cha misitu hiyo kuharibika ni kutokana na serikali kutoipa kipaumbele sekta hiyo ya maliasili na kusema kuwa changamoto  inayowakabili ni baadhi ya wananchi kutokujua umuhimu wa misitu na kuitumia vibaya kwa uchomaji mkaa hovyo kilimo ndani ya misitu , pamoja na ufugaji horela na kutolea  mfano  msitu wa mamiwa kisara North ulivyohalibiwa kwa shughuli za Kilimo pamoja na misitu ya Gairo ilivyoharibiwa kwa Ufugaji horela wa mifugo na uchomaji wa mkaa na kusababisha eneo hilo kuwa jangwa.

                                         misitu ya maguha wilayani gairo jinsi ilivyoathiliwa na ufugaji horela.

Pia amewaasa wananchi wanaokaa pembezoni mwa misitu kuacha kufanya shughuli za uhalibifu wa msitu ikiwemo uchomaji moto kwa ajili ya uwindaji shughuli za kilimo  pamoja na uchomaji wa mkaa. Na kuongeza kwa kusema kuwa anawataka wananchi kuitunza vizuri misitu ili kuweza kuendelea  kupata mvua kwa wingi na kuondokana na mabadiliko ya hali ya hewa yaliyopo kwa sasa. 
 













Tanki la maji likiwa likiwalimekauka kutokana na ukame uliopo sehgemu hiyo uliotokana na ufugaji horela na uchomaji wa mkaa.
 Mashamba yakiwa katikati mwa msitu wa mamiwa kisara North kata ya lumbiji wilayani kilosa.
Aidha amesema kuwa kila mwananchi anajukumu la kutunza misitu kwa kusema kuwa mwananchi anapoona magunia ya mkaa barabarani akae akitambua kuwa kuna misitu imeteketea na kusisitiza kuwa kila mwananchi anapaswa kuwa mlinzi wa mwenzake.
  
 biashara ya mkaa maguha yazidi kuteketeza misitu wilayani gairo

Wednesday, April 23, 2014

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA KILOSA AWATAKA MADEREVA KUFUATA KANUNI NA TARATIBU ZA BARABARANI.



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Masalu Mayaya amewataka madereva wanaoendesha vyombo vya moto kufuata kanuni na taratibu ya barabara.

Ameyasema haya wakati akizungumza na HABARIKWANZA  kuhusu  ujenzi wa uzio wa Shule ya  Msingi  Mazinyungu ambao unagharimu kiasi cha shilingi milioni miamoja arobaini na saba miambili themanini na tano na mia nane thelathini elfu na kusema  kuwa ujenzi huo kwa sasa upo kwenye utaratibu na kusema kuwa bado hakuna fungu la fedha kwa ajili ya ujenzi huo kwa sasa na kuwaomba wadau kujitokeza kwa ajili ya kuweza kufanikisha shughuli za ujenzi huo.

Pia Mayaya amesema kuwa kutafanyika utaratibu kwa ajili ya kuweka matuta katika eneo hilo la shule ya msingi mazinyungu ili kuzuia kutokea kwa ajali eneo hilo, pia ameongeza kwa kusema kuwa madereva waendelee kupewa elimu kuhusu matumizi ya barabara.

Naye Mkuu wa Shule hiyo  ya Msingi Mazinyungu Lameck Mkude amesema kuwa shule hiyo inakitengo maalumu cha watoto walemavu wapatao 74 wavulana 44 , wasichana 30 amesema kuwa wanahitaji uzio kwa ajili ya usalama wa watoto hao na mali zao. Pia Mkude amesema kuwa pindi ujenzi wa uzio huo utakapokamilika utafanya mali za shule na watoto hao kuwa salama kutokana na baadhi  ya watu wasiokuwa na nia njema na watoto hao. Na kuongeza kuwa kitengo hicho cha watoto walemavu kuna watoto wenye ulemavu wa ngozi (albino) ambapo kuna baadhi ya watu  kuwa na imani potofu.

Tuesday, April 15, 2014

AFARIKI DUNIA AKIJARIBU KUVUKA MTO WILAYANI MVOMERO MKOANI MOROGORO.



Mkazi  wa kijiji cha manembo kitongoji cha Mng’ongo wilaya mvomero mkoani Morogoro Theresia Herry mwenye umri wa miaka 80 amefariki baada ya kusombwa na maji katika mto mseleleko mwishoni mwa wiki hii.

Akizungumzia mazingira ya kifo hicho mtoto wa marehemu Martin Cosmas amesema kuwa mama yake alienda shamba siku ya ijumaa akiwa ameongozana na Dada yake Serapia Cosmas na baadaye walipokuwa wanarudi walipofika mtoni Bi, Theresia alipokuwa anajaribu kuvuka  alisombwa na maji hayo na mwanaye aliyekuwa naye alipojaribu kumuokoa alishindwa kutokana na maji hayo kuwa na nguvu na ndipo marehemu alipokutwa na umauti huo.

Aidha mmoja wa  shuhuda wa tukio hilo Charles Golaga amesema kuwa wameshtushwa na kusikitishwa  sana na msiba huo kwa kusema kuwa marehemu alikuwa hajaumwa na alikuwa anatoka shamba ndipo akakutwa na umauti huo.

 Naye mwenyekiti wa kijiji cha mng’ongo amethibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mto huu ni mara ya kwanza kusababisha tukio hilo na kuongeza kwa  kusema  kuwa anawataka wananchi kuwa makini  na maji yanayotiririka mtoni na kuacha tabia kujaribu kuvuka maji yenye kina kirefu na yenye kasi.
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoani Morogoro Faustine Shilogile amesema kuwa tukio hilo bado halijawafikia na kuahidi kulifuatilia.