Thursday, January 9, 2014

Mbunge wa jimbo la kilosa atembelea miradi mbalimbali katika jimbo lake

        Mbunge wa jimbo la kilosa Mustafa Haidi mkulo amefanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezajiwa miradi ya maendeleo katika kata za Lumuma na kidete wilayani klilosa.
        Akiwa katika ziara hiyo,Mkulo aliongozana na katibu wa wazazi wilaya  Abdul Gombe na wataalamu mbalimbali kutoka wilaya ya kilosa.
         Katika kata ya kidete Mbunge mkulo amekagua mradi wa ujenzi wa bwawa la kidete ambalo hadi sasa halijakamilika tangu mwaka 2010 ulipoanza,Sababu ikiwa ni kutowaingizia pesa inayosimamia mradi huo wa ujenzi wa bwawa.
         Aidha amekagua mradi wa uchongaji wa barabara wa lumuma-kibasingwa yenye urefu wa kilometa nane ambayo imechongwa kilometa sita hadi sasa barabara hiyo imechongwa na mfuko wa jimbo wa mkulo,ambapo mbunge huyo ameahidi kutoa fedha kwa ajili ya kumalizia kilometa mbili zilizobaki.
Mbunge mkulo amefanya ziara hiyo January 6 n January7 ambapo pia ameweza kutembelea mradi wa barabara ya lumuma Mnozi ambayo haijakamilika hadi sasa na mbunge huyo ameahidi kuwa barabara hiyi itaanza kuchongwa mapema hivi karibuni.
         

Friday, January 3, 2014

HALMASHAURI YA KIJIJI CHA CHANZURU KINATARAJIA KUKUSANYA MILIONI THELATHINI NA MOJA LAKI TATU NA AROBAINI ELFU



Halmashauri ya kijiji cha chanzuru wilayani kilosa mkoani morogoro inatarajia kukusanya kiasi cha shilingi milioni Thelathini na moja laki tatu na arobaini elfu kwa ajili ya maendeleo ya kijiji.
Hayo yamesemwa mapema mwanzoni mwa wiki hii na mtendaji wa kijiji hicho salumu kibugula wakati akiongea kwenye mkutano wa wananchi na viongozi wa kijiji hicho alipokuwa akisoma bajeti ya mapato na matumizi ya nusu ya mwaka wa fedha 2013/2014.
Kibagula amesema kuwa katika bajeti hiyo ya mwaka wa fedha 2013/2014 kijiji kinatakiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni ishirini na moja laki tatu na Arobaini kupitia vyanzo vyake vya ndani na shilingi milioni kumi kutoka kwa wahisani na ruzuku ya halmashauri ya wilaya kilosa.
Katika mkutano huom pia kumejadiliwa mgogoro wa mashamba kati ya mwekezaji aliyefahamika kwa jina la Bahamisi na wananchi wa kijiji hicho kuhusiana na mipaka iliyowekwa na idara ya ardhi wilayani kilosa

VIJANA WATAKIWA KUUNDA VIKUNDI ILI WAPATE MIKOPO KIURAHISI



Mbunge wa jimbo la mikumi mkoani morogoro Abdulsalama Amer amewataka vijana waendesha pikipiki za kubeba abiria maarufu kama bodaboda kuunda vikundi ili waweze kupatiwa mkopo wa pikipiki zitakazowawezwsha kujikwamua kiuchumi.
Abdulsalama maarufu kwa jina la sas gesametoa wito huo kwa vijana wa jimbo lake la mikumi wakati alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha kitete msindazimapema wiki hii wakati wa ziara yake kwenye kijiji hicho kilichopo kwenye kata ya Ruhembe wilayani kilosa.
Sas gas amesema kuwa tayari ameshafanya mazungumzo na kampuni husika itakayotoa mikopo hiyo na sasa kinachosubiriwa ni vijana hao kuunda vikundi na kufuata taratibu zinazotakiwa ili waweze kukopeshwa.
Mbunge huyo amesema mikopo hiyo itawasaidia vijana hao kupata pikipiki na wataweza kuacha kuendesha pikipiki za matajiri wao na kuendesha za kwao kitu ambacho kitawasaidia kijikwamua kiuchumi.
Wakiongea vijana hao wamesema kuwa wanampongeza mbunge wao kwa jitihada hizo kwani watakapokopeshwa hizo pikipiki zitawasaidia kupata pesa na kuweza kutimiza ndoto zao za maisha bora kwa upande wao.