Wednesday, May 21, 2014

VIKUNDI VYA WAJASILIAMALI WANUFAIKA NA MAFUNZO YA WORLD VISION



Shirika la world vision lililoanzishwamwaka 1959 nchini marekani na kuingianchini Tanzania mwaka 1980 lenyelengo la kuleta ustawi wa motto kuwa na maisha mazuri, Afya njema na kumjua mungu , May 20 mwaka huu limetoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vikundi vya vikoba wilayani kilosa.

Katika mafunzo hayo yaliyohudhuliwa na wajumbe kutoka katika vikundi mbalimbali katika kutoa mafunzo hayo wamewezeshwa jinsi ya kuendesha vikundi vyao na taratibu na kanuni za kufuata katika kuendesha vikundi vyao.
NayemenejawamradiwaUlaya ADP katikashirikala  world vision Mathias Mwingila amesema kuwa katika kutoa mafunzo hayo 

                             MWEZESHAJI AKITOA MAFUNZO YA UJASILIAMALI KATIKA UKUMBI WA MANYOVU - KILOSA
Wanakumbana nachangamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya wanavikundi kudai posho wakati wanapoitwa kupewa mafunzo na kusema kuwa lengo la world vision nikutoa mafunzo ya kuweza kujikwamua kimaisha na kuleta maendeleo katika jamii.

Aidha ameongeza kuwa changamoto nyingine ni mapokeo hasi kwa baadhi ya wajumbe wakidhani kuwa world vision inaeneza dini ya kikristo kutokana na shirika hilo kuanzishwa na watu wa dini ya kikristo na amebainisha kuwa shirika hilo halipo upande wowote wakidini ila lipo kwaajili ya kutoa mafunzo ya kujikwamua kimaisha kwa wajasiriamali wadogowadogo.

 WANAVIKUNDI WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA MAFUNZO .
Nameongeza kuwa mradi huo kwasasa upo katika tarafa ya ulaya na Magole na utachukua muda wamiaka kumi na mitano na mikakati waliyojiwekea nikuhakikisha wajasiriamali na wananchi kwaujumla wanapata maendeleo kwa haraka.

Pia mwezeshaji katika semina hiyo Agripina P. Mtende amewataka wanavikundi hao kuwa na nidham ya fedha pindi wanapokopa katika vikundi vyao. 



Baaadhi ya wanavikundi hao Mwanaharusi Athumani, Donard Kusema na Stamili Shabani Kiwanga wamesema kuwa wameshukuru kwa shirika hilo  la world vision kwa kuwapatia elimu hiyo juu ya uendeshaji wa vikundi vyao.

Tuesday, May 20, 2014

WADAU WA ELIMU WATAKIWA KUFUATA KANUNI NA TARATIBU ZA ELIMU KATIKA KUANZISHA SHULE

Mkaguzi mkuu wa shule wilayani kilosa Ally Abdulhaman amewataka wadau wa elimu kufuata kanuni na taratibu za kuanzisha shule pamoja na vyuo.

Ameyasema hayo ofisini kwake wakati akizungumzia usajili wa Snai Media school iliyopo manzese wilayani kilosa na kusema kuwa shule hiyo haikusajiliwa tangu ilipoanzishwa mwaka 2009 na kusema kuwa walishatoa maelekezo kwa mmiliki wa shule hiyo kuwa ataje usajili wa shule hiyo mapema na kuongeza kuwa shule hiyo iliamuliwa kufungwa na mkaguzi wa mkoa mnamo tar 31 january lakini shule hiyo bado inaendelea kutoa mafunzo hayo ya elimu.

Aidha amesema kuwa wahisani hao huanzisha shule hizo kwa kupitia ofisi ya ustawi wa jamii yaani child care lakini ndani yake hutoa elimu ambapo ni kinyume na taratibu na sheria na kubainisha kuwa watoto kuanzia umri wa miaka 0 hadi 4 ndio wanaotakiwa kuwa kwenye child care na wanapofikia umri wa miaka 5 huyo anakuwa na umri wa kuanza elimu ya awali.

Naye mkurugenzi wa Snai media school Mery Paul Komba amesema kuwa shule yake ipo kwenye mchakato wa kuisajili likini pia amesema kuwashule hiyo bado ipo chini ya ustawi wa jamii na wapo kwenye mpango wa kuisajili lakini serikali inawapelekesha haraka na wanashindwa cha kufanya kwa sababu wanachanganywa na kuongeza kuwa swala la kufungwa kwa shule hiyo limewaumiza sana wazazi wenye watoto katika shule hiyo na kueleza kuwa elimu wanayoipata watoto katika shule hiyo ni nzuri na wanaumizwa wanapooona shule hiyo inataka kufungwa.

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa lengo la kuanzisha shule hiyo ni kutokana na kuona kiwango cha elimu kinashuka na changamoto kubwa na swala la lugha ya kiingereza.

Nao wanafunzi katika shule hiyo ya Snai media school shurut palma na careen fredy wamesema kuwa changamoto inayowakabili shuleni hapo ni kutokuwepo maji kalibu pia vyoo kutofanyiwa usafi ulio sahihi kwa usalama wao.

Monday, May 19, 2014

UKAWA WAITIKISA KILOSA

Umoja wa katiba ya wananchi [UKAWA]Wameendelea kuwahamasisha wananchi juu ya umuhimu wa katiba na ukawa walivyojitoa kwenye bunge maalum la katiba wakipinga mabadiliko yanayotarajiwa toka kwa kamati na kanuni,wakidai kuwa yanaenda kinyume na azimio lililopitishwa na bunge hilo kwa kuleta maridhiano. 

Akiongea katika mkutano ulioitishwa na UKAWA katibu wa chama cha CUF wilayani kilosa Sudy muhombolage amesema kuwa sababu ya ukawa kujitoa katika bunge maalum la katiba ni Lugha za kibaguzi,Vitisho vilivyojitokeza katika bunge maalum la katiba pamoja na kuchakachua kwa rasimu ya katiba kwa baadhi ya wajumbe wa bunge hilo la katiba.



Naye kamanda wa chama cha demokrasia na maendeleo [chadema] mkoa wa morogoro Abdalah Hamisi amesema kuwa msimamo wa Ukawa ni serikali tatu na kuwahamasisha wananchi juu ya umuhimu wa serikali tatu,Pia ameongeza kwa kusema kuwa Ukawa wanania nzuri na wananchi lakini kuna baadhi ya vyama wanamsimamo wa kivyama na ndio wanaosababisha mgogoro bungeni kwa kupingana na maoni ya wananchi ambayo yalikusanywa na Tume ya mabadiliko ya katiba

Saturday, May 17, 2014

WANACHAMA WA DECI WAENDELEA KULALAMIKIA SERIKALI KUHUSU PESA WALIZOZULUMIWA



Waliokuwa  wanachama wa chama cha kupanda  na kuvuna DECI Wilayani Kilosa wameoiomba serikali iwarejeshee pesa zao kama ilivyowaahidi au itoe tamko lolote juu ya pesa zao ili wafahamu kinachoendelea.

Wakizungumza na HABARIKWANZA baadhi ya wanachama hao wamesema serikali  imekaa kimya kwa muda mrefu kitu ambacho kinawapa wasiwasi wa kurejeshewa pesa zao kama serikali ilivyowaahidi.

Mmoja wa wanachama hao Nassoro Machengo ambaye alipanda zaidi ya milioni moja amesema baada ya serikali kuthibitisha na kuifungia taasisi hiyo na kuipeleka mahakamani ili ahidi kurejesha pesa kwa wananchi waliopanda ambacho wanavielelezo mara tu kesi hiyo itakapokamilika .

Machengo amesema wanashangazwa na ukimya wa serikali wakati kesi imeshakamilika na serikali imeshindwa kufanya hivyo wanaomba serikali iwarudishie pesa kama ilivyo ahidi au itoe tamko lolote juu ya kinachoendelea kwa kukaa kwao kimya kinawapa wasiwasi na kuhisi kuwa hawatapata tena pesa hizo .

Takribani miaka 7 iliyopita kuiibuka taasisi ya kifedha ya DECI iliyokuwa ikijiendesha katika utaratibu wa kupanda na kuvuna pesa ambapo wananchi mbalimbali waliwekeza pesa kwa  lengo la kuvuna pesa zaidi , lakini taasisi hiyo ilikuwa ikiendeshwa kinyume na taratibu za kisheria hivyo serikali ilisimamisha kufanya shughuli hizo huku ikiwa imekusanya  mabilioni ya watanzania.

Friday, May 16, 2014

SHIRIKA LIISILO LA KISERIKALI PARALEGAL CENTER LATOA MAFUNZO YA HAKI ZA BINADAMU WILAYANI KILOSA



Shilika lisilo la kiselikari morogoro paralegal center kwa ufadhili wa shirika la Legal Fund [LSF]Limehitimisha mafunzo ya kisheria kwa muda wa siku tano tangu May 12, 2014 hadi May 16, kwa watu 25 wilayani kilosa lengo likiwa ni kutoa mafunzo msaada wa kisheria kwa jamii masikini ambayo haiwezi kumudu gharama ya wakili.

Baada ya mafunzo hayo naibu wa wasaidizi wa kisheria wilayani kilosa[kilosa paralegal Association]Wilfredy Sumari amewataka wahitimu wote waliopata mafunzo mafunzo hayo ya haki za binadamu kujituma katika kutetea haki za wananchi hasa waishio vijijini na kuongeza kuwa anawaomba wananchi kuwapokea vizuri watetezi hao na kuwatumia kwa sababu wapo kwa ajili yao.

Nao baadhi ya wahitimu hao wa mafunzo ya kisheria ya haki za binadamu Sophia Paul,Ramadhan Hassan,Stella Venus na Henry Lembele wamelipongeza shirika hilo kwa kuwapatia elimu hiyo na kusema kuwa waliyofundishwa ni hali halisi ambayo ipo kwenye jamii na wameahidi kufanya kazi bega kwa bega na wananchi,Pia wamezungumzia baadhi ya mafunzo waliyoyapapata ni pamoja na Ukatili wa kijinsia,Wosia,Talaka pamoja na dhana ya ndoa hizo ni mada chache kati ya walizojifunza zinazoisumbua jamii na jamii kutotambua haki yao kwa kuipata.

Thursday, May 15, 2014

UCHAGUZI SIMBA WAIVA.

KUMEKUCHA SIMBA ,UCHAGUZI NAFASI YA  UJUMBE,MKAMBALLAH KUKGOMBEA NAFASI YA UJUMBE
 
 
Mweka hazina wa tawi la mpira pesa la magomeni mikumi bwana  IDD NASSORO MKAMBALLAH  akichukia fomu ya kugombea nafasi ya ujumbe.
 




Idd Nassor Mkamballah akirejesha fomu kwa Katibu msaidizi wa kamati ya uchaguzi wa club ya Simba bwana Khalid Kamguna

Saturday, May 3, 2014

WATANZANIA WATAKIWA KUKABILIANA NA RUSHWA



Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dk Mohamed Gharib Bilal amewataka watanzania kuwa wazalendo na nchi yao kwa kufichua vitendo vya rushwa vinavyoendelea kukithili nchini.
 Ameyasema hayo katika uzinduzi wa mbio za mwenge uliozinduliwa rasmi 2may katika mkoa wa kagera wilayani bukoba  katika viwanja vya kaitaba wenye kauli mbiu isemayo Tujitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba bora  na kusema kuwa rushwa ni chanzo cha kufifia kwa maendeleo kwa kuathili kila sekta na kusema kuwa watanzania wote tushirikiane katika kutokomeza rushwa na kusema kuwa jukumu la kutokomeza rushwa si jukumu la Taasisi ya kupambana na kutokomeza rushwa TAKUKURU peke yake bali sote tushirikiane katika kupambana na rushwa .Pia ameeleza sababu ya rushwa ni pamoja na mmomonyoko wa maadili,tama ya kujilimbikizia mali na kukosekana kwa uzalendo.Na kutoa Rai kwa watanzania kuacha kutoa na kupokea rushwa na wanapoona vitendo hivyo walipoti taarifa mapema kwa mamlaka husika.
Naye Waziri wa habari vijana tamaduni na michezo Fenera Mkangara amesema kuwa mwenge wa uhuru ni tunu na ishara ya uhuru wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania pia amesema kuwa mwenge wa uhuru ni unatumika kuchochea maendeleo kwa wananchi kwani wananchi huamasishwa kubuni na kuandaa miradi mbalimbali ya kijamii na uchumi.
Aidha amesema kuwa kwa mwaka huu mwenge wa uhuru utakimbizwa kwa siku 165 katika halmashauri za wilaya zote za Jamhuri ya muungano wa Tanzania na kusema kuwa mbio hizo za mwenge zinatarajiwa kifikia tamati katika mkoa wa Tabora tarehe 14 October 2014 na atakayehitimisha mbio hizo za mwenge ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete.