Friday, June 27, 2014

WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA WATAKIWA KUJADILI NA KUCHAMBUA RASIMU YA PILI YA KATIBA ILI KUPATA KATIBA ILIYO BORA KWA KILA MWANANCHI WA KITANZANIA



Wito umetolewa kwa wote wanaohusika katika mchakato wa kupata katiba mpya kungalia maslahi ya Taifa kwanza badala ya kuangalia maslahi binafsi au ya vyama vyao.
Hayo yamesemwa na afisa wa shirika la Oxfam nafasi za wanawake katika kupata Katiba Mpya Heri Ayubu wakati wa mdahalo wa mchakato wa katiba na jinsia uliofanyika Juni 26 na kuwahusisha Wanawake mbalimbali kutoka tarafa ya Kilosa.
Ayubu amesema tangu kuanza kwa mchakato wa kupata katiba Mpya kumekuwepo na changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya makundi kuvutia kwake hususani watu wa vyama vya siasa hali inayotoa mashaka ya kupatikana kwa katiba nzuri iliyopendekezwa na wananchi.
Aidha ayubu ameongeza kusema kuwa wanaendelea kutoa elimu mbalimbali kwa wadau hususani wanawake ili muda utakapofika wakati wa kupiga kura ya  katiba wawe na ufahamu mkubwa ju ya katiba hiyo  maamuzi watakayotoa yawe sahihi.
Kwa upande wa wajumbe waliohudhulia mdahalo huo mwalimu Sikuzani Mfinanga  na Rehema Mhini kwa niaba ya wanawake wenzao wamesema kuwa wanashukuru kwa kufanyika kwa mdahalo kwani umeweza kuwapanua kifikra na wamewaomba wajumbe wa bunge maalumu la katiba kuheshimu mawazo yao na kutoa wito kwa wanawake nchi kuisoma kwa makini katiba mpya itakapotoka na kujitokeza katika kuipigia kura.
Mdahalo huo umeandaliwa na shirika la msaada wa kisheria morogoro Palaregal kwa kushirikiana na mashirika ya Restress Development,

Wednesday, June 25, 2014

MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUKANYAGWA NA GARI WILAYANI KAHAMA




Mkazi wa mjini Kahama Mkoani Shinyanga Ismail Mohamed-(47) ambaye pia alikuwa mwamuzi wa Soka, amefariki dunia  kwa kugongwa kisha kukanyangwa na Lori la mchanga wakati akiendesha baiskeli katika eneo la Bijampola mjini humo.

Kwa mujibu wa tovuti ya farajimfinanga.com Mmoja wa mashuhuda Kapambara Juma amesema  kwamba, chanzo cha ajali hiyo ambayo imetokea jana jioni ni mwendokasi wa Roli hilo Aina ya Fuso lenye no.T 161 AQR Mali ya Ndeleye Trans lilokuwa linaendeshwa kwenye barabra ya Lami iendayo nchi za Rwanda na Burundi.
Tukio hilo limetokea mwezi mmoja tangu ajali nyingine iliyomuua msichana ambaye hakujulikana, hali iliyosababibisha Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani wilayani humo kuahidi kuyaondoa mara moja magari makubwa yanayoegeshwa na kubana njia barabarani hapo.

Wananchi waliokuwa kwenye eneo hilo wamehoji ahadi ya Jeshi la Polisi kuyaondoa magari hayo huku yakizidi kuongezeka kila siku na wala hakuna hatua zozote za utekelezaji zilizoweza kuchukuliwa.

Ofisa wa kikosi cha usalama barabarani aliyefika kwenye tukio hilo Thoma Muyonga alipotakiwa kuzungumzia malalamiko hayo amesema, Polisi kwa kushirikiana na serikali walikuwa wakikamilisha hatua za kuhamisha maegesho hayo kuyapeleka nyakato hatua ambayo imekwisha kamilika.

Jeshi la Polisi wilayani humo linamtafuta dereva wa lori hilo ambaye alikimbia baada ya kupata ajali ambapo mazishi ya mwili wa Marehemu Mohamed yamefanyika jioni katika makaburi ya waislamu yaliyopo mtaa wa majengo mjini kahama. 




KESI YA MSICHANA ALIYEBAKWA NA WANAUME 6 NCHINI KENYA YAZUA MAANDAMANO





Kesi dhidi ya mshukiwa mmoja anyetuhumiwa kumbaka msichana mmoja katika eneo la Bumala Magharibi mwa Kenya imeahirishwa. 

Mshukiwa mmoja kati ya sita wanaodaiwa kumbaka na kumtupa katika shimo msichana huyo kwa jina Liz, alifikishwa kizimbani na kufunguliwa mashtaka ya kumbaka na kujaribu kumuua msichana huyo, katika kisa ambacho kimezua hasira na hamasa miongoni mwa wakenya wa tabaka zote

Kinyume na kesi zingine, kesi hii iliendeshwa faraghani huku mawakili wanaowakilisha pande husika na maafisa wa mahakama ndio walioruhusiwa kuwepo mahakamani.

Afisa kutoka ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu aliwaambia waandishi wa habari kuwa ni mkubwa pekee ambaye anapaswa kuzungumzia suala hili, kutokana na uzito wake.

Mawakili wa mshichana huyo wamesema kuwa wao waliamua kuomba kesi hiyo kuendeshwa faraghani ili kumlinda mhusika ambaye yuko chini ya umri wa miaka 18. Pia uamuzi huo ulichukuliwa ili kuwapa wanaohusika Imani ya kutoogopa mtu yeyote.

Mwandishi wa BBC ambaye yuko mjini Busia Robert Kiptoo, anasema kuwa kinyume na ilivyokuwa Jumatatu wakati mamia ya watu waliandamana, leo hali ilikuwa shwari huku jamaa na marafiki tu ndio waliofika mahakamani.

Liz alitoa ushahidi wake leo asubuhi na kisha kuhojiwa nyakati za alasiri kuhusiana na tukio hilo ambalo lilimuacha kama amelemazwa kabisa.

Washukiwa wengine watano bado wanasakwa na polisi na duru zinasema kuwa wazazi wao wamepewa ilaani kuwawasilisha washukiwa hao mahakamani.

Liz inadaiwa alibakwa na wavulana sita Juni mwaka jana na kututwa katika shimo la choo, hali iliyosababishia majeraha ambayo kwa sasa yamemlemaza.

Tangu wakati huo wanaharakati wa kijamii wamekuwa wakishinikiza mkuu wa polisi nchini Kenya kuhakikisha kuwa waliombaka Liz wamefikishwa mahakamani.

Hata hivyho sakata hiyo ilichukua mkondo tofauti pale, ilipofichuliwa kuwa waliombaka waliachiliwa huru na polisi baada ya kuadhibiwa kufyeka nyasi katika kituo kimoja cha polisi.

Kesi dhidi ya mshukiwa mmoja wa ubakaji wa msichana Liz na kumjeruhi vibaya nchini Kenya imeahirishwa hadi tarehe 8 mwezi Juni. 

Kesi ya Liz ilisababisha ghadhabu sana sio Kenya tu bali duniani kote hasa kwa ambavyo polisi waliishughulikia.
Muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali yanayopinga dhuluma dhidi ya wanawake, uliongoza waandamanaji ambao baadaye walikusanyika katika kituo cha mkuu wa jimbo, Isaiah Nakoru.
Liz alibakwa mwaka jana na kuachwa na majeraha mabaya mwilini mwake
Walimkabidhi mkuu huyo nyaraka zilizotiwa saini kutaka Liz atendewe haki.

Waliotia saini nyaraka hizo wanamtaka mkuu wa polisi kuwakamata washukiwa na kitendo hicho cha unyama dhidi ya Liz ambao walimbaka na kisha kutupa mwili wake ndani ya shimo lenye urefu wa futi 25 mjini humo.

Viongozi wa maandamano wanasema kuwa idadi kubwa ya wasichana waliobakwa tangu kusikika kwa kisa cha Liz wamekuwa wakienda kuwashitaki watuhumiwa kwa polisi.
Liz alibakwa na wanaume sita ambao walimuwacha na majeraha mabaya kwenye mwili wake kiasi cha kulazwa hospitalini kwa miezi kadhaa.

Mamake Liz alikuwa miongoni mwa waandamanaji.

SERIKALI YATAKIWA KUPANGA BEI MAALUMU YA MAZAO ILI KUWAINUA WAKULIMA KIUCHUMI



Wito umetolewa kwa Serikali kupanga bei maalumu kwa wakulima itakayo weza kuleta tija pindi watakapo vuna mazao yao hali itakayo pelekea kuepukana na bei za wafanya biashara ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Wito umetolewa juni 24 mwaka huu na wananchi wa wilayani kilosa wakiongea katika kitao walichokaa na waandishi wa habari kujadili mada iliyokuwa ikisema ni kipaumbele gani kimetolewa kwa wakulima juu ya mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN).
Mmoja wa wananchi hao Skutoka Mgeta ambaye hatukuweza kupata jina lake amesema  kuwa bei wanayouzia mazao yao inapangwa na wafanya biashara   kwani bei zao haziendani  na ghalama za uzalishaji hivo kushindwa kuendesha maisha yao na kubaki kuwa watu wa maisha duni.
Ameongeza kwa kusema kuwa Serikali inatakiwa kuweka mikakati ya bei ya wakulima kama ilivyo kwa wafanya biashara  ili waweze kuepukana na umasikini kupitia kilimo.
Naye mchangiaji aliyejitambulisha kwa jina la Mr Kipala amesema kuwa Serikali iandae soko la kuuza mazao ya wakulima kwa urahisi.na kwamba wasipoweka utaratibu mkulima atazidi kukandamizwa kwani mfanyabiashara atanunua  bidhaa kwa bei anayo itaka kutokana na uwitaji wa mteja.

WANANCHI WA KILOSA WAPATA ELIMU KUHUSIANA NA KATIBA



Kituo cha usaidizi wa Kisheria  Paralegal (KIPA) kilichopo Kilosa Mkoani Morogoro kimepokea vitabu vya aina 3 vya usaidizi wa kisheria kutoka Kituo cha Sheria na haki za Binadamu kwa kushirikiana na Twaweza lengo ni kuwaongezea uwezo wa kujitambua wananchi kuhusiana na Katiba mpya na  haki zao.
Akizungumza na HABARIKWANZA ofisini kwake Msaidizi wa Kisheria wa Wilaya ya Kilosa Vimwaya Manyoli amesema kuwa wamepokea jumla ya vitabu elfu ishirini na nne juni 22 mwaka huu ambavyo ni kitabu Katiba ni nini,Twende wapi na Hashuki mtu hapa.
 Amesema kuwa vitabu hivyo ni vizuri kwani vinaelimisha Jamii na wananchi kwa Ujumla pia mtu anaweza kuelewa kwa kuangalia picha zilizomo kitabuni humo na amewashauri wananchi  kuwa na mazoea ya kujisomea vitabu ili waweze kukuza uelewa wao wa Kimawazo.
Aidha ameongeza kuwa wananchi endapo watajenga mazoea na kusema kuwa yaliyomo ndani ya vitabu hivyo yanasadifu maisha yaliyopo sasa.