Wednesday, August 27, 2014

VIONGOZI WATAKIWA KUACHA KUJALI MASLAHI YAO BINAFSI

Viongozi wametakiwa kuacha kufanya kazi kwa maslahi yao binafsi badala yake wametakiwa kuwajibika kwa ajili ya maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
                                                Wanafunzi wa shule ya sekondari ukwiva
Hayo yamesemwa na Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvurungu august 26 mwaka huu na amewataka viongozi kusimamia miradi ya maendeleo katika maeneo yao ambapo amewataka viongozi wa Kata ulaya kusimamia miradi hiyo ya maedeleo iliyokuwa viporo vya muda mrefu katika maeneo yao hasa ujenzi wa nyumba za walimu ambao ni mradi wa muda mrefu lakini bado hauja kamilika.
              Baadhi ya majengo ya nyumba za walimu ambayo bado hayajamaliziwa katika ujezi wake

Aidha mkuu wa shule ya ukwiva Liberath Ngure ambapo ndipo kwenye ujenzi wa nyumba za walimu ambazo hazimaliziki kwa ujenzi wake amesema kuwa shule hiyo ya ukwiva inakabiliwa na changamoto nyingi lakini lakini changamoto hizo hazifanyiwi kazi na viongozi na kusema kuwa Mtendaji wa kata alishaahidi ahadi nyingi na hakutekeleza ahadi hizo na kusema kuwa alishamuandikia barua  tar 28/05/2014 kutoka katika kamati ya ujenzi inayohusiana na ujenzi wa nyumba tatu [3] za walimu ambapo ambayo barua hiyo ilikuwa ikimkumbusha kuhusu ujenzi wa nyumba hizo lakini kukawa hakuna taarifa yoyote ya utekelezaji.
                                                 Mkuu wa shule ya ukwiva Liberath Ngure
Naye mwenyekiti wa kamati ya ujenzi shuleni hapo Timotheo Mahembula amesema kuwa Halmashauri ilishatoa fedha kwa ajili ya umaliziaji wa nyumba hizo lakini fedha hizo zilitumika kwa shughuli nyingine jambo ambalo linaleta sitofahamu katika urudishaji wa fedha hizo za umaliziaji wa majengo hayo na kuongeza kuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kilosa Amer Mubarack na alimwagiza mtendaji kutafuta njia ya upatikanaji wa fedha ya umaliziaji wa nyumba hizo lakini halmashauri ilishamaliza swala hilo la ujenzi wa nyumba.
                     Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa shule ya sekondari ukwiva Timotheo Mahembula

Monday, August 25, 2014

RAIS KIKWETE AWATAKA WAFUGAJI KUWA WASTAARABU KATIKA MIFUGO YAO.

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete amewataka viongozi wilayani kilosa kutowapokea wafugaji bila mpangilio kwani ndio sababu kubwa ya migogoro ya mara kwa mara wilayani humo.
Rais wa jamhuri ya muungano Tanzania Jakaya Kikwete akiwa anaongea na wananchi wa wilayani kilosa mkoani morogoro.

Ameyasema hayo August 24,mwaka huu katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo wilayani kilosa mkoani morogoro ambapo amekagua mradi wa kufua umeme wa maji kisanga pia ameweka jiwe la msingi katika barabara ya kiwango cha lami kutoka Dumila hadi Rudewa.
Aidha Kikwete amesema kuwa viongozi wasiwe wakarimu kupita kiasi cha kuwakalibisha wafugaji wengi katika eneo moja na kusema kuwa mifugo inaongezeka lakini ardhi haiongezeki pia amezungumzia swala la wahanga wa mafuriko wa 2010 kuhusu kupatiwa viwanja kwa ajili ya makazi mapya ambapo amemhoji mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya kilosa kuhusu swala hilo na mkurugenzi kuahidi kuanza kulishughulikia zoezi hilo la ugawaji wa viwanja mwanzoni mwa wiki hii.
Wananchi waliokusanyika kwa ajili ya kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr,Jakaya Kikwete

Sambamba na hayo Rais kikwete amekumbana na changamoto nyingi za wananchi wa wilayani kilosa ambapo wananchi wa wilayani kilosa wanauhitaji wa maji safi na salama,barabara ya lami pamoja na umeme mambo ambayo ameyasema kuwa yapo kwenye mchakato.
Wakwanza kutoka kulia ni MKuu wa mkoa wa Morogoro John Bendera na wa kwanza kutoka kushoto ni mbunge wa jimbo la mikumi Sas ges.

Katika ziara hiyo ya Rais kikwete pia ameambatana na waziri wa ujenzi John Pombe Magufuli ambaye naye ameongea na wananchi wa kilosa kuhusu ujenzi wa barabara ya lami itokayo Dumila hadi mikumi na kusema kuwa ujenzi huo wameugawa kwa awamu tatu awamu ya kwanza ni kutoka Dumila hadi Rudewa ambapo ujenzi huo tayari umeshakamilika na awamu ya pili ni kutoka Rudewa hadi kilosa na mwisho kutoka kilosa hadi mikumi.
            Mheshimiwa Jakaya kikwete akihojiana na mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya kilosa

Aidha mbunge wa jimbo la kilosa Mustafa Mkulo amemuuomba Rais kikwete kukamilisha ujenzi huo wa barabara ya lami kwabla hajaondoka madarakani kwa ajili ya kuwapatia maendeleo wakazi wa wilayani kilosa.
                                            Wananchi wakitawanyika mara baada ya mkutano

Pia Rais kikwete amezawadiwa zawadi mbalimbali kutoka wilayani kilosa ikiwa ni pamoja na ng’ombe wawili majike na wote wanamimba na dume moja la ng’ombe,kinyago cha tembo kutoka TANAPA picha ambayo wamemchora Rais kikwete pamoja na mchele tani moja ambao unalimwa wilayani kilosa mkoani morogoro.

MAHAFARI YA 39 YA SHULE YA MSINGI MAZINYUNGU YAFANA YASABABISHA KUTATUA KERO ZA SHULENI HAPO.

Shule ya msingi mazinyungu inakabiliwa na changamoto ya kukosa uzio wa shule hali inayopelekea wasiwasi mkubwa wa amani kutokana na shule hiyo kuwa na kitengo maalum cha watoto walemavu wasioona na walemavu wa ngozi [Albinism].
                                         Meneja wa NMB tawi la kilosa Lameck Matemba
Hayo yamebainishwa august 22 mwaka huu kwenye mahafari ya 39 ya wahitimu wa darasa la saba katika shule ya msingi mazinyungu ambapo kwa mwaka 2014 huu wanahitimu wanafunzi 88 wasichana wakiwa 45 na wavulana 43 na wanaotarajiwa kuhitimu darasa la saba kati ya hao walemavu ni sita wakiwemo wasichana watano na mvulana mmoja,ambapo katika risala hiyo iliyoandaliwa na shuleni hiyo imeeleza kuwa hali wa wanadamu kwa sasa imebadilika kutokana na baadhi ya watu wasio wema kuwasaka walemavu hao wa ngozi kwa imani za kishirikina kwa kueleza kuwa shuleni hapo waendesha pikipiki hupita mara kwa mara na wakiwa mwendo wa kasi hali ambayo ni hatari kwa wale walemavu wa macho.
                Meneja wa Benk ya NMB Lameck Matemba wa pili kutoka kulia akifuatiwa na mwalimu mkuu wa shule ya mazinyungun Lameck Mkude ambaye niwatatu kutoka kushoto


Sambamba na hayo shule hiyo ya mazinyungu inakabiliwa na changamoto ya ukosefu madawati hali inayopelekea wanafunzi kukaa wengi katika dawati moja na kueleza kuwa pamoja na upungufu wa madawati shuleni hapo wanauhitaji mkubwa wa SIMTANK kwa ajili ya kuhifadhia maji shuleni hapo.Pia serikali imeombwa kuwajali walimu ili kuepusha migogoro ya mara kwa mara kwani inadidimiza kiwango cha ufaulu mashuleni.
                      Wanafunzi wahitimu wa darasa la saba katika shule ya msingi mazinyungu iliyopo wilayani kilosa mkoani Morogoro
Katika mahafari hayo yaliyohudhuliwa na Meneja wa Bank ya NMB tawi la kilosa ambaye ndiye aliyekuwa mgeni Rasmi Lameck Matemba amesema kuwa kuhusu changamoto zilizotajwa shuleni hapo wao kama Benk ya NMB wapo tayali kuisaidia shule hiyo na kwani tayari wameshaandika andiko kwenda makao makuu kuhusu changamoto mbalimbali za shuleni hapo pamoja na hapo meneja huyo ametoa kiasi cha shilingi laki moja na nusu kwa ajili ya chakula kwa wale wahitimu wa darasa la saba siku ya mtihani.
                    Watoto wenye ulemavu ambao ni kitengo maalum katika shule ya msingi mazinyungu
Ameongeza kwa kuiasa jamii kuwa wawe walinzi wazuri kwa watoto wao hasa kwa hawa waliopo shuleni hapo wenye ulemavu kwa kuwajali na kuwapa huduma muhimu na ameongeza kuwa wazazi wanatakiwa wajipange kwa watoto wao wanaotarajia kufanya mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi hivi karibuni na pindi matokeo yanapotoka waweze kujiunga na kidato cha kwanza.
Meneja wa NMB Tawi la kilosa Lameck Matemba akiwapa zawadi walemavu baada ya kuonyesha uhodari wa kupiga ngoma na uwimbaji katika mahafali yao.
Kwa wake Katibu wa chama cha mapinduzi [CCM] wilayani kilosa Dodo Duguli Sambu akizungumza kwa niaba ya wazazi amewapongeza walimu kwa kuwapatia elimu na malezi watoto wao kwa kipindi chote walichokuwa shuleni pia amewaomba wazazi wenzake kuwa na ushirikiano na walimu katika kukuza kiwango cha ufaulu..........cue ya katibu wa ccm kilosa dodo duguli sambu.
Katibu wa CCM wilayani kilosa Dodo duguli sambu akiongea kwa niaba ya wazazi katika mahafari ya 39 ya shule ya msingi mazinyungu.

Saturday, August 23, 2014

VIONGOZI WAWA KIKWAZO KIKUBWA CHA MIMBA MASHULENI



Imesemekana kuwa tatizo la wasichana kupata mimba wakiwa mashuleni linasababishwa na viongozi  kutowafuatilia waliowakatisha masomo wasichana hao wakiwa bado wapo shuleni. 
              Bodi ya shulewa kwanza kushoto ni mratibu elimu kata akifuatiwa na mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ukwiva Liberath patrick Ngure na kufuatiwa na mwenyekiti wa bodi ya shle Mussa Hamisi na wa pili kutoka kulia na ni Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvulungu

Akizungumza katika bodi ya shule august 22 mwaka huu Mkuu wa shule ya Ukwiva Liberath Patrick Ngure amesema kuwa tatizo la wasichana kupata mimba shuleni hapo limekuwa sugu kutokana na kila mwaka kuongezeka kwa wasichana wanaopata mimba ambapo hadi kufikia February mwaka huu tayari wasichana wane walionekana kuwa na ujauzito na kufikia mwezi may msichana mmoja aligundulika kuwa ni mjamzito na kusema kuwa swala hilo kwa upande wake amewasilisha majina kwa Afisa mtendaji kata kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi lakini hakuna jitihada zozote zilizoonyeshwa kutoka kwa kiongozi huyo jambo ambalo ameeleza kuwa linamkatisha tamaa.
                                           Mwalimu mkuu wa shule ya ukwiva Liberath Patrick Ngure
Aidha ameongeza kuwa aliandika barua yenye kumbukumbu namba USS.CS.HM.VOL11/69 iliyokuwa ikihitaji taarifa juu ya mimba za wanafunzi wane [4]zilizoripotiwa katika  ofisi ya kata na mtendaji wa kata aliahidi kuleta namba za kesi zilizofunguliwa mahakamani jambo ambalo hajalitekeleza.
Kwa upande wake Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael mvulungu amesema kuwa bodi ya shule inatakiwa kusimamia maswala ya kishule kwa makini ili kumpa nafasi mkuu wa shule kuweza kuendesha shule kwa makini kwa kubaki na swala la kukuza elimu shuleni hapo na si vinginevyo.

 
                                            Mjumbe katika bodi ya shule Crensensia Mfanyakazi
Wakichangia mada hiyo ya kuongezeka kwa mimba mashuleni baadhi ya wajumbe Mratibu elimu kata Robert Mshani,Crensensia Mfanyakazi wamesema kuwa viongozi ngazi ya kata wamekuwa wapuuziaji juu ya ufuatiliaji na utatuzi wa matatizo ya shuleni hapo jambo ambalo linakwamisha maendeleo shuleni hapo.
                                       Mjumbe wa bodi hiyo ya shule Rubanga Mapesi

Mwisho mwenyekiti wa bodi hiyo ya shule Mussa Hamisi kwa kushauriana na wajumbe wameamua kuunda kamati itakayowafuata viongozi wanaoonyesha kukwamisha swala la ufuatiliaji wa kufungua kesi mahakamani dhidi ya wale wasichana waliopata mimba.
 Mwenyekiti wa bodi ya shule Mussa Hamisi

RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA DARAJA LA MTO KILOMBERO

Wananchi wa wilayani kilombero mkoani morogoro watanufaika na barabara itokayo Ruaha wilayani kilosa hadi Ifakara wilayani kilombero.

Kauli hiyo imetolewa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipokuwa akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa daraja la mto kilombero.
Pia rais kikwete amezungumzia shabaha ya serkali kuwa na viwanda kumi vya sukari na kusema kuwa mchakato unafanyika ili kupata hekta laki mbili na nusu kwa ajili ya uwekezaji huo.
Wakati huohuo Rais Kikwete amefungua mradi wa umeme katika mji wa mwaya unaofadhiliwa na REA ambapo tayari zaidi ya vijiji ishirini na saba 27 vinanufaika na mradi huo sambamba na kujionea mfumo mpya wa matibabu ujulikanao kwa jina la TELMEDICINE katika kituo cha afya cha mwaya mfumo huo unasaidia kutoa matibabu kwa wataalam ambao watakuwa katika kituo kingine kwa kumpatia mtaalam anayetoa matibabu maelekezo ya nini afanye kwa mgonjwa hasa upasuaji.
Aidha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,  Alhamisi, ya Agosti 21, 2014, ameweka historia nyingine katika ziara yake ya Mkoa wa Morogoro wakati aliposafiri kwa treni ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), ikiwa ni mara yake ya kwanza kutumia usafiri huo katika kipindi chake cha Urais.
Rais Kikwete, akifuatana na Mama Salma Kikwete, amesafiri kilomita 143 ndani ya Behewa la Kirais (Presidential Coach) la T-One kwa kiasi cha saa tatu na dakika 25 akitokea stesheni ya Ifakara katika Wilaya ya Kilombero kwenda Stesheni ya Kisaki, Wilaya ya Morogoro vijijini.
Baada ya hapo Rais kikwete anatarajiwa kuwasili wilayani kilosa august 24 mwaka huu siku ya ijumapili na atazindua miradi mbalimbali ukiwemo mradi wa umeme katika kata ya kisanga na kuzindua barabara ya lami kutoka Dumila wilayani kilosa hadi Rudewa wilayani kilosa na kufuatiwa na kuongea na wananchi wa wilayani kilosa.

Tuesday, August 19, 2014

WAKULIMA WILAYANI KILOSA WAILAUMU SERIKALI KWA KUWAPOKEA WAFUGAJI AMBAO WANAHARIBU MAZAO YAO

Wakulima wa wilayani kilosa mkoani morogoro wailalamikia serikali kwa kutowajali kutokana na mifugo kuingia kiholela wilayani humo na kuharibu mazao yao mashambani mwao.  
                     wananchi wakiwa kwenye majadiliano kwenye mkutano juu ya usuluhishi wa kuvamiwa na mifugo kijijini hapo
Wakizungumza katika mkutano wa kijiji august 19 mwaka huu baadhi ya wakulima wa kijiji cha ulaya mbuyuni Timotheo Mahembula,Saidi Hamisi na Zena kondo Wamesema kuwa wanapata manyanyaso kutoka kwa wafugaji hao kutokana na kulishiwa mazao yao mashambani na viongozi kutotoa msaada wowote kwao,na wameongeza kwa kusema kuwa tarehe 12 august ya mwaka huu walikaa kikao na kuahidiwa na Afisa Tarafa Raphael Mvurungu kuwa baada ya siku saba [7] watapatiwa majibu sahihi juu ya mgogoro uliopo kati ya wakulima na wafugaji katika kijiji hicho lakini haikuwa hivyo kutokana na siku hiyo ya saba viongozi hao kutoonekana katika mkutano huo  wa wakulima.
                            Mifugo ikiwa shambani ikishambulia mazao aina ya mbaazi
Wameongeza kwa kusema kuwa kwa sasa hawana Imani na viongozi wa kijiji chao kutokana na viongozi hao kushindwa kuwaondoa wafugaji katika kijiji chao na kutowasikiliza wakulima kuhusu kilio chao cha mifugo kuingia mashambani na kula mazao yao. 

Aidha kwa upande wake Afisa tarafa wa Tarafa ya Ulaya Raphael Mvulungu amesema kuwa yeye hakufika katika kikao hicho kutokana na tatizo hilo kuendelea kulitafutia ufumbuzi Zaidi na uliosahihi na ameongeza kuwa wananchi waondoe hofu kwani mgogoro huo utakwisha na wakulima wataendelea na shughuli zao kama kawaida kikubwa amewataka kuwa na mvumilivu katika kupa suluhu juuu ya tatizo hilo.

Tuesday, August 12, 2014

WANANCHI WA KIJIJI CHA ULYA MBUYUNI WILAYANI KILOSA WANUFAIKA NA MRADI MKAA ENDELEVU NA UVUNAJI WA HEWA SAFI KWA KUJENGEWA OFISI YA KIJIJI NA SHIRIKA LA MKUHUMI



Wananchi wa kijiji cha Ulaya mbuyuni wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamelishukuru shirika TFLG na Mjumita kwa kuwajengea ofisi ya kijiji kijijini hapo.
                         Maandalizi ya ujenzi wa ofisi ya kijiji katika kijiji cha mbuyuni wilayani kilosa mkoano morogoro

Afisa Tarafa wa Tarafa hiyo ya Ulaya Raphael Mvulungu amesema kuwa wanalishikuru shirika hilo kwani wamenufaika nalo kwa kiasi kikubwa kutokana na mpango ulioanzishwa kijijini hapo wa matumizi bora ya ardhi ambapo unahusishwa na uvunaji wa hewa ukaa na kuongeza kuwa hadi sasa kijiji kimejipatia fedha nyingi kupitia mradi huo. 
                                             Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvulungu

Naye mwenyekiti wa kijiji hicho cha Ulaya Mbuyuni Khamisi Mjomba amesema kuwa kupitia shirika hilo kijiji kina fedha zaidi ya shilingi milioni 41 kwenye benki ya CRDB na fedha hizo zitatumika katika shughuli za kimaendeleo.
                                       Mwenyekiti wa kijiji cha ulaya mbuyuni Rashid Mjomba

Na ameongeza kuwa katika ujenzi huo wa ofisi ya kijiji gharama zote zitakuwa ni za shirika na siyo zile fedha ambazo zimeshakusanywa.
                                             Ujenzi wa ofisi ya kijiji ukiwa unaendelea

Naye Mwanakamati katika ujenzi huo wa ofisi ya kijiji Comledy Robert amesema kuwa wanashukuru shirika hilo kwani katika kijiji chao hakuna ofisi ya kijiji na  ofisi inayojengwa sasa itakuwa na ukumbi wa mikutano , mahabusu na ofisi yenyewe na amesema kuwa ujenzi huo unatarajiwa kuanza hivi karibuni na kukamilika mwishoni mwa mwezi wa tisa.

MIFUGO YAWA TISHIO WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WAKULIMA WAHANGAIKA WASIJUE PAKWENDA



Mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amewataka viongozi  wa vijiji kutowapokea wafugaji  wanaotoka maeneo ya vijiji vya  jirani na kuvamia katika maeneo ya wakulima.
                                            Baadhi ya mifugo iliyopo kijiji cha ulaya mbuyuni

Ameyasema hayo agost  11 mwaka huu wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na wafugaji kuvamia maeneo ya wakulima wilayani kilosa mkoani morogoro na kusema kuwa katika wilaya yake kuna wafugaji wengi hivyo hahitaji tena wafugaji kutokana na wilaya hiyo kuwa na wafugaji wengi na kukwamisha shughuli nyingine za kimaendeleo. 
                       mazao aina ya mbaazi yakiwa yameharibiwa na mifugo katika kijiji cha ulaya mbuyuni

Ameongeza kwa kusema kuwa viongozi waliopo vijijini wanawakaribisha wafugaji hao kwa kupewa rushwa na wanapoona mambo yanawashinda  huchukua hatua ya kuwafukuza na na kushindwa kutokana na rushwa ambayo wameshaipokea.
Pia amesema kuwa pindi atakapo baini kuwa kiongozi yeyote amepokea rushwa kwa ajili  ya kumkalibisha mfugaji katika eneo lake basi atakuwa amepoteza sifa ya kuwa kiongozi. 
                                   mifugo aina ya ng'ombe ikiendelea kula mazao aina ya mbaazi

Aidha ametoa wito kwa wakazi wa kilosa kuwa na matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya wakulima na wafugaji kwa ajili ya kulinda ardhi na pia kuondoa migogoro.
Kwa upande wake katibu tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvurungu amesema kuwa katika kata yake ni kweli mifugo ipo lakini hajui wafugaji hao wameingia vipi kutokana na wenyeviti wa viji kuwatetea wafugaji hao kuwa wanawatambua uwepo wao hivyo kushindwa kuwachukulia hatua za kisheria wafugaji hao
                                    Mwenyekiti wa kijiji cha ulaya mbuyuni Rashid Mjomba

Naye mwenyekiti wa kijiji cha ulaya mbuyuni Rashidi Mjomba amesema kuwa katika kijiji chake kuna wafugaji wamevamia kijiji hicho na hajui wametoka wapi na hatua za kuwaondoa wafugaji hao zinachukuliwa na ameeleza kuwa  kuna changamoto inayowakumba kwa sasa ni kwa baadhi ya wananchi kudai kuwa endapo wafugaji hao wa jamii ya kimasai wataondoka uchumi utashuka kijijini hapo kutokana na wafugaji hao kiuwa wateja wazuri kiatika biashara zao.

Monday, August 11, 2014

KIKWETE AFANYA KWELI KWENYE MASOMO YA SAYANSI KWA SHULE ZA SEKONDARI NCHINI TANZANIA



Afisa Tarafa wa tarafa ya Ulaya Raphael Mvulungu amewataka wananchi kuendelea kuchangia ujenzi  wa  Maabara tatu katika shule za sekondari.
                                   Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvulungu

Ameyasema hayo August 10 mwaka huu wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari  utakayogharimu kiasi cha fedha cha shilingi milioni 84 ambapo kwa sasa wameanza kuchangisha fedha hizo  kwa wananchi kiasi cha shilingi 5000 kwa kila mwananchi ambapo katika Tarafa hiyo kuna nguvu  kazi 5000 ambao wanatakiwa kutoa mchango huo ambapo hilo ni  agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Jakaya Kikwete ambapo amehitaji  kila shule sekondari  iwe na maabara tatu za Sayansi , Bailojia , Kemia na Fizikia na amehitaji maabara hizo kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
                  Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Ukwiva Liberath Patrick Ngure

Kwa upande wake mkuu wa shule ya Sekondari ya Ukwiva Liberath ngure amesema kuwa mpango huo utasaidia kukuza kiwango cha ufaulu kwa upande wa masomo ya sayansi na kusema kuwa changamoto iliyopo ni baadhi ya wazazi kushindwa kujua umuhimu wa maabara na aamewaomba wananchi kwa ujumla kuwa na moyo wa kuendelea kuchangia ili kukamilisha ujenzi wa maabara hizo.                                                                                                                                                        
     wanafunzi wa shule ya sekondari ukwiva wakiwa katika jengo lililojengwa na TANAPA Shuleni hapo