Friday, October 29, 2010

UJIO WA PILI DOKTA SLAA NJOMBE



Mgombea Urais kwa tikeki ya chama cha demokrasia na maendeleo Chadema dokta WILBROD SLAA leo amefanya ziara yake mkoani njombe katika maeneo ya Saja, Ilembula na Kata ya Igwachanya kwa lengo la kuzinadi sela za chama hicho.

Dr.Slaa ambaye tayari alishafanya mikutano yake ya kampeni katika mkoa wa njombe safari hii amekuja ikiwa ni siku chache kufikia siku ya uchaguzi hapo jumapili.

Akiwa katika kata ya saja ambapo helkopta anayotumia mgombea huyo ilishindwa kutua kwa muda kutokana na hali mbaya ya hewa katika eneo hilo lakini nusu saa baadae helikopta hiyo iliweza kutua katika eneo hilo.

Akiwahutubia wananchi wa maeneo hayo ya saja na ingwachanya nakuzinadi sera za chama hicho DOKTA WILBROAD SLAA amewaomba wananchi hao kukichagua chama cha chadema ili kuweza kuleta mabadiliko nchini.

mgombea huyo wa urais pia amehaidi kuimarisha elimu ya mtanzania ili kupiga vita ujinga, umasikini na maradhi,na kwamba ili kuboresha elimu nchini si kuishia elimu ya msingi bali ni hadi vyuo, kwani elimu ya lazima kwa mtoto wa kitanzania si tu elimu ya msingi.

Mara baada ya kumaliza mkutano katika eneo hilo la igwachanya dokta Slaa ataelekea katika mkoa wa Ruvuma katika eneo la mbamba bay wilayani Mbinga na baadae katika wilaya ya Songea akiendelea na kampeni zake katika mkoa huo.




Wakati Mkoa wa Iringa ukiwa bado unashikilia nafasi ya kwanza kitaifa kwa kuwa na kasi kubwa ya maambukizi ya ukimwi, Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Manispaa ya Iringa (Iruwasa), imeanza mkakati wa kutenga Sh 4 milioni kila mwaka kwa ajili ya kupambana na ugonjwa huo kwa wafanyakazi wake.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa baraza la wafanyakazi wa Iruwasa na bodi mpya ya mamlaka hiyo, Mkurugenzi wa mamlaka hiyo, Marko Mfugale alisema wameamua kufanya hivyo kutokana na ukweli kwamba, ukimwi ni kati ya magonjwa ambayo yamekuwa yakirudisha nyuma utendaji wa kazi, kutokana na kuathiri wafanyakazi wengi.

Alisema mamlaka hiyo imekuwa ikiendesha semina na mafunzo mbalimbali kazini kwa ajili ya kutoa elimu ya ukimwi kwa wafanyakazi wake, sambamba na kuwatumia washauri nasaha kwa ajili ya kuwapima kwa hiari wafanyakazi hao.

“Ukimwi unaathiri kila kona, na umekuwa ukipoteza nguvu kazi kubwa ya taifa, tumeona ni muhimu kwetu kuanza kupambana na janga hili kwa kutoa elimu kwa wafanyakazi kwani hakuna ambaye hajawahi kuathiriwa na ugonjwa huu tishio,” alisema Mfugale.

Katika kuboresha maslahi ya wafanyakazi na kuongeza ufanisi kazini, Mfugale alisema kwa kushirikiana na Benki za CRDB na Barclays wamefanikiwa kuwakopesha wafanyakazi zaidi ya Sh 333.2 milioni sambamba na kuanzisha chama cha akiba na mikopo.

“Watumishi wetu wamekuwa wakipata mikopo kutoka maeneo mbalimbali na mamlaka inahakikisha wanapata stahili zao ili kuleta ufanisi kazini kwani kama wakiwa na kipato duni, ni vigumu sana kuendeleza jitihada za kutoa huduma bora za maji kwa jamii,” alisema.

Awali, Mwenyekiti mpya wa bodi ya Iruwasa, Cecilia Shirima aliitaka bodi hiyo kufanya kazi vizuri na kufikia malengo ya kufikisha huduma ya maji safi na majitaka kwa asilimia 100 na kupata alama ya kiwango cha ubora cha utoaji huduma kimaifa (ISO) kama ilivyo kwa mamlaka nyingine.

Bodi hiyo inaundwa na wajumbe wengine, Katibu tawala Mkoa wa Iringa Getrude Mpaka, Katibu wa CCM, Mkoa wa Iringa, Mary Tesha, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mkwawa, Profesa Mushi na Mwanasheria Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Reuben Swai.

No comments:

Post a Comment