Saturday, October 30, 2010

WAZIRI MKUU MIZENGO PETER PINDA NJOMBE.

WAZIRI MKUU MIZENGO PETER PINDA.

Waziri mkuu na Mjumbe wa kamati kuu ya siasa ya chama cha mapinduzi ccm,na mbunge wa jimbo la mpanda mheshimiwa , mizengo pinda,amefanya ziara mkoani hapa na ameupongeza uamzi wa serikali wa kuugawa mkoa wa iringa katika mikoa miwili ya njombe na iringa.

Waziri pinda ameyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi wa jimbo la njombe kaskazini katika ziara yake ya kufunga harakati za kampaini za chama cha mapinduzi kwa majimbo ya njombe.

Akiwa katika jimbo la njombe kaskazini katika ziara yake ya kwanza mkoani hapa pinda amewapongeza viongozi wa mkoa wa iringa katika juhudi za kuboresha sekta ya elimu.

Katika sekta ya elimu mheshimiwa pinda ambae pia ni waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania amewapongeza viongozi wa mkoa wa iringa kwa ujenzi wa vyuo vikuu ambapo sasa vimefikia 6.

Pia kufuatia kujengwa kwa kituo kikubwa cha afya katika mji wa makambako Waziri Pinda amehaidi kutoa gari la wagonjwa katika mji huo wa makambako.

Katika hatua nyingine waziri pinda amewataka wananchi mkoani hapa kujitokeza katika kupiga kura ili kuwachagua rais, wabunge na madiwani.

No comments:

Post a Comment