Thursday, September 28, 2017

UVCCM YAFANYA UCHAGUZI KUWAPATA VIONGOZI WAPYA WILAYANI KILOSA

Umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi UVCCM Wilaya ya Kilosa Septemba 25 mwaka huu wamefanya uchaguzi wa Viongozi wa ngazi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Vijana kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.
Uchaguzi huo umefanyika kwenye ukumbi wa MT lodge uliopo Mjini Kilosa na kuudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa chama hicho wa Wilaya na ambapo ndugu Salehe  Nasibu Mhando amefanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa umoja wa vijana Wilaya kwa kupata ushindi wa jumla ya kura 311 na kuwapita wapinzani wenzake wawili ambao ni Malko Madenge aliepata kura 65, Catherine Mtugo aliepata kura 134 ambapo idadi ya kura zote zilizopigwa ikiwa ni 524 huku zilizoharibika ni kura 14.

Akizungumza baada ya kuapishwa mwenyekiti huyo mpya Salehe Nasibu Mhando amesema anawashukuru wajumbe wote waliojitokeza kumpigia kura na kuahidi kuwa atahakikisha kutenga ofisi za Vijana katika kila eneo kuutumikia umoja wa Vijana wa chama cha mapinduzi kwa kutumia baraza la wilaya kwa kushirikiana na kamati ya utekelezaji ili kusaidia umoja huo kuwa na idadi kubwa ya vijana kwenye chama tawala.

Naye Mwenyekiti aliemaliza muda wake Michael Mkolokoti amemshauri Mwenyekiti Huyo mpya kuhakikisha anawasaidia vijana kwa kuwaondoa katika hali ya kutumika vibaya bila manufaa hasa kipindi cha uchaguzi.

Friday, August 18, 2017

WAFANYAKAZI WATAKIWA KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI ILI WAWEZE KUNUFAIKA NACHO

Chama cha Wafanyakazi Wilayani Kilosa kimewataka Wafanyakazi kutoka kwenye Taasisi na Mashirika mbalimbali kujiunga na chama hicho ili kiwasaidie pindi wanapodhurumiwa haki zao.

Hayo yamesemwa na Katibu Msaidizi kanda ya Mashariki wa Chama cha Wafanyakazi Wilaya ya Kilosa  Gerald Edgar Tayari alipokua akitatua moja ya mgogoro wa Wafanyakazi wa Kampuni ya Mbeula Security Guard Limited ambao hawakupata malipo yao.

Wakizungumzia mgogoro huo baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni hiyo Chacha Paulo, Maiko Msagati, Tausi Ally na Kaniki Kusekwa wamesea kuwa hawajapata malipo yao tangu walipoanza kufanya tarehe 12/7/2017 hadi agost 18 mwaka huu na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo kutoweka eneo la kazi pasipo na taarifa maalum kwa Wafanyakazi wake na wanapojaribu kuwasiliana nae kwa njia ya simu hapatikaniki.

Aidha kwa upande wake Meneja wa Kampuni hiyo Mpemba Erasto amesema kuwa hana taarifa kamili yakuondoka kwa bosi wake kwani aliondoka huku akidai kuwa anafuata vifaa vya ulinzi lakini tangu alivyoondoka hadi sasa hakurejea kazini.

Thursday, August 3, 2017

WAMAMA WATAKIWA KUWAPA WATOTO WAO LISHE BORA


WANANCHI WILAYANI KILOSA WAMETAKIWA KUZINGATIA UMUHIMU WA LISHE BORA NA TARATIBU SAHIHI ZA ULISHAJI WATOTO WACHANGA NA WADOGO ILI KUKABILIANA NA TATIZO LA UTAPIAMLO.

HAYO YAMEELEZWA AGOST 2 NA KAIMU MGANGA MKUU WA WILAYA THOMASI KIBULA KWA NIABA YA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI AMBAYO IMEANZA AGOST 1 NA ITAFIKA TAMATI AGOST 7 MWAKA HUU.

KIBULA AMESEMA KAULI MBIU YA MWAKA HUU KWENYE MAADHIMISHO HAYO NI ''SOTE KA PAMOJA TUENDELEZE UNYONYESHAJI WA MAZIWA YA MAMA " MAADHIMISHO HAYO YAMEBEBA UJUMBE UJUMBEAALUMU UNAOLENGA KUHAMASISHA NA KUONGEZA UELEWA WA JAMII KUHUSU IMUHIMU WA LISHE BORA KWA WATOTO NA TARATIBU SAHIHI ZA UZALISHAJI WATOTO WACHANGA NA WADOGO ILI KUKABILIANA NA TATIZO LA UTAPIAMLO.

AMEONGEZA KWA KUSEMA MAADHIMISHO HAYO YANALENGO LA KUSISITIZA UMUHIMU WA KULINDA, KUIMARISHA NA KUENDELEZA UNYONYESHAJI WA MAZIWA YA MAMA ILI WATOTO WAKUE KATIKA AFYA NJEMA.

TANZANIA HUUNGANA NA NCHI NYINGINE DUNIANI KUADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA YA MAMA.

Sunday, July 30, 2017

ZAIDI YA WAFANYAKAZI 400 MKOANI MOROGORO HATIANI KUFUTWA KAZI

Zaidi ya Wafanyakazi 400 wa Serikali wanatarajia kuondolewa kazini mkoani Morogoro kutokana na kushindwa kujiendeleza kielimu baada ya kuajiriwa miaka 13 iliyopita wakiwa na vyeti vya elimu ya msingi.
Watumishi hao ambao wengi wao ni wauguzi, wahudumu wa afya, madereva, wahudumu wa ofisi, watendaji wa mitaa, vijiji na kata tayari wamenyimwa mishahara yao ya mwezi huu.
Akizungumzia zoezi hilo aliyekuwa Mtendaji wa Kata ya Kimamba wilayani Kilosa, Mashaka Motile amesema katika wilaya hiyo watumishi zaidi ya 80 wamenyimwa mshahara bila maelezo yoyote na walipofuatilia ndipo walipofahamishwa kuwa walipewa muda wa kujiendeleza na wameshindwa kufanya hivyo.
“Hakuna barua yoyote tuliyopewa ya kusimamishwa kazi ila mshahara wa Julai hatujapewa na tulipofuatilia tuliambiwa kuna waraka wa Serikali unaosema wale wote walioajiriwa kuanzia mwezi Mei 20, 2004 wakiwa na elimu ya msingi na wameshindwa kujiendeleza wanatakiwa kuondolewa,” amesema.
Motile anasema yeye na baadhi ya watendaji wengine walisimamishwa kazi kimakosa kwani agizo linasema wasimamishwe kazi walioajiriwa kuanzia Mei 20, 2004 lakini wao waliajiriwa Mei Mosi, 2004.
Akizungumzia uamuzi huo wa Serikali, mhudumu wa afya wa manispaa ya Morogoro ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema uamuzi huo umekuwa wa ghafla mno na haujatoa muda wa wao kujiendeleza.
“Naiomba serikali ituongeze japo miaka mitatu ili tuweze kujiendeleza maana hivi tulivyosimamishwa kazi ghafla familia zetu zitaathirika sana na kuna hatari ya watoto wetu kuacha shule, tunaomba tuongezewe muda,” amesema.
Alipotakiwa kuzungumzia zoezi hilo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Kilosa, Kessy Mkambala alisema bado zoezi linaendelea litakapokamilika ndo ataweza kulizungumzia.
Naye Katibu wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) mkoani Morogoro, Lawrence Mdega amesema wamepokea malalamiko toka kwa wafanyakazi zaidi ya 150 wanaolalamika kuondolewa kwa kuwa wana elimu ya msingi.
“Nimeshawasilisha haya malalamiko makao makuu ya TALGWU ili washughulikie lakini tunachotaka watumishi hawa walipwe mshahara wa Julai ambao tayari waliufanyia kazi lakini pia walipwe mafao yao maana waliitumikia Serikali kwa uadilifu na vyeti vyao hivyo vya elimu ya msingi.

Thursday, July 27, 2017

VIONGOZI WAASWA KUSIMAMIA SERA YA ELIMU BURE ILI KUKUZA KIWANGO CHA ELIMU

Maafisa elimu kata na wenyeviti wa shule zote Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wametakiwa kuelimisha jamii juu ya tamko la Serikali la elimu bure ili wawe makini kufuatilia mienendo ya watoto pindi wawapo shuleni kwa kujenga taratibu za kuwachunguza iwapo wanafuatilia masomo yao au lah.

Wito huo umetolewa Julai 27 mwaka huu na afisa elimu Taaluma Mohamed Mwingilihela wakati wa mafunzo ya siku 3 yanayoendelea katika ukumbi wa Shule ya msingi Mazinyungu yaliyoanza Julai 25 mpaka Julai 28 kwa lengo la kutoa elimu kwa maafisa elimu kata na na viongizi mbalimbali wa shule jinsi ya kuwaelimisha wananchi wanaowazunguuka kujenga utaratibu wakuwafuatilia watoto wao pindi wawapo masomoni.

Mwingilihela amesema wanajamii wamesahau majukumu yao kwa kufuatilia masomo na mienendo ya watoto kwa kuwaacha wakizurula badala ya kukaa na kujisomea nakwenda kwenye mabanda ya video yaliyopo kila kona kwenye vijiji ambayo watumiaji wakubwa wa mabanda hayo ni wanafunzi hao.

Sambamba na hayo amewataka wazazi kuchangia michango midogo ya shule inayowahusu ikiwemo michango ya chakula cha mchana cha wanafunzi na michango mingine   ikiwemo ya miundombinu ya barabara kwani michango hiyo ipo nje na tamko ka serikali la elimu bure.

Aidha nae Mtendaji elimu kata kutoka Ulaya Wilayani Kilosa Rehema Kakwembe amesema wameyapokea kwa mtazamo chanya mafunzo hayo na watahakikisha kufikisha elimu tosha kwa jamii zote Wilayani hapa juu ya kushiriki katika michango inayowahusu hasa kufanikisha wanafunzi katika shule zote wanapata chakula cha mchana mashuleni vilevile kuwazuia watoto wao kwenda kwenye mabanda ya video na badala yake kuutumia muda huo katika kujisomea.

WAKAZI WAKILOSA WAONDOKANA NA ADHA YA USAFIRI ILIYOKUWA IKIWASUMBUA

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro imeanza kukarabati barabara zilizopo kwenye kata ya Kimamba B ili  kuwarahisishia watumiaji wa barabara hizo huduma za usafiri.
Akizungumza na Mwandishi wetu Diwani wa kata ya Kimamba B Yahaya Muhina amesema zoezi hilo limeanza kutekelezwa kwa fedha za Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kupitia makusanyo ya ndani.
Muhina amesema kwa muda mrefu barabara hizo hazikuwa nzuri kutokana na Mvua zilizonyesha na kusababisha kuharibika hivyo kukamilika kwa barabara hizo ni faraja kwa wananchi wake kwani zinawarahisishia shughuri zao.
Aidha kwa upande mwingine Diwani Muhina amewataka wananchi wa kata yake na watumiaji wengine wa barabara hizo kuzitunza ili ziweze kudumu kwa muda mrefu kwani Halmashauri hiyo ni kubwa na bajeti ya ukarabati wa barabara waliyonayo ni ndogo ukilinganisha na mahitaji ya vijiji na kata zinazohitaji kukarabatiwa barabara zao.
Hivi karibuni Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imekuwa kwenye mpango wa kukarabati baadhi ya barabara za mitaa na vijiji zilizoharibika wakati wa kipindi cha mvua sehemu mbalimbali Wilayani hapa.

Wednesday, July 26, 2017

WATOTO WA JAMII YAKIFUGAJI WILAYANI KILOSAWASHINDWA KUHUDHULIA MASOMO YAO KWA AJILI YAKUCHUNGA

Jeshi  la  Polisi  Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro , Iimepiga marufuku  Wananchi  Jamii  ya Kifugaji  kuwatuma Watoto kuchunga Mifugo badala ya Kuwapeleka  Shule  kusoma.

Agizo  hilo limetolewa Julai 24 Mwaka huu na Mrakibu  Mwandamizi   wa Jeshi la Polisi (SSP)  Wilaya  ya Kilosa  Afande Mayenga  Thobiasi  Mapalala  Wakati  akizungumza  na HABARIKWANZA  Ofisini Kwake kuhusiana na Swala hilo.
Afande  Mapalala  amesema kuwa kumekuwepo na Tabia kwa Baadhi ya Wafugaji   kuwatumikisha watoto katika Kuchunga Mifugo badala ya kuwapeleka shule jambo linalowakosesha watoto hao haki yao ya msingi ya kupata Elimu ili waweze kuelimika na kuendeleza maisha yao.

Afande Mapalala  amemuomba  Afisa Elimu Msingi Wilayani  Kilosa kufatilia suala hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, ili kuwabaini Wazazi na Walezi ambao wanaacha kuwasomesha Watoto , na badala  yake wanawatumikisha  katika kuchunga  Mifugo ili waweze kuchukuliwa hatua stahiki.

Aidha ametoa wito kwa jamii kutoa Taarifa kwa  Afisa  Elimu Msingi  ama Jeshi la Polisi iwapo kuna Mzazi ama Mlezi anayeacha kumpelekeka  Mtoto wake Shule na kumtumikisha katika kazi nyingine .

Friday, June 30, 2017

WAKULIMA WILAYANI KILOSA WATAKIWA KUJIUNGA NA VYAMA VYA USHIRIKA ILI KUJIPATIA MAENDELEO KWA NJIA YAKUSHILIKIANA

Wakulima wilayani kilosa mkoani morogoro wametakiwa kuvitumia vyama vya ushirika ili waweze kunufaika na mazazo yao pale wanapohitaji kuyauza.
Hayo yamesema katika mkutano mkuu wa kumi wa chama cha ushirika wilayani kilosa [kilosa co-operative union]KICU na muwakilishi wa mkuu wa wilaya Afisa utumishi mkuu wa wilaya ya kilosa Bw,Emmanuel .T. Nzunda akisoma hotuma iliyoandaliwa na mkuu wa wilaya hiyo ya kilosa Adam Mgoyi na ameviomba vyama vya ushirika kuwapatia wakulima pembejeo za kilimo na madawa ya mazao yauhakika na ametoa onyo kwa  wakulima kuacha kuchanganya mazao yao na mchanga hasa zao la ufuta kwani kwa kufanya hivyo kunashusha soko la biashara ya mazao na kushusha kipato katika wilaya pia amewahamasisha akina mama kujiunga na vyama vya ushirika ili kuleta chachu ya maendeleo katika sekta ya nzima ya ushirika.
Naye mwenyekiti wa mkutano huo Bw,Thadei Mnhangwi amewahamasisha wanawake,vijana na makundi yote kujiunga na chama cha ushirika ili kujipatia maendeleo kwa njia ya kushirikiana kwa sababu chama hicho kitawasaidia wakulima, kuuza mazao yao kwa bei nzuri na kuwahamasisha wakulima kujiunga na chama hicho, kwani wataweza kulima kilimo cha mkataba kilimo ambacho kitawasaidia wakulima kumudu gharama za kilimo na kuyauza mazao yao kiurahisi. Ameongeza kwa kusema kuwa kwa miaka hii, vyama vya ushirika vinaonekana kufifia na vingine kufa kwa sababu ya vyama hivyo kuingiliwa na siasa na kuwepo kwa soko hulia pia amewataka wakulima kuyatunza mazao yao vizuri mara baada ya kuyavuna ili kukuza soko la biashara ya mazao na kuyauza kupitia vyama vya ushirika ili kuwa na Takwimu kamili ya mazao yaliyouzwa.
Kwa upande wake meneja wa viwanda vya pamba vya ushirika wilayani kilosa Bw,Mohamedi Kindwiku amewaomba wakulima kujihusisha na kilimo cha pamba kwa kuwatia moyo kuwa kiwanda hicho kipo wilayani kilosa na mashine zipo.
Aidha Afisa kilimo Abel A.mchome aliyemwakilisha Afisa ushirika wilaya amewataka wanachama hao wao kuwa mstari wa mbele katika kilimo ili wawe mfano mzuri kwa wanachama wanaotakiwa kujiunga na ameahidi kutoa ushirikiano katika kuliendeleza shirika hilo.
Naye afisa ushirika mkoa wa morogoro Bi,Esther Kisiga amewaomba wajumbe kuyatekeleza yale yaliyoadhimiwa kwenye kikao na kuwaomba vijana kuwa mstari wa mbele kujiunga katika vyama vya ushirika ili kujipatia maendeleo na amewatoa wasiwasi wakulima kuwa masoko yapo hivyo amewahimiza kujitahidi katika kilimo.
Kwa upande wake mjumbe wa chama cha  wakulima wa pamba Tanzania[TACOGA] Bi,Zena Kabonga amewaomba wanakilosa kulima zao la pamba na kuiomba serikali kuhusu pembejeo za kilimo hasa madawa kwani kuna baadhi ya dawa si nzuri haziui wadudu hivyo kusababisha kuendelea kuharibu mazao yao.

Friday, June 23, 2017

WAKAZI WA WILAYANI KILOSA KATA YAMAGUBIKE WAKABIDHIWA HATI MILIKI ZA KIMILA ZA KUMILIKI ARDHI KISHERIA

Wananchi wa kijiji cha magubike kilichopo wilayani kilosa mkoani morogoro wamekabidhiwa hati milki za ardhi kutoka Bodi ya Taifa ya mpango yakuasinisha rasilimali za biashara za wanyonge nchini MKURABITA.

Akikabidhi hati hizo kwa wananchi Mkuu wa wilaya ya kilosa Adamu Mgoli katika kijiji cha magubike kilichopo kata ya magubike baada ya bodi ya Taifa ya mpango wa kuasinisha Rasilimali za biashara za watu wanyonge nchini MKURABITA kuwaendea wakulima kisha kupima mashamba yao chini ya usimamizi wa uongozi wa serikali ya vijiji kwa lengo la kuepusha migogoro baina yao sanjali na kutumia hati hizo kujinufaisha kiuchumi.

Naye mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya kilosa Juma kesi Mkambala amewapongeza wananchi wamagubike kwa kupata hati miliki hizo kwani zitawasaidia kutatua migogoro ya ardhi kwani hati hizo zinaonesha mwanzo na ukomo wa eneo unalolimiliki. 

Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya MKURABITA Kepteni mstaafu John Chiligati amesema bodi hiyo imeamua kuanzisha mchakato huo kwa sababu hati miliki za kimila kusudio ni kuhakikisha wananchi wananufaika kiuchumi na kuondokana na migogoro baina yao.

Saturday, April 22, 2017

WANAKIJIJI WA KIJIJI CHA MBWADE WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WAILALAMIKIA SERIKALI KWA KUTOKUWA NA VIONGOZI WA SERIKALI YA KIJIJI

Wakazi wa kijiji cha mbwade wilayani kilosa mkoani morogoro wailalamikia serikali kwa kutokuwa na wenyeviti wa vitongoji na kusababisha kushuka kwa maendeleo katika kijiji Chao kwa kukosa wawakilishi katika vikao vya halmashauri ya kijiji.
Mmoja kati ya wakazi hao aliyeomba jina lake Lihifadhiwe amesema kuwa chanzo cha kijiji hicho kutokuwa na wenyeviti wa vitongoji nikutokana uchaguzi wa mwaka 2014 wa ngazi ya serikali ya mitaa kudai kuwa kuvamiwa nawatu ambao si wakazi wa kijiji hicho ambao walipiga kura jambo ambalo liliwafanya wakazi wa eneo hilo kugomea uchaguzi kutokana na watu hao kuonekana kupiga kura kuchagua mgombea kwa maslahi yao binafsi.

Kwa upande wake kaimu mtendaji wa kijiji hicho Huruma Kandili amesema kijiji hicho kina jumla ya vitongoji vitano ambavyo ni madoto lunch, mkwajuni, kichangani, usagarani, na mtapenda kati ya vitongoji vyote vitano kimoja kina mwenyekiti wa kitongoji ambacho ni kitongoji cha madoto lunch kwa upande wake amesema kuwa kijiji chake hakina wenyeviti wa vitongoji nikutokana na wanakijiji kuvunja masanduku yakupigia kura wakidai kuwa Kuna watu waliovamia uchaguzi ambao si wakazi wa kijiji hicho jambo ambalo amelikanusha na ameeleza kuwa watu hao ni wakazi wa kijiji hicho ila kijiji hicho kina jamii mbili ya wakulima na wafugaji hivyo jamii ya wafugaji watu wakuhama hama wakitafuta malisho yamifugo yao hivyo Muda wa uchaguzi walirudi kwa ajili yakufanya uchaguzi katika kijiji Chao.

Alipotafutwa mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya kilosa Kesi Juma Mkambala kuelezea ukweli wa taarifa hii amesema kuwa yeye hana taarifa kuhusiana na tatizo hilo na ameahidi kulifuatilia.

Thursday, April 20, 2017

KAYA 151 ZIMEATHILIWA NA MAFURIKO KATIKA KATA YA MVUMI WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO

Kaya takribani 151 zimeathilika na mafuriko katika kata mvumi wilayani kilosa mkoani morogoro mafuriko yaliyotokea alfajili ya april 20 mwaka huu na kuathili vitongoji viwili bomba kumi na mvumi A katika kata hiyo.
Akizungumzia hali halisi ya mafuriko hayo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya kilosa Kesi Juma Mkambala amesema mafuriko hayo yameathili kaya 151 na kati ya kaya hizo kaya 15 zimebomoka kabisa na wakazi kukosa mahali pa kuishi pamoja na taasisi mbili za serikali ikiwemo shule ya msingi mvumi A pamoja na ofisi ya kijiji kuvamiwa na mafuriko hayo.Ameongeza kwa kusema kuwa tayari serikali imetenga eneo kwa waathilika wa mafuriko hayo kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwapatia chakula huku kamati ya maafa ya wilaya ikiendelea kutoa misaada mbalimbali kwa wahanga wa mafuriko hayo.

Akielezea chanzo cha mafuriko hayo mtendaji kata wa kata ya mvumi Aloyce izdoli amesema kuwa chanzo cha mafuriko hayo ni mto kisangata kujaa maji na kupasua na kuingia katika makazi ya watu na maji kukosa mahali pakutokea kutokana na eneo hilo kutokuwa na kalavati la kupitisha maji kwa kuwa eneo hilo kuna barabara ya lami itokayo dumila kuelekea kilosa hivyo maji kushindwa kupita kwenda upande wa pili wa barabara.

Baadhi ya wahanga wa mafuriko hayo Betha Magesa na Mashaka Rock wamesema kuwa athali walizozipata ni kubwa kutokana na mafuriko hayo kuingia ghafla na wao hawakuweza kuokoa vitu vyovyote katika makazi yao na baadhi yao kukosa mahali pakuishi kutokana na nyumba kubomoka na mazao kuingia maji.

Wednesday, April 19, 2017

BREAKING NEWS MAFURIKO YAWAVAMIA WAKAZI WA MVUMI WILAYANI KILOSA

Wakazi wa mvumi wilayani kilosa mkoani Morogoro waathirika na mafuriko yaliyotokea leo asubuhi na shughuli za uokoaji zinaendelea

Thursday, April 13, 2017

SIMBA YAIBUKA KIDEDEA KATIKA RUFAA YAO DHIDI YA KAGERA SUGAR

Simba wameshinda rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar na wamepewa point tatu baada ya kuibainika mchezaji wa kagera Sugar Mohammed Fakhi alicheza mechi ya Simba akiwa na kadi tatu za njano katika michezo dhidi ya Mbeya City, Majimaji, African Lyon hizo ndio mechi ambazo amepata kadi za njano
Hivyo simba inaongoza Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuwa na point 61 ikifuatiwa na waasimu wao yanga wakiwa na point 56

RUFAA YA SIMBA KUJULIKANA LEO

HATIMA ya rufaa iliyokatwa na Klabu ya Simba dhidi ya Kagera Sugar ambayo ilimchezesha beki wake Mohammed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano, inatarajiwa kujulikana leo baada ya kikao cha Kamati ya Saa 72 ya Usimamizi wa Ligi Kuu itakapokutana. 

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Tanzania Bara namba 194, iliyofanyika Aprili 2, mwaka huu kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, Simba ilikubali kichapo cha mabao 2-1. 

Taarifa kutoka kwa kiongozi mmoja wa bodi ya ligi (jina tunalihifadhi) ilieleza jana kuwa, kikao hicho kitafanyika leo kama ilivyopangwa na uamuzi juu ya rufaa hiyo utatolewa baada ya kikao hicho kumalizika. 

'Kikao kipo kama ilivyoelezwa, tayari maandalizi na nyaraka muhimu ambazo zilihitajika zimeshawasili, wajumbe wote wanaohusika wameshataarifiwa juu ya kuhudhuria kikao hicho," alisema kiongozi huyo wa bodi ya ligi. 

Kiongozi huyo alisema kuwa mbali na rufaa hiyo ya Simba, pia kikao hicho kitajadili taarifa za mechi nyingine mbili za ligi hiyo zilizofanyika juzi kwenye viwanja viwili tofauti hapa nchini. 

"Kikao kitajadili pia taarifa za mechi za juzi (Jumatatu) kati ya Mbao FC dhidi ya Simba na mchezo wa Mtibwa Sugar dhidi ya Azam FC, si unajua lazima nazo zijadiliwe kabisa kwa sababu tayari taarifa zimeshatumwa," aliongeza kiongozi huyo. 

Mechi ambazo Fakhi anadaiwa alionyeshwa kadi za njano ni ile iliyofanyika Desemba 17, 2016 katika mchezo namba 122 kati ya Mbeya City dhidi ya Kagera Sugar uliopigwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya na nyingine ilikuwa ni Januari 18, mwaka huu kwenye Uwanja wa Kaitaba, walipokipiga dhidi ya African Lyon ya Dar es Salaam. 

Machi 4, mwaka huu Fakhi alionyeshwa kadi nyingine ya tatu katika mchezo namba 190 kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba wakati Kagera ilipoikaribisha Majimaji ya Songea. 

Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Mecky Maxime, alikaririwa na vyombo vya habari kuwa mchezaji huyo alikuwa na kadi mbili za njano na si tatu kama Simba wanavyodai.