Wednesday, December 18, 2013

Anusurika kuuawa na majambazi wilayani kilosa

Mkazi wa manispaa ya wilaya ya kilosa mkoani morogoro,costa mwamba amenusurika kuuawa baada ya kushambuliwa kwa mapanga na watu wanaosadikiwa ni majambazi.


Akizungumzia tukio hilo mtendaji wa kijiji cha munisagara Donald mgulambwa amesema kuwa tukio hilo limetokea dec 17 mwaka huu majira ya saa nane usiku ambapo watu hao walifika nyumbani kwa bwana mwamba na kuvunja mrango kwa jiwe maarufu kama jiwe Fatuma.,
Amesema kuwa majambazi hao ambao wanasadikiwa kuwa ni wane baada ya kufanikiwa kuvunja mlango huo waliingia ndani na ndipo walipoanza kumcharanga kwa mapanga bwana mwamba pamoja na mkewe Chiku Salumu na kasha kufanikiwa kuchukua kiasi cha pesa shilingi laki nane.

Mgulambwa amesema kuwa baada ya majambazi kufanya uhalifu huo majeruhi hao walipiga kelele za kuomba msaada kwa majirani ndipo majambazi hao wakatokomea kusiko julikana.

Majirani wa eneo hilo walimkimbiza bwana Mwamba katika hospitari ya wilaya ya kilosa kutokana na majeruhi makubwa aliyoyapata huku mkewe akipelekwa katika katika zahanati ya kijiji hicho.

Tukio kama hili ni la pili kutokea katika kijiji cha munisagara ambapo viongozi wa kijiji viongozi wametoa taarifa katika kituo cha polisi wilani kilosa kwa uchungzi zaidi.

No comments:

Post a Comment