Friday, January 3, 2014

HALMASHAURI YA KIJIJI CHA CHANZURU KINATARAJIA KUKUSANYA MILIONI THELATHINI NA MOJA LAKI TATU NA AROBAINI ELFU



Halmashauri ya kijiji cha chanzuru wilayani kilosa mkoani morogoro inatarajia kukusanya kiasi cha shilingi milioni Thelathini na moja laki tatu na arobaini elfu kwa ajili ya maendeleo ya kijiji.
Hayo yamesemwa mapema mwanzoni mwa wiki hii na mtendaji wa kijiji hicho salumu kibugula wakati akiongea kwenye mkutano wa wananchi na viongozi wa kijiji hicho alipokuwa akisoma bajeti ya mapato na matumizi ya nusu ya mwaka wa fedha 2013/2014.
Kibagula amesema kuwa katika bajeti hiyo ya mwaka wa fedha 2013/2014 kijiji kinatakiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni ishirini na moja laki tatu na Arobaini kupitia vyanzo vyake vya ndani na shilingi milioni kumi kutoka kwa wahisani na ruzuku ya halmashauri ya wilaya kilosa.
Katika mkutano huom pia kumejadiliwa mgogoro wa mashamba kati ya mwekezaji aliyefahamika kwa jina la Bahamisi na wananchi wa kijiji hicho kuhusiana na mipaka iliyowekwa na idara ya ardhi wilayani kilosa

No comments:

Post a Comment