Wednesday, October 1, 2014

KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU CHA SIMAMA IMARA KWA KUPATIKANA KWA HAKI KWA KILA MWANANCHI



Kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC mwishoni mwa wiki iliyopita kimetimiza umri miaka 19 toka kuanzishwa kwake.
 Baadhi ya wasaidizi wa kisheria waliohudhulia katika sherehe za kutimiza miaka 19 ya kituuo cha kutetea haki za Binadamu LHRC Jijini Dar es salaam.
Katika sherehe hiyo ya kusheherehekea miaka 19 toka kuanzishwa kwake yaliyohudhuliwa na mgeni Rasmi Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania Jaji Joseph Walioba pamoja na viongozi mbalimbali kwa ngazi za kisiasa na kiserikali.
Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko Jaji Joseph Warioba akiongea wakati wa maazimisho hayo ya 19 ya kituo cha wasaidizi wa kisheria.

Katika sherehe hiyo ya kutimiza miaka 19 toka lianzishwe shirika hilo la kutetea haki za binadamu Walioba ameliomba shirika hilo kusimama imara kwa kuhakikisha kila Mtanzania anapata haki yake stahiki hasa

                 Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za Binadamu Bi,Helen Kijobi Simba
 kipindi hiki cha mchakato wa kupata katiba mpya amesema kuwa wananchi wanapaswa kutambua katiba ili inapofika wakati wa kuipigia kura wajue wanaipigia kura katiba ipi.
Wakwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Waroba akifuatiwa na Mkurugenzi wa kituo cha usaidizi wa kisheria Bi,Helen Kijobi Simba akifuatiwa na Askofu

Aidha Warioba amewataka wasaidizi wa kisheria kuwapa elimu wananchi waliopo vijijini na mjini ili kuhakikisha wananchi walio wengi wanajitambuana kutambua umuhimu wao katika jamii na Taifa kiujumla.
 Baadhi ya wasaidizi wa kisheria kutoka wilayani Serengeti wakipokea zawadi baada ya utendaji mzuri wa kazi zao
Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika hilo la kutetea haki za binadamu nchini Tanzania LHRC Helen Kijobi Simba amesema kuwa katika utendaji wao wa kazi wakiwa wasaidizi wa kisheria wanakumbana na changamoto nyingi ikiwemo wanasiasa kuingilia katika utendaji wao wa kazi na kuonekana wasaidizi wa 

Mwenyekiti wa chama cha CUF Prof;Ibrahim Lipumba[kushoto] akiwa na mmoja na wajumbe katika Tamasha la miaka 19 ya kituo cha sheria na haki za binadamu.


kisheria kama wapinga maendeleo na kuwa kikwazo jambo ambalo Bi,Simba amesema ni kikwazo kikubwa kwao katika ufanyaji wa kazi.
Inayoonekana kwa mbele ni keki iliyoandaliwa katika tamasha la kituo cha sheria na haki za binadamu. 

Aidha Bi,Simba amewataka wasaidizi wa kisheria kutokata tamaa katika kutetea haki za wananchi ambao hawajui hata pakuanzia.



No comments:

Post a Comment