Thursday, July 27, 2017

WAKAZI WAKILOSA WAONDOKANA NA ADHA YA USAFIRI ILIYOKUWA IKIWASUMBUA

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro imeanza kukarabati barabara zilizopo kwenye kata ya Kimamba B ili  kuwarahisishia watumiaji wa barabara hizo huduma za usafiri.
Akizungumza na Mwandishi wetu Diwani wa kata ya Kimamba B Yahaya Muhina amesema zoezi hilo limeanza kutekelezwa kwa fedha za Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kupitia makusanyo ya ndani.
Muhina amesema kwa muda mrefu barabara hizo hazikuwa nzuri kutokana na Mvua zilizonyesha na kusababisha kuharibika hivyo kukamilika kwa barabara hizo ni faraja kwa wananchi wake kwani zinawarahisishia shughuri zao.
Aidha kwa upande mwingine Diwani Muhina amewataka wananchi wa kata yake na watumiaji wengine wa barabara hizo kuzitunza ili ziweze kudumu kwa muda mrefu kwani Halmashauri hiyo ni kubwa na bajeti ya ukarabati wa barabara waliyonayo ni ndogo ukilinganisha na mahitaji ya vijiji na kata zinazohitaji kukarabatiwa barabara zao.
Hivi karibuni Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imekuwa kwenye mpango wa kukarabati baadhi ya barabara za mitaa na vijiji zilizoharibika wakati wa kipindi cha mvua sehemu mbalimbali Wilayani hapa.

No comments:

Post a Comment