Wednesday, July 26, 2017

WATOTO WA JAMII YAKIFUGAJI WILAYANI KILOSAWASHINDWA KUHUDHULIA MASOMO YAO KWA AJILI YAKUCHUNGA

Jeshi  la  Polisi  Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro , Iimepiga marufuku  Wananchi  Jamii  ya Kifugaji  kuwatuma Watoto kuchunga Mifugo badala ya Kuwapeleka  Shule  kusoma.

Agizo  hilo limetolewa Julai 24 Mwaka huu na Mrakibu  Mwandamizi   wa Jeshi la Polisi (SSP)  Wilaya  ya Kilosa  Afande Mayenga  Thobiasi  Mapalala  Wakati  akizungumza  na HABARIKWANZA  Ofisini Kwake kuhusiana na Swala hilo.
Afande  Mapalala  amesema kuwa kumekuwepo na Tabia kwa Baadhi ya Wafugaji   kuwatumikisha watoto katika Kuchunga Mifugo badala ya kuwapeleka shule jambo linalowakosesha watoto hao haki yao ya msingi ya kupata Elimu ili waweze kuelimika na kuendeleza maisha yao.

Afande Mapalala  amemuomba  Afisa Elimu Msingi Wilayani  Kilosa kufatilia suala hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, ili kuwabaini Wazazi na Walezi ambao wanaacha kuwasomesha Watoto , na badala  yake wanawatumikisha  katika kuchunga  Mifugo ili waweze kuchukuliwa hatua stahiki.

Aidha ametoa wito kwa jamii kutoa Taarifa kwa  Afisa  Elimu Msingi  ama Jeshi la Polisi iwapo kuna Mzazi ama Mlezi anayeacha kumpelekeka  Mtoto wake Shule na kumtumikisha katika kazi nyingine .

No comments:

Post a Comment