Saturday, September 7, 2013

CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.



CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.

Chuo cha mtakatifu Joseph kilichopo mkoani Morogoro leo  kimefanya tamasha la michezo katika viwanja vya michezo vya chuo cha kilimo (Sua) kwa lengo la kuboresha michezo na afya za wananchuo kupitia michezo .

Michezo hiyo iliyoanza nyakati za asubuhi na kuhitimishwa saa kumi jioni ilihusisha pia wanachuo kutoka katika chuo cha  Morogoro school of journalism (MSJ) ambapo michezo ya mpira wa miguu,mpira wa pete,kuvuta kamba ,kukimbiza kuku,na mbio za mita mia nne kwa upande wa wanafunzi na wakufunzi wao kutoa katika vyuo vyote viwili.

Mechi ya mpira wa miguu kati ya timu ya St Joseph Morogoro na Chuo cha habari morogoro(MSJ) Iliyoisha kwa ushindi wa goli 3(MSJ)  kwa 1 St Josep (Picha na Beatrice Majaliwa) 


Tamasha hilo lilokuwa na lengo la kuwaweka wanafunzi katika hali nzuri kiafya ,kufahamiana na kuweka mahusiano na ushirikiano baina ya vyuo shiriki.

Akisoma hutuba kwa mgeni rasmi Rais wa wanachuo  kutoka katika chuo cha Mtakatifu Joseph bwana Emanuel  Kabakeza amesema miongoni mwa chanagamoto wanazokutana nazo katika michezo ni pamoja na upungufu wa vifaa vya michezo ambavyo huwafanya kushindwa kufanya michezo yao kikamilifu.

Akijibu risala hiyo wakati wa kufunga bonanza hilo  mwakilishi wa mbunge wa Morogoro mjini ,katibu wa mbunge huyo bwana Mourice Masala  amesema kwa upande wake amefurahishwa na tamasha hilo lilioandaliwa na chuo hicho na kusema kwa sasa chuo kimekuwa na umuhimu mkubwa katika manispaa ya morogoro.

Masala  amesema kuwa kwa sasa chuo cha mtakatifu Joseph kimekuwa mkombozi kwa vijana wengi  katika mkoa wa morogoro na mikoa mingine kwa ujumla ikiwa ni sehemu mojawapo ya kupata taaluma katika fani mbalimbali.

Katika kupunguza adha ya ukosefu wa vifaa vya michezo ofisi ya mbunge imetoa seti moja ya jezi ya mchezo wa mpira wa miguu na mpira mmoja wa mchezp wa pete kwa wasichana ili kuongeza ari ya michezo kwa wanachuo hao.

Thursday, September 5, 2013

CHEKA AKARIBISHWA KWA VURUGU BUNGENI,NGUMI ZACHAPWA.

 
Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.

VURUGU ZA BUNGE LA TANZANIA ZAWAKERA WANANCHI.

 
 
Baada ya kuibuka mvutano mkali bungeni jana, kati ya Naibu Spika, Job Ndugai na wabunge wa Kambi ya Upinzani, wasomi, wanaharakati, Chama cha Madaktari Tanzania (Mat), Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), vimesema kinachoendelea sasa ndani ya Bunge ni masilahi ya vyama vya siasa siyo taifa.

Tuesday, September 3, 2013

SERIKALI YAJIBU MAPIGO KWA MTANDAO WA KENYA ULIOANZA KUICHOKONOA TANZANIA


 
 Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari- (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza  na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam  kuhusu  mtandao wa kijamii wa nchini Kenya ulioituhumu  Serikali ya Tanzania.

Tuesday, April 16, 2013

NMB KANDA YA MASHARIKI YATOA MSAADA WA MADAWATI 38 YENYE THAMANI YA TSH MIL 2.5 KATIKA SHULE YA MSINGI MTYANGIMBOLE WILAYANI KILOMBERO

Zaidi ya
wanafunzi 80 wa darasa la nne na la
tano wa shule ya msingi ya
Mtyangimbole
iliyopo kijiji cha Ikule kata ya
Mngeta wilayani
Kilombero,wanasomea kwenye
banda la nyasi huku wakiwa
wamekaa chini.

HabariKwanza Blog imeshuhudia hali hiyo
wakati wa makabidhiano wa msaada
wa madawati
38 yenye thamani ya shilingi milioni
mbili na laki tano uliotolewa na
Benki ya
Nmb Kanda ya mashariki shuleni
hapo.

Akizungumzia
hali hiyo Mwalimu Mkuu wa shule
hiyo bwana Emanuely Njavike amesema
kuwa wamelazimka
kufanya hivyo kutokana na shule
hiyo kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa
kwani vyumba
vilivyopo kwa sasa ni
viwili ambavyo vinatumiwa kwa
kupokezana kwa darasa la kwanza,la
pili,la tatu
na la sita.

Mwalimu Njavike
amesema kuwa hali hiyo
imewafanya
wanafunzi kutohudhuria masomo
kikamilifu kutokana na miundombinu
ya shule hiyo
kuwa mibovu hususan kipindi hiki
cha masika ambapo maji hujaa
katika vyumba hivyo na kuwafanya
wanafunzi hao kusoma katika
mazingira magumu na hatarishi.

Naye mwenyekiti wa kitongoji cha
Mtyangimbole Bwana Sangalufu John
Kibonde amesema
kuwa wananchi wa kitongoji hicho
walijenga maboma mawili mara
mbili na
yakabomoka kutokana na mvua za
masika
zinazoendelea kunyesha baada ya
serikali
kuchelewa kumalizia maboma hayo
hali inayowakatisha tamaa wananchi
kuchangia
ujenzi wa shule hiyo.
Shule ya
Mtyangimbole yenye wanafunzi 195
kuanzia
darasa la kwanza hadi la sita
inakabiliwa na upungufu wa vyumba
vitano vya madarasa na matundu
nane ya vyoo.

Hata hivyo maafisa wa benki ya NMB na Mbunge wa viti maalumu kupitia
Chama cha demokrasia
na maendeleo chadema Mheshimiwa
Suzan Kiwanga wamesikitishwa na
hali hiyo na
kusema kuwa shule hiyo inahitaji
msaada wa hali na mali ili
kuwanusuru watoto
hao wanaosoma katika mazingira
magumu na hatarishi

Monday, April 15, 2013

AJINYONGA KUEPUKA MADENI

MTU mmoja aliyejulikana kwa jina la
Karimu Kamwenda(41) mkazi wa
Kitongoji
cha Michenga A kijiji cha Michenga wilayani Kilombero
amejinyonga usiku wa kuamkia
leo kwa kile kinachodaiwa ni kukwepa madeni.

Kwa mujibu Mwenyekiti wa Kijiji cha Michenga
Bwana Iddi Kamila ameiambia
habarikwanza
kuwa kwa maelezo ya Kaka wa
Marehemu huyo, kuwa Marehemu amejinyonga
kwa
kinachosadikiwa kuwa ni kuwa na
madeni mengi aliyokuwa akidaiwa na watu mbalimbali.

Jeshi la polisi Wilayani Kilombero
limethibitisha kuwepo kwa taarifa za
mkazi huyo kujinyonga.

Wakati huo huo kijiji hicho cha
Michenga kinataraji kusoma mapato
na matumizi
ya kijiji mwishoni mwa wiki hii kwa
muujibu wa Mwenyekiti wa kijiji hocho Bwana
Idi Kamila.

Bwana Kamila ameuambia mtandaao
huu kuwa vikao vya ndani
vitakapokamilika
hiii leo taarifa itawekwa hadharani
siku ya kusoma mapato na matumizi
hayo.

KINANA KUONGEA NA WAKAZI WA IFAKARA KESHO

Katibu Mkuu wa Chama cha
Mapinduzi Taifa Bwana
Abdurahaman Kinana kesho
anataji kufanya ziara ya siku moja
Wilayani Kilombero na kuzungumza
na
Wananchi katika eneo la stendi ya
Kwa Makali.

Katibu wa siasa na uenezi CCM
Wilaya ya Kilombero Bwana
Pellegrine Kifyoga
ameiambia Habarikwanza kuwa
lengo la ziara hiyo ni
kuhamasisha ,kuangalia
utekelezaji wa ilani ya chama hicho
na kukagua uhai wa chama na
jumuiya
zake.

Bwana Kifyoga amesema kuwa
Bwana Kinana atafungua mashina ya
wakereketwa
na miradi ya kijamii na baada ya
hapo atazungumza na wananchi
pamoja na
wanachama wa CCM katika mkutano
wa hadhara utakaofanyika saa tisa
alasiri
katika Eneo la Stendi ya Kwa makali
Ifakara Mjini.

Katika Ziara ya Katibu huyo wa CCM
atambatana na Viongozi wa CCM
TAIFA, Katibu
wa NEC Itikadi na uenezi Bwana
Nape Nnauye na Katibu wa Nec
Oganaizesheni
Taifa Bwana Mohamed Seif  Khatib.

Amewataka wanachama na wananchi
kwa ujumla kujitokeza kwa wingi
kuwasikiliza
viongozi hao na kupokea maelekezo
yatakayotolewa na viongozi hao
katika
mkutano huo ili waweze kuyafanyia
kazi zaidi

Friday, April 5, 2013

SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO

SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO .

JUMLA ya Fedha shilingi Bilioni 3 Milioni 396 na Laki 9 na Elfu 9 Mia 2 na Tano zitatumika kama Gharama ya Ujenzi wa  Skimu ya Umwagiliaji katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa Wilayani Kilombero.

Kwa muujibu wa Taarifa ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero juu ya Mradi wa Ujenzi wa  Banio na Mfereji wa Umwagiliaji imeeleza  kuwa fedha zilizopatikana mpaka sasa ni Milioni 510 Laki 2 na Elfu 61 Mia 3 na Sabini na Tano Huku fedha zinazohitajika kukamilisha Ujenzi wa Skimu zikiwa ni Bilioni 2 milioni mia 916 Laki 6 na Elfu Arobaini na Saba Mia 8 na Thelathini na Tatu.

Taarifa imefafanua kuwa kati ya fedha hizo shilingi Milioni 416 na Laki 4 Elfu Sitini na Saba na Mia 3 Sabini na moja zimetumika katika Ujenzi wa Miundombinu Mfereji Mkuu Mita 900, Mifereji ya Kati 3 Mita 925 na Maumbo mbalimbali 12.

 Sehemu ya ujenzi wa mladi wa umwagiliaji wilayani kilombero  
(picha na Henry Bernard Mwakifuna.)
Mradi huo utakaosaidia upatikanaji wa uhakika wa Chakula na ongezeko la Kipato kuondokana na Kilimo cha kutegemea Mvua utasaidia Kaya 1204.

Mradi huo wenye eneo la Ukubwa wa Hekta 675 umepitia hatua mbalimbali tangu  Mwaka 1975 ukiwa chini ya Wachina walioanzisha Kituo cha Mafunzo ya kilimo ukipitia hatua mbalimbali unataraji kukabidhiwa Mwishoni mwa Mwezi ujao.

Sunday, March 17, 2013

TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI KUIWINDA MOROCCO

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 17, 2013

TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI KUIWINDA MOROCCO

Taifa Stars imeanza kambi jana jioni (Machi 16 mwaka huu) ambapo wachezaji 14 kati ya 23 walioitwa wameripoti na kufanya mazoezi leo asubuhi chini ya Kocha Kim Poulsen.

Wachezaji walioripoti ni nahodha Juma Kaseja kutoka Simba na msaidizi wake Aggrey Morris wa Azam, Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba), Shomari Kapombe (Simba) na Salum Abubakar (Azam).

Wengine ni Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mrisho Ngasa (Simba) na Simon Msuva (Yanga).

Wachezaji Hussein Shariff, Issa Rashid na Shabani Nditi ambao timu yao ya Mtibwa Sugar jana ilicheza mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) mjini Turiani wataripoti kambini leo jioni.

Kikosi hicho kitakamilika Jumanne asubuhi baada ya wachezaji walio katika kikosi cha Azam nchini Liberia kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho kurejea nchini. Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemorasi ya Congo (DRC) wanatarajiwa kutua nchini kesho usiku.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/-

MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/-

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Ruvu Shooting na Yanga iliyochezwa jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 62,228,000 kutokana na watazamaji 10,929.

Viingilio katika mechi hiyo namba 146 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,336,764.95 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,492,406.78.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,289,880.48, tiketi sh. 4,136,390, gharama za mechi sh. 4,373,928.29, Kamati ya Ligi sh. 4,373,928.29, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,186,964.14, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 850,486.06 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 850,486.06.

WAANGOLA KUCHEZESHA MECHI YA STARS

WAANGOLA KUCHEZESHA MECHI YA STARS

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Angola kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Morocco (Lions of the Atlas).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ivory Coast ndiyo inayoongoza kundi hilo ikiwa na pointi nne na kufuatiwa na Taifa Stars yenye pointi tatu.

Mwamuzi wa mechi hiyo ni Helder Martins de Carvalho wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Inacio Manuel Candido huku Ricardo Daniel Cachicumi akiwa mwamuzi msaidizi namba mbili. Mwamuzi wa mezani (fourth official) ni Antonio Muachihuissa Caxala.

Waamuzi hao watawasili nchini saa 1.20 usiku Machi 22 mwaka huu kwa ndege ya Kenya Airways wakitokea Luanda, Angola kupitia Nairobi, Kenya.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa David Fani kutoka Botswana anatarajiwa kuwasili Machi 22 mwaka huu saa 1.45 usiku kwa ndege ya South African Airways.

Naye mtathmini wa waamuzi (referee assessor) Neermal Boodhoo kutoka Afrika Kusini atawasili nchini Machi 22 mwaka huu 1.45 usiku kwa ndege ya South African Airways.

Saturday, March 16, 2013

WATOTO WALEMAVU WA KITUO CHA BETHELEHEMU WILAYANI KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA

WATOTO WA KITUO CHA BETHELEHEMU KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA.

Wanawake wa kata ya Kibaoni Wilayani Kilombero wametoa msaada wa mbuzi wawili kwa ajili ya sikukuu ya pasaka kwa watoto walemavu wa akili wa kituo cha bethelehemu unaogharimu jumla ya shilingi 180,000.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo Mratibu wa kamati ya sherehe ya siku ya mwanamke duniani Bi Sophia Msiku amesema kuwa msaaada huo umepatikana baada ya wanawake hao kufanya harambee katika sherehe ya siku ya wanawake duniani.

Bi Msiku amesema kuwa katika kusherekea siku ya mwanamke duniani walipanga kushiriki na watoto hao lakini kutokana na mambo kuingiliana walishindwa kufanya hivyo na badala yake walipanga siku ya kupeleka msaada huo.

Akizungumza wakati akipokea msaada huo mlezi mkuu wa kituo hicho Sister Maria Dorothea Lyimo amewashukuru akina mama hao na amewataka watu wengine kuiga mfano huo kwa kutoa msaada huo kwa watoto hao .

Tuesday, March 12, 2013

WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU

WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU .

Wakulima wa vitongoji vya lipangalala,lihami,kwa mkuya na kiyongwile kata ya Ifakara Wilayani Kilombero wamelalamikia kucheleweshwa mbolea ya ruzuku  ambayo ilitakiwa kufika tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana.

Wakizungumza na Mtandao huu wa habarikwanza Baadhi ya wakulima wamesema kuwa pembejeo katika maeneo hayo zimechelewa kufika hali ambayo imewafanya wakulima hao kushindwa kuzitumia hasa zile za kupandia kutokana na muda kupita.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya kugawa vocha za pembejeo katika maeneo hayo Bwana Paulo Magehema amekiri malalamiko ya wakulima hao ambapo amesema kuwa mbolea hiyo ilitakiwa ifike mwaka jana lakini imefika mwezi machi mwaka huu  huku  mimea ikiwa imeshaota na kukua hivyo kwa upande wa mbolea ya kupandia haitafanya kazi yoyote.

Hata hivyo amesema pamoja na kucheleweshwa kwa mbolea hizo wakulima 300 watanufaika na mbolea hizo ambazo zimefika  chache ambazo hazitakidhi idadi ya wakulima waliotuma maombi ya kupatiwa mbolea hizo




WANAFUNZI WILAYANI KILOMBERO WAHIMIZWA KUONGEZA BIDII KATIKA MASOMO YAO KUEPUKA AIBU YA MATOKEO KATIKA MITIHANI YAO YA KUHITIMU

WANAFUNZI WILAYANI KILOMBERO WAHIMIZWA KUONGEZA BIDII KATIKA MASOMO YAO

Wanafunzi wilayani Kilombero wamehimizwa kuongeza bidii katika masomo ili wafanye  vizuri katika mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne na kuondokana na aibu ambayo taifa imepata  kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha nne  kwa mwaka 2012 kufeli.

Hayo yameelezwa leo na mbunge wa jimbo la Kilombero Mheshimiwa Abdul Mteketa wakati akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kata ya Kibaoni alipokuwa akitoa msaada wa vitabu 100 vya masomo ya hesabu,jiografia,kemia,fizikia na bailojia katika shule hiyo.

Mh,Mteketa amesema kuwa kufeli kwa wanafunzi wengi inatokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa vitabu ,walimu na baadhi ya wanafunzi kutokuwa na nidhamu hivyo amewataka   wazazi ,walezi na walimu kushirikiana  kikamilifu ili kuinua kiwango cha taaluma shuleni hapo .

Kuhusu baadhi ya wanafunzi kutokuwa na nidhamu kwa walimu na utoro,amesema suala la nidhamu kwa mwanafunzi ni ushirikiano kati ya wazazi na walimu na hivyo amewataka wazazi kuwa wakali kwa watoto wao pindi wanapokosea  badala ya kuwatetea , hali hiyo inasababisha wanafunzi wengi kutokuwa na nidhamu pindi wanapoona wanatetewa na wazazi wao.

Awali akizungumza wakati akipokea msaada huo kwa niaba ya shule mkuu wa shule hiyo  Bwana Zakaria Kalinga amemshukuru Mh Mteketa  kwa msaada wa vitabu 100 na amemuomba asichoke kuitembelea shule hiyo na kutatua changamoto zinazowakabili ili kuinua kiwango cha taaluma shuleni hapo.

Bwana Kalinga amesema shle hiyo inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vitabu,uchache wa samani za ofisi,uhaba wa walimu hasa wa masomo ya sayansi,ukosefu wa nyumba za walimu,ukosefu wa hostel na ukosefu wa vifaa vya michezo na fedha kwa ajili ya matengenezo ya uwanja .

Kuhusu vifaa vya michezo na matengenezo ya uwanja mbunge huyo  amewaahidi atahakikisha anatekeleza ahadi hiyo.

Monday, March 11, 2013

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA MSAADA WA VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA  VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE

MBUNGE wa Jimbo la Kilombero Mheshimikwa Abdul Mteketa ametoa msaada wa Vitabu 200 vya Masomo mbalimbali kwa Shule ya Sekondari ya Kiyongwile iliyopo Kata ya Ifakara.

Akizungumza na Wanafunzi na Walimu wa Shule  hiyo Wakati akikabidhi msaada huo Mheshimiwa Mteketa amewaeleza kuwa  Lengo  la msaada huo ni kuinua Taaluma na kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi  wa shule hiyo na pia ni moja ya kutekeleza ahadi ya kuboresha Elimu kwa shule za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Kilombero.

Amewataka Wanafunzi na Walimu kuvitunza Vitabu hivyo ili Viwasaidie wanafunzi waliopo kwa sasa na watakaokuja baadaye.
Msaada uliotolewa ni Vitabu vya Masomo ya Fizikia, Kemia, Jiografia, Baiolojia na Hisabati.

Mbali na Msaada huo Mbunge huyo ametoa Msaada wa Kalamu za Wino na Mkaa zenye Thamani ya Shilingi Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000/=)kwa shule ya Msingi ya Lipangalala huku akiwaahidi kujenga Vyoo na kuweka Maji katika Shule hiyo.

Mheshimiwa Mteketa ametoa ahadi hiyo baada ya uongozi wa shule hiyo kumweleza matatizo hayo likiwemo  na tatizo la Ukosefu wa Umeme shuleni hapo.










KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA MSAADA WA PIKIPIKI KWA JESHI LA POLIS WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75

KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA  PIKIPIKI KWA JESHI LA POLISI WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75 
 
Kituo Kidogo cha Polisi cha Mngeta kilichopo wilayani Kilombero kimepatiwa msaada wa pikipipiki moja aina ya bajaji Boxer yenye thamani ya shilingi 1,750,000 kutoka kampuni ya Kilombero Plantation Limited KPL.

Meneja Rasilimali watu wa kampuni hiyo Bwana David Lukindo amesema kuwa msaada huo umekabidhiwa hivi karibuni na mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bwana Cater Coleman.

Bwana Lukindo amesema kuwa kampuni imetoa msaada huo baada ya kutambua kituo hicho kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa usafiri na msaada huo na anaamini kwa kiasi kidogo watakuwa wamesaidia katika kuimarisha ulinzi katika tarafa ya mngeta.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa msaada wa pikipiki hiyo Mkuu wa kituo hicho Mkaguzi msaidizi wa Polisi Joseph Elias,ameishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na anawaomba wadau wengine kuiga mfano wa KPL.

Bwana Elias amesema kuwa jeshi la polisi linakabiliwa na changamoto nyingi hususan usafiri hali inayowafanya kushindwa kuwafikia wananchi katika maeneo mengi hivyo kupatikana kwa  usafiri huo utasaidia jeshi hilo kupambana na wahalifu kwa kuwafikia wananchi wengi ,ili kupunguza vitendo vya uhalifu katika tarafa ya mngeta.
 

Friday, March 8, 2013

WAKANDARASI WAASWA KUFANYA KAZI ZAO KATIKA KIWANGO KINACHOSTAHILI.

WAKANDARASI WAASWA WILAYANI KILOMBERO

WAKANDARASI wa Ujenzi Nchini wametakiwa kufanya Kazi  zao kwa kuzingatia Sheria, ubora na Kiwango cha Hali ya Juu.

Akiongea mara baada ya kukagua maandalizi ya Awali ya Ujenzi wa Daraja la Mto Kilombero Mkoani Morogoro, Naibu Waziri wa Ujenzi Injinia Greyson Lwenge amesema kuwa ubora wa hali ya juu unahitajika katika ujenzi unaofanyika na makandarasi wakabidhi Daraja likiwa katika kiwango cha juu.

Amesema kuwa jumla ya fedha Shilingi Bilioni 53 zitatumika katika kukamilisha Ujenzi wa Daraja hilo litakalokamilika Januari 2015.

Tayari shilingi Bilioni 8 zimekwishatolewa kwa ajili ya Mandalizi ya Awali ya Ujenzi wa Daraja hilo linalounganisha Wilaya ya Kilombero na Ulanga.
 Kivuko katika mto kilombero kikitumika kuvusha abiria,wakati wakazi wake wakisubiri    kumalizika kwa daraja mwaka 2015. (picha na Henry Bernard Mwakifuna.)


Awali Injinia Mkuu wa Kampuni ya China Railways Group wanaojenga Daraja hilo Liang Yan Ping amesema kuwa watajenga Daraja hilo kwa Kiwango kwa kuwa wanauzoefu wa Ujenzi wa madaraja.

Liang amesema kuwa Muda wa Miezi 24 uliowekwa utatumika kukamilisha ujenzi huo, ingawa wako Nyuma katika Miezi Mitatu waliopewa kwa ajili ya Maandalizi ya Ujenzi huo.

Wakati huo huo Naibu Waziri wa Ujenzi Injinia Greyson Lwenge amesema kuwa Barabara ya Mikumi, Ifakara, Lupiro hadi Lumecha Mkoani Ruvuma ipo kwenye mchakato wa kupata Wakandarasi watakaoiwekea Lami.

Amesema kuwa Barabara hiyo yenye Urefu wa Kilomita 512 ni muhimu kwa Mkoa wa Morogoro na Taifa kwa Ujumla inataraji kuwa katika Kiwango kizuri ifikapo Mwaka 2015.

Thursday, March 7, 2013

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO BI AZIMINA MBILINYI KUONGOZA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI HUMO.



SIKU YA MWANAMKE DUNIANI


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Bi Azimina Mbilinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani ambayo yataadhimishwa na wanawake wa  kata ya Kibaoni katika viwanja vya soko la Kibaoni.

Mratibu wa kamati ya maandalizi ya maadhimisho hayo Bi Sophia Msiku ambae ni Afisa Mtendaji wa kata hiyo amesema kuwa kata ya kibaoni imejipanga vizuri katika maadhimisho hayo .

Bi Msiku  amesema kuwa maadhimisho hayo yataanza kwa maandamano kuanzia maendeeleo na maandamano hayo yatapokelewa na Mgeni rasmi katika viwanja hivyo.

Amesema katika maadhimisho hayo kutakuwa na maonyesho ya sanaa,michezo mbalimbali,na pia wanawake watatoa ushuhuda mbalimbali.

Ameongeza kuwa Mbali na kutoa ushuhuda mbalimbali pia  elimu ya watu kujua haki zao katika kupambana na rushwa itatolewa
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema kuwa uelewa wa masuala ya jinsia katika jamii,ongeza kasi.




SERIKALI YA KIJIJI CHA MCHOMBE YAHUSIKA NA UPOTEVU WA FEDHA JUMLA YA MILIONI 2.19

WANANCHI WA KIJIJI CHA MCHOMBE WAWAONDOA VIONGOZI WAO  WA SERIKALI MADARAKANI.


Wananchi wa Kijiji cha Mchombe wamewaondoa madarakani viongozi wa serikali ya kijiji hicho  katika mkutano wa kijiji kutokana na kuhusika na upotevu wa fedha jumla ya shilingi 2,190,000.

Kaimu Afisa Tarafa wa Tarafa ya Mngeta Bwana Shabani Mgaya amesema kuwa Kuondolewa madarakani kwa serikali hiyo kumetokana na taarifa ya mkaguzi wa ndani wa hesabu za serikali kubaini  makosa mbalimbali yaliyofanywa na serikali hiyo.

Amesema serikali hiyo imefanya upotevu wa shilingi 2,190,000 ambazo zimepotea kwa uzembe wa viongozi hao ambapo shilingi 1,780,000 ilitolewa benki na ilitumika bila ya idhini ya serikali.

Aidha Bwana Mgaya amesema kuwa kwa mujibu wa taarifa ya mkaguzi imeeleza kuwa kati ya fedha hizo shilingi 300,000  zilitokana na uuzwaji wa ardhi ya kijiji ambapo ni kinyume na sheria kwani ardhi hiyo iliuzwa bila ya kufuata taratibu na pesa hiyo haikuonekana.

 Taarifa hiyo ya mkaguzi ambayo imewafanya wananchi kuuondoa uongozi madarakani imeeleza kuwa shilingi 1,100,000 fedha kutoka mfuko wa jimbo ambayo ilikuwa kwa ajili ya uchimbaji wa visima imetumika kwa matumizi mengine tofauti na yaliyokusudiwa.

 Aidha miongoni mwa mambo yaliyobainika katika taarifa ya  mkaguzi wa ndani kwa viongozi wa serikali hiyo ni udhaifu wa serikali katika kukusanya mapato,udhaifu wa kutosimamia shughuli za maendeleo na kutosoma taarifa za mapato na matumizi kwa vipindi vitatu mfululizo.




Wednesday, March 6, 2013

MAZISHI YA MWIGIZAJI ALIYEPOTEA MKOANI NJOMBE YAFANYIKA.

Mazishi ya Mkazi Mmoja wa Kibena Mjini Njombe bwana Mexon Nyekelela Chota Yamefanyika Katika Makaburi ya Kibena,Ikiwa ni Baada ya Kupatikana Kwa Mwili wa Marehemu Uliokuwa Amezama Kwa Siku ya Tano Katika Mabwawa ya Kampuni ya TANWAT Mjini Njombe.

Akizungumza Mara Baada ya Kupatikana Kwa Mwili Huo Afisa Tarafa ya Njombe Mjini Bi Lilian Nyemele Ameishukuru Kampuni ya TANWAT Kwa Namna Ilivyoshiriki Katika Kusaidia Zoezi Hilo Pamoja na Wananchi Wote Walioshiriki.





Mwili wa Marehemu Ulipatikana Leo Majira ya Saa Nane Mchana Ikiwa ni Baada ya Jitihada za Muda Mrefu za Wananchi na Viongozi Kuweza Kuutafuta Mwili Huo Bila Mafanikio Kutokana na Ukosefu wa Vifaa Vya Uokozi.

Akizungumza Mara Baada ya Kuwasili Mkoani Njombe Mtaalam wa Uzamiaji Kutoka Jijini Dar Joseph Mapunda Anasema Kuna Haja Kwa Serikali ya Mkoa wa Njombe Kuanza Kutoa Mafunzo Kwa Wananchi na Wataalam Mbalimbali Ili Kuweza Kupata Wataalam wa Uzamiaji.

Marehemu Mexon Nyekelela Chota Alizama Kwenye Mabwawa Hayo Mnamo March Mosi Mwaka Huu Majira ya Saa Kumi na Moja Jioni Wakati Akiwa na Wenzake Mara Baada ya Kumaliza Shughuli Zao za Sanaa.

Monday, March 4, 2013

PONGEZI KWA AZAM FC KUSONGA MBELE


Release No. 037
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 4, 2013

PONGEZI KWA AZAM KUSONGA MBELE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa timu ya Azam ya Tanzania Bara kwa kufanikiwa kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho iliyo chini ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Ushindi wa jumla ya mabao 8-1 ambao Azam imeupata dhidi ya Al Nasir Juba ya Sudan Kusini si fahari kwa timu hiyo tu, bali Tanzania kwa ujumla, na unaonyesha jinsi klabu hiyo ilivyojipanga kiushindani katika michuano hiyo ya Afrika.

Hata hivyo, ni vizuri Bodi ya Wakurugenzi ya klabu hiyo, benchi la ufundi na wachezaji wa timu hiyo wakautazama ushindi huo kama changamoto kwao kuhakikisha wanajipanga vizuri zaidi kwa raundi inayofuata.

Timu ya Azam inayofundishwa na Mwingereza John Stewart Hall ilishinda nyumbani mechi ya kwanza mabao 3-1, na jana kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 ugenini jijini Juba.

Kwa kufanikiwa kuing’oa Al Nasir Juba, Azam sasa watacheza raundi ya kwanza (raundi ya 16 bora) ya michuano dhidi ya Barrack Y.C.II ya Liberia ambayo katika raundi ya awali iliitoa Johansens ya Sierra Leone. Barrack ilishinda bao 1-0 nyumbani katika mechi ya kwanza na kulazimisha suluhu katika mechi ya marudiano jijini Freetown.

Azam itaanzia mechi hiyo ugenini kati ya Machi 15,16 na 17 mwaka huu wakati mechi ya marudiano itachezwa Tanzania kati ya Aprili 5,6 na 7 mwaka huu.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

TIMU YA KIKAPU YA ST JOSEPH MOROGORO YACHAKAZWA 71-16

TIMU YA KIKAPU YA ST JOSEPH MOROGORO YACHAKAZWA 71-16.


Mchezaji wa timu ya Mt.Joseph Andrew,akijaribu kuokoa mpira katika mchezo uliofanyika juzi katika uwanja wa Polster Club dhidi ya Kihonda Hits(Picha na Mussa Enock)

Timu ya kikapu ya chuo cha Mtakatifu Joseph kilichopo kihonda barabara mpya Mkoani morogoro imechakazwa vibaya kwa jumla ya point/alama  71-16 dhidi ya timu ya Kihonda Hits katika mchezo wa kirafiki uliofanyika siku ya jumamosi ya tarehe 02 mwezi 03 mwaka huu.

Mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Polister Club  uliopo Kihonda Maghorofani ulimalizika  kwa timu ya chuo cha Mtakatifu Joseph kwa kucharazwa jumla ya point/alama 71 kwa 16 dhidi ya wapinzani wao Kihonda Hits.

Mchezo huo ulioanza kwa kasi na kuwafanya timu ya Kihonda Hits kuanza kupata point/alama 6 mfululizo na katika dakika ya 8 ya mchezo mchezaji hatari wa  st joseph maarufu kwa jina la Kulwa aliweza kuwainua mashabiki wa timu ya Chuo cha Mtakatifu Joseph kwa kufunga point zililochochea kasi ya mchezo kuongezeka kwa timu hiyo.

Hata hivyo jitihada hizo hazikuleta matumaini ya kutosha kwa upande wa timu ya chuo cha  Makatifu Joseph kwani hadi timu zinaenda mapumziko matokeo yalikua ni 37-12,Matokeo ambayo yalianza kuwavunja moyo wachezaji na mashabiki wa timu hiyo.

Tuesday, February 26, 2013

PICHA YA PAMOJA YA BAADHI YA STAFF WA CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH CHA MKOANI MOROGORO.

PICHA YA PAMOJA YA BAADHI YA STAFF WA CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH CHA MKOANI MOROGORO HII LEO...

Friday, November 2, 2012

BAADA YA KIMYA KIREFU SASA JIANDAE KUPATA HABARI ZAIDI.

WASOMAJI WA MTANDAO HUU WA HABARIKWANZA,BAADA YA KIMYA KIREFU KWA KUTOKUWALETEA HABARI NA MATUKIO MBALI MBALI,SASA HABARIKWANZA INAKUJA KWA KASI ZAIDI ILI KUWEZA KUKUJUZA WEWE MTANZANIA NA MSOMAJI WETU POPOTE PALE DUNIA. HABARIKWANZA ITAKUWA YA KWANZA KUKUHABARIRISHA..KAA TAYARI KUPATA HABARI ZAIDI.

Saturday, October 1, 2011

SHULE YA SEKONDARI YAKOSA VYOO KWA MIAKA NANE.

SHULE YA SEKONDARI MLABANI WILAYANI KILOMBERO YAKOSA VYOO KWA KIPINDI CHA MIAKA NANE

Shule ya sekondari ya Mlabani iliyopo kata ya Ifakara wilayani Kilombero, inakabiliwa na uhaba wa vyoo kwa muda wa miaka minne sasa na kuwafanya wanafunzi wa shule hiyo kuwa katika hali ya hatari ya kukumbwa na magonjwa ya mlipuko.

Hayo yameelezwa katika taarifa ya shule hiyo iliyosomwa na makamu mkuu wa shule,hiyo mwalimu Idrissa Lyoko katika mahafali ya kwanza ya shule hiyo kwa mgeni rasmi, imeeleza kuwa shule hiyo ina choo chenye matundu manane tu, ikiwemo matundu sita yanayotumiwa na wanafunzi wa shule hiyo wapatao 635.

Taarifa hiyo imeeleza Kwa sasa shule hiyo inahitaji matundu 28 ya choo
na ina upungufu matundu 22 ya choo.

Risala hiyo imeeleza kati ya wanafunzi hao wavulana 350 na wasichana 285, pia walimu wako kumi, wanaume sita na wanawake wanne, shule ina mchepuo wa sayansi, biashara na sanaa.

Mgeni rasmi katika mahafali hayo ambayo ni ya kwanza katika shule hiyo meneja wa shirika la PLAN INTERNATIONAL Tawi la Ifakara, bwana HAIDARI MFINANGA amesema viongozi wa serikali za vitongoji vilivyopo katika vijiji vya Mlabani na Katindiuka na uongozi wa halmashauri wapange mikakati ya kuiendeleza shule hiyo kimajengo

Bwana Mfinanga amesema shirika lake la Plan halitasaidia tena katika ujenzi wa majengo bali kwa sasa inafadhili watoto wanaosoma, hivyo amewataka jamii na wazazi washirikiane kuleta maendeleo ya shule hiyo kwa njia ya michango.

Tuesday, September 27, 2011

RASIMU YA HESABU KATIKA HALMASHAULI YA WILAYA YA KILOMBERO


RASIMU YA HESABU WILAYA YA KILOMBERO


Jumla shilingi bilioni 15 milioni 690 laki 944,313.00 zimepitishwa na baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya kilombero katika kikao cha kupitisha rasimu ya kitabu cha hesabu za mwisho za halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha ulioisha juni 30 mwaka huu.

Fedha hizo zimepitishwa na baraza la madiwani hii leo katika kikao maalumu cha kupitisha Rasimu ya kitabu cha hesabu za mwisho za Halmashauri kwa mwaka wa fedha ulioisha 20110/2011kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya.

Rasimu hiyo imeonyesha kuwa kiasi hicho cha fedha ni majumuisho ya mali za kudumu ambazo zimefikia kiasi cha shilingi bilioni 10 milioni 499,16,346.00 na mali za muda mfupi shilingi bilioni 5 milioni 191 laki 927,967.00.

Aidha sehemu kubwa ya mali hizo zimetokana na fadha za ruzuku kutoka serikali kuu na michango ya wahisani kiasi cha shilingi bilioni 14 milioni 79 laki 763,492.00 na ziada ilyohifadhiwa ni shilingi bilioni 1 milioni 611 laki 180,821.00.

Friday, September 23, 2011

AFYA WA WANANCHI WA KILOSA HATARINI BAADA YA KUPASUKA KWA BOMBA LA MAFUTA,LIENDALO ZAMBIA.

BOMBA LA MAFUTA LAPASUKA WILAYANI KILOSA
Jumla ya ekari 1400 za mazao mbalimbali katika kata ya Malolo wilayani Kilosa Mkoani Morogoro,zimeharibiwa na mafuta machafu yanayovuja kutoka katika bomba kubwa linalosafirisha mafuta hayo kutoka Tanzania kwenda Zambia lililopita katika kata hiyo.

Afisa kilimo cha umwagiliaji wa kata hiyo, Bwana Mwelasi amesema bomba hilo la mafuta tangu lipasuke hadi sasa ni muda wa miezi miwili na limeharibu mfumo wa umwagiliaji wa mashamba jumla ya ekari 500 ya mazao ya vitunguu na mahindi.

Bwana Mwelasi ameyataja mazao yaliyoathirika kutokana na kupasuka kwa bomba hilo kuwa ni vitunguu na mahindi ambapo hata kiwango cha uzalishaji wa mazao hayo amesema kuwa kimeshuka.

Afisa kilimo huyo amesema mimea imekauka kutokana na mafuta yanayovuja kutoka katika bomba hilo na kuingia chini ya ardhi na kuathiri mazao na kusababisha kushuka kwa kiwango cha uzalishaji.

Akizungumzia uzalishaji wa mazao katika kata hiyo Amesema hapo awali kabla ya bomba hilo kupasuka ekari moja ilikuwa ikizalisha magunia 70 ya mazao, lakini sasa ekari moja inazalisha gunia 20 ya mazao kiwango ambacho amesema kimeshuka kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo amevitaja Vijiji vilivyoathirika na mafuta hayo kuwa ni Malolo "A", Malolo "B" na Mgogozi ambapo wananchi wanaoishi katika vijiji hivyo wamo hatarini kuharibu afya zao kutokana na maji wanayotumia kwa kunywa na shughuli zinigine.

Kutokana na athari hiyo kutokea Mbunge wa jimbo la Mikumi, bwana Abdulsalam Ameri tayari amekwisha peleka mtambo wake wa kuchimba visima vya maji katika kata hiyo na kila kijiji kati ya vijiji hivyo vitachimbiwa visima viwili na kufanya idadi ya visima sita katika kata hiyo ambavyo vitasaidia kuokoa maisha ya wananchi wa kata hiyo.

UKOSEFU WA WATAALAMU MBALI MBALI KATIKA SEKTA YA KILIMO CHA MIWA NI KIKWAZO KIKUBWA KWA WAKULIMA WA MIWA KILOMBERO

UKOSEFU WA WATAALAMU MBALI MBALI TATIZO KWA WAKULIMA WA MIWA KILOMBERO
Ukosefu wa Wataalamu wa Uchumi , Mizani na Sheria ni baadhi ya changamoto zinazovikabili vyama vya Wakulima wa Miwa katika Bonde la Kilombero.

Akizungumza katika mahojiano na mwandishi wetu Katibu wa Chama Cha Wakulima wa Miwa cha Msolwa Ujamaa (MUCGA) Modestus Chitemi amesema ili kuwezesha ongezeko la bei kwa Wakulima kwa Uwiano kama ilivyo kwa Nchi Jirani Wataalamu zaidi wanahitajika.

Akitolea mfano wa Nchi ya Malawi, Bwana Chitemi amesema kuwa Wakulima wa Miwa waNchi hiyo wana uwiano wa kupata asilimia Sitini (60) wakati Viwanda vya Sukari vinapata asilimia Arobaini(40).

Ameongeza kuwa kutokuwepo kwa mgao na Ruzuku ya pembejeo kutoka Serikalini katika zao la Miwa ingawa Mahitaji ya mbolea na dawa za magugu ni makubwa sana ni changamoto nyingine inayoikabili vyama vya Wakulima wa Miwa katika Bonde la
Kilombero

Mfanyakazi katika shamba la miwa akiendelea na zoezi la ukataji miwa..(picha juu)
Changamoto nyingine ni ukosefu wa Mtaji kuanzisha na kuendeleza Kilimo cha bega kwa bega na Umwagiliaji na kukosa kasi kubwa ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara na mifereji mashambani.

Mbali ya changamoto hizo katibu huyo amesema kuwa Ajira kwa Wananchi, Idadi ya Wakulima na pato la Mkulima, limeongezeka baada ya ubinafsishaji wa Viwanda na matumizi ya mfumo Mauzo ya miwa kwa uwiano wa mapato.

Shamba la miwa wilayani kilombero..

KCY YATUMIA MILIONI TISINI KWA AJILI YA MISAADA.

KCY YATUMIA MILIONI TISINI KWA AJILI YA MISAADA MBALI MBALI.

Kampuni ya Kilimo Cha Yesu (KCY) iliyopo Mpanga Wilayani Kilombero imetumia jumla ya Shilingi Milioni Tisisni (90,000,000/=) katika Mwaka 2010 kwa ajili ya Misaada mbalimbali.

Akitoa maelezo kuhusu kazi ya Kampuni ya KCY kwenye siku ya Sekta Binafsi Tanazania, Mkurugenzi wa KCY Mpanga Bruno Wicki Bruno amesema wametumia Milioni Ishirini na Laki Tano (20,500,00/=)kwa ajili ya Kusomesha watoto ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha, Milioni Kumi na Saba na Laki Tano (17,500,000/=) misaada ya Dawa kwa walemavu na kusafirisha Wagonjwa na Milioni Kumi na Saba na Laki Tano (17,500,000/=) kusaidia Kanisa.

Shilingi Milioni Thelathini (30,000,000/=) walitumia kufidia hasara katika kampuni ya KCY na Milioni Nne na Laki sita (4,600,000/=)kwa misaada mbalimbali ya wasiojiweza.

Amesema kwa Msimu wa Kilimo uliopita walilima juml;a ya Ekari Elfu NNE mia sita(4600) na wamekopesha Shilingi Milioni Themanini (80,000,000/=) kwa Marejesho ya Riba ya Shilingi Elfu Tano(5,000) kwa Ekari kwa Vikundi kumi vyenye jumla ya Ekari elfu mbili (2000).

Kampuni ya KCY inayojishughulisha na maendeleo na kufundisha neono la Mungu kwa maneno na Matendo imeanzishwa mwaka 2004 kwa lengo la kusaidia Watanzania kuendelea katika shughuli za Kilimo.

TANZANIA KUNUFAIKA NA MSAADA WA EURO MILIONI 15 KUTOKA SERIKALI YA UHOLANZI

TANZANIA KUNUFAIKA NA MSAADA WA EURO MILIONI 15

TANZANIA itafaidika na msaada wa Euro milioni 15 ambazo ni sawa na (zaidi ya Sh bilioni 30 za kitanzania ) kutoka Serikali ya Uholanzi kugharamia mradi wa Kujenga Uwezo kwa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini unaojulikana kwa jina la NICHE.

Meneja wa mradi huo, Ute Jansen ameyasema hayo alipotembelea Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro, kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao kwa Mzumbe, unatoa ufadhili kwa Shule ya Biashara na kuboresha mafunzo ya utawala wa Serikali za Mitaa.

Jansen amesema ana matumaini makubwa kuwa mradi huo utakapokamilika, utaboresha sekta
zilizoainishwa kwenye mradi huo ambazo ni kujenga uwezo katika kutoa elimu kuhusu afya, sekta binafsi na Serikali za Mitaa.

Kwa upande wake, Msimamizi wa mradi huo nchini kupitia Shirika la NUFFIC, Johanna Van Nieuwenhuizen, amesema Uholanzi imeridhishwa na jinsi Tanzania inavyoitumia misaada kutoka nchini mwake, hivyo kujihakikishia fursa zaidi za kusaidiwa katika miradi mbalimbali.

Naye Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa Mugishi Nkwabi Mgasa, aliyemwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo, ameishukuru Serikali ya Uholanzi kwa kufadhili mradi huo na kueleza kuwa ufadhili huo una maana kubwa kwa chuo hicho kwa sababu utapanua uwezo wa chuo hicho katika kutoa mafunzo ya biashara na utawala wa Serikali za Mitaa

Thursday, September 22, 2011

PAMBAZUKO FM RADIO 90.7 MHz IFAKARA YAZIDI KUONGEZA USIKIVU.

PAMBAZUKO FM RADIO 90.7 MHz YAZIDI KUONGEZA USIKIVU

Kituo cha radio mjini Ifakara Mkoani Morogoro Panbazuko Fm sterio 90.7MHz, kwa sasa wameongeza usikivu wao kwa lengo la kuwafikia wananchi walio wengi katika sehemu mbali mbali.

Wakizungumza na mtandao huu kwa nyakati tofauti,mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho bi THERESIA MAKUNGU amesema kwa sasa wameweza kuwa na usikivu mzuri na kuwafikia wananchi walio wengi mara baada ya kumaliza kufunga mitambo yao mipya.

Bi Makungu amesema lengo kubwa la kituo chao ni kuwahabarisha wananchi yale yanayokuwa yakiendelea katika maeneo yao na duniani kwa ujumla.

Mafundi wakiimarisha mitambo ya radio pambazuko fm ifakara(picha juu)

Nae mwariri mkuu wa kituo hicho bwana ELIAS MAGANGA amesema kwa sasa wamekuwa katika wigo mpana katika kuwahabarisha wananchi wa maeneo mbali mbali ambako radio hiyo imekuwa ikirusha matangazo yake.

Maganga amesisitiza kuwa lengo kubwa la kutoa habari ni kuwajulisha wananchi yale yanayokuwa akiiendelea katika sehemu mbali mbali katika maeneo yao,na kuongeza kuwa siku zote chombo cha habari hakina ugomvi na yeyote bali vimekuwa vikitoa yale mazuri na maovu yanayofanywa katika jamii.

Wakati huo huo aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kilombero na mkuu mpya wa mkoa wa Mwanza mheshimiwa Evarist Ndikilo ameipongeza radio pambazuko kwa juhudi zake katika kuwaelimisha na kuwahabarisha wananchi wa wilaya ya kilombero.

Ndikilo ameyasema hayo katika taarifa yake fupi aliyoitoa moja kwa moja kupitia kituo hicho cha radio katika kipindi cha JIONI LEO siku ya alhamisi alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya ya kilombero katika kuwaaga kwake.

Radio Pambazuko fm kwa sasa inasikika katika mikoa ya Morogoro,Lindi ,Ruvuma na Iringa hususani katika wilaya mpya ya KILOLO

Sehemu ya antena mpya za pambazuko fm radio katika picha ya anga...

SEHEMU YA MIJI YETU INAVYOONEKANA KATIKA PICHA ZA ANGA.


Hii ni baadhi ya mitaa katika miji yetu hapa nchini Tanzania,sehemu hii inawakilisha maeneo mengi ambayo maisha ya mtanzania wa kawaida huyaendesha kila siku katika kujitafutia kipato chake cha siku..

Na hii ni kutoka katika mkoa mpya wa NJOMBE mooja ya mikoa mipya inayopatikana hapa nchini kwetu.

MKUU MPYA WA MKOA WA MWANZA AWAOMBA WAZEE KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WAPYA KILOMBERO

MKUU MPYA WA MKOA WA MWANZA AWAOMBA WAZEE KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WAPYA KILOMBERO
Ombi limetolewa kwa wazee kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkuu wa wilaya atakayekuja kuongoza katika wilaya ya kilombero pamoja na viongozi wengine wanaobaki kama walivyoshirikiana vizuri na mkuu wa wilaya aliyepita.

Ombi hilo limetolewa na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kilombero ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa mwanza mhandisi Evarist Ndikilo katika mkutano wa kuwaaga na kuwashukuru wazee wa wilaya ya kilombero uliyofanyika leo katika ukumbi wa jamosi mjini Ifakara.

Mhandisi ndikilo amewaeleza wazee, kuwa kwa kipindi cha miaka mitano aliyofanya kazi katika wilaya amefanikiwa kuleta maendeleo katika sekta ya elimu,kilimo,afya,miundombinu na mazingira,

Mbali na mafanikio hayo mhandisi ndikilo hakusita kuwaeleza wazee changamoto ambazo zinaikabili wilaya ya kilombero zikiwemo umaskini,migogoro ya Ardhi na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na mifugo na kilimo cha umwagiliaji.

Kwa upande wao wazee wamezitaja changamoto zinazowakabili ikiwemo kutibiwa bure na ajali za bodaboda zinazotokea mara kwa mara ,lakini pia wamemshukuru mhandisi Ndikilo kwa ushirikiano aliouonesha kwa wazee kwa kipindi cha miaka mitano aliyokuwa akifanya kazi wilayani hapa na kumtakia kazi njema huko aendako.

SHIRIKA LA MICHE LA ITALY LATOA KOMPYUTA KWA SHULE YA MSINGI MJINI IFAKARA

SHIRIKA LA MICHE LA ITALY LATOA KOMPYUTA KWA SHULE YA MSINGI MJINI IFAKARA
Shule ya msingi ya Madukani iliyopo kata ya Ifakara wilayani Kilombero, hivi karibuni imepokea Kompyuta kumi na Printer moja kutoka shirika la MICHE la Italia.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo, bibi Ester Nuruva ameueleza mtandao huu kuwa kompyuta walizopata kutoka katika shirika hilo watazitumia kwaajili ya kuwafunza wanafunzi wa kuanzia darasa la tatu hadi darasa la saba.

Aidha mwalimu mkuu huyo amesema hapo awali shule hiyo ilikuwa inafundisha somo la TEHAMA ambapo ilikuwa inahusu kompyuta kwa nadharia, kutokana na kupata msaada huo wa kompyuta sasa somo hilo litafanywa kwa vitendo.

Bibi Nuruva amesema aliyekabidhi msaada huo kwa shule hiyo alikuwa Rais wa shirika hilo, bibi Eva Maria Bardeleben kutoka Italia.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Madukani, amelishukuru shirika hilo kwakuwa na moyo wa kujitolea kwa upande wa sekta ya elimu, hivyo ameyaomba mashirika mengine kuwa na moyo wa kutoa misaada hususani katika sekta ya elimu.

AFARIKI KWA AJALI YA PIKI PIKI WILAYANI KILOMBERO-IFAKARA

AJALI YA PIKI PIKI WILAYANI KILOMBERO-IFAKARA

Mtu mmoja amekufa na wawili wamejeruhiwa kutokana na ajali ya gari iliyomgonga mwendesha pikpiki jana (20/9/011) eneo la kwa shungu kata ya Kibaoni wilayani Kilombero.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Adolfina Chialo ameieleza radio pambazuko kuwa ajali hiyo imetokea jana majira saa tisa na nusu alasiri baada ya gari hilo lenye usajili wa Na.T 184 AAC lilikuwa likiendeshwa na David Mtazama(39) mkazi wa kitongoji cha Mkuya na kumgonga mwendesha pikipiki Emanuel Amnungi(17) mkazi wa Mlabani aliyekuwa akiendesha pikipiki yenye usajili ya Na. T590 DRM ainaya TIBETA.

Aidha Chialo amemtaja aliyekufa katika ajali hiiyo ni Abdulazaki Mgoima(4) aliyekuwa amebebwa na mama yake Anna Sabu ambaye amejeruhiwa wakati wamebebwa katika pikipiki hiyo wakitokea mjini Ifakara kuelekea nyumbani kwao Kijiji cha Mbasa

Kamanda huyo amesema gari lililogonga pikipiki lilikuwa likitokea mjini Ifakara kuelekea Kibaoni na imegonga pikipiki kwa nyuma.

Amewataja majeruhi waliiojeruhiwa katika ajali hiyo ni Anna Sabu abiria wa pikipiki na dreva wa pikipiki Emanuel Mnungi ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mtakatifu Francis ya mjini Ifakara katika wodi ya wagonjwa mahututi.

Hata hivyo kamanda Chialo amesema dreva amejisalimisha polisi na tayari leo amekwisha fikishwa mahakamani kujibu mashitaka manne ya kusababisha kifo, kusababisha majeruhi wawili na uharibifu wa mali.

MBUNGE WA MIKUMI ACHANGIA SHILINGI MILIONI 27.3KWA MIRADI YA MAENDELEO

MBUNGE WA MIKUMI ACHANGIA SHILINGI MILIONI

Mbunge wa jimbo la Mikumi kwa tiketi ya CCM, bwana Abdulsalam Ameri hadi sasa kwa muda wa miezi kumi akiwa mbunge, amekwisha tumia jumla ya shilingi milioni 27.3 kwa kuchangia miradi ya maendeleo ya kata.

Bwana Ameri amesema jimbo lake la mikumi lina jumla ya kata 14 na yuko katika ziara ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagu kuwa mbunge na kupita kata hadi kata.

Amesema hadi Septemba 20 mwaka huu amekwisha tembelea kata kumi kwa kufanya mikutano ya kuwashukuru na kupata kero kutoka kwa wananchi wa kata husika.

Hivyo amewataka wananchi wa jimbo hilo kuwa uchaguzi umekwisha mwaka 2010 na makundi yamekwisha sasa imebaki kufanyakazi ya kujenga uchumi wa nchi yetu na amewataka viongozi wa serikali za kata wafanye kazi isiyokuwa na jazba.

Aidha mbunge huyo amewaasa viongozi waache kufuata makundi, wafanye kazi waliyotumwa pia amewataka viongozi wa vijiji kuwasomea taarifa ya mapato na matumizi wananchi wa vijiiji vyao kwa kila kipindi cha miezi mitatu ili wananchi wawe na imani na viongozi wao na kuhamasika kujiletea maendeleo.

WANANCHI WA KIDODI WILAYANI KILOSA WACHANGA SHILINGI MILION TATU KWA AJILI YA MRADI WA MAJI.

SHILINGI MILION TATU KWA AJILI YA MRADI WA MAJI.

Jumla ya shilingi mil.3 zimekusanywa kutokana na mchango wa wananchi wa kijiji cha lumango kata ya kidodi wilayani kilosa kwaajili ya mradi wa maji ya mtiririko.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na afisa mtendaji wa kijiji hicho sept 18 mwaka huu katika mkutano wa hadhara uliofanyika katia kata ya kidodi kwa mbunge wa jimbo la mikumi bwana Abdulsalam Amer,imeeleza kuwa kijiji hicho kimepangiwa kuchangia mradi huo kiasi cha shilingi mil 4 na laki 5.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa kwa mbunge wa jimbo hilo imeeleza kuwa wananchi wa kijiji hicho hadi sasa wanadaiwa shilingi mil 1 na laki 5 kwa ajili ya mradi hou.

Diwani wa kata ya kidodi bwana Ibrahim Fatahaki amesema kuwa katika kata hiyo,kijiji cha lumando kinaongoza kwa mchango wa mradi wa maji katika kata ya kidodi.

Wakati huohuo wananchi wa kijijik hicho wamfyatua jumla ya matofali 20000 ya kuchoma kwa ajili ya ujenzi wa zahanati unaotarajia kuanza hivi karibuni.


Hata hivyo mbunge wa jimbo hilo bwana Amer ameahidi kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo kwa kutoa vifaa vya ujenzi.