HII NI BLOG ITAKAYOKUKUTANISHA NA WANAHABARI MBALI MBALI WAKIKUHABALISHA NA KUKUJUZA YALE YANAYOTOKEA SEHEMU MBALI MBALI ZA DUNIA HII..KARIBU KWA KUFAHAMU MENGI ZAIDI KUPITIA HABARI.....
Saturday, September 7, 2013
CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH MOROGORO CHAFANYA TAMASHA LA MICHEZO ILI KUBORESHA MICHEZO NA AFYA ZA WANACHUO.
Thursday, September 5, 2013
CHEKA AKARIBISHWA KWA VURUGU BUNGENI,NGUMI ZACHAPWA.
VURUGU ZA BUNGE LA TANZANIA ZAWAKERA WANANCHI.

Tuesday, September 3, 2013
SERIKALI YAJIBU MAPIGO KWA MTANDAO WA KENYA ULIOANZA KUICHOKONOA TANZANIA
Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari- (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu mtandao wa kijamii wa nchini Kenya ulioituhumu Serikali ya Tanzania.
Tuesday, April 16, 2013
NMB KANDA YA MASHARIKI YATOA MSAADA WA MADAWATI 38 YENYE THAMANI YA TSH MIL 2.5 KATIKA SHULE YA MSINGI MTYANGIMBOLE WILAYANI KILOMBERO
wanafunzi 80 wa darasa la nne na la
tano wa shule ya msingi ya
Mtyangimbole
iliyopo kijiji cha Ikule kata ya
Mngeta wilayani
Kilombero,wanasomea kwenye
banda la nyasi huku wakiwa
wamekaa chini.
HabariKwanza Blog imeshuhudia hali hiyo
wakati wa makabidhiano wa msaada
wa madawati
38 yenye thamani ya shilingi milioni
mbili na laki tano uliotolewa na
Benki ya
Nmb Kanda ya mashariki shuleni
hapo.
Akizungumzia
hali hiyo Mwalimu Mkuu wa shule
hiyo bwana Emanuely Njavike amesema
kuwa wamelazimka
kufanya hivyo kutokana na shule
hiyo kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa
kwani vyumba
vilivyopo kwa sasa ni
viwili ambavyo vinatumiwa kwa
kupokezana kwa darasa la kwanza,la
pili,la tatu
na la sita.
Mwalimu Njavike
amesema kuwa hali hiyo
imewafanya
wanafunzi kutohudhuria masomo
kikamilifu kutokana na miundombinu
ya shule hiyo
kuwa mibovu hususan kipindi hiki
cha masika ambapo maji hujaa
katika vyumba hivyo na kuwafanya
wanafunzi hao kusoma katika
mazingira magumu na hatarishi.
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha
Mtyangimbole Bwana Sangalufu John
Kibonde amesema
kuwa wananchi wa kitongoji hicho
walijenga maboma mawili mara
mbili na
yakabomoka kutokana na mvua za
masika
zinazoendelea kunyesha baada ya
serikali
kuchelewa kumalizia maboma hayo
hali inayowakatisha tamaa wananchi
kuchangia
ujenzi wa shule hiyo.
Shule ya
Mtyangimbole yenye wanafunzi 195
kuanzia
darasa la kwanza hadi la sita
inakabiliwa na upungufu wa vyumba
vitano vya madarasa na matundu
nane ya vyoo.
Hata hivyo maafisa wa benki ya NMB na Mbunge wa viti maalumu kupitia
Chama cha demokrasia
na maendeleo chadema Mheshimiwa
Suzan Kiwanga wamesikitishwa na
hali hiyo na
kusema kuwa shule hiyo inahitaji
msaada wa hali na mali ili
kuwanusuru watoto
hao wanaosoma katika mazingira
magumu na hatarishi
Monday, April 15, 2013
AJINYONGA KUEPUKA MADENI
MTU mmoja aliyejulikana kwa jina la
Karimu Kamwenda(41) mkazi wa
Kitongoji
cha Michenga A kijiji cha Michenga wilayani Kilombero
amejinyonga usiku wa kuamkia
leo kwa kile kinachodaiwa ni kukwepa madeni.
Kwa mujibu Mwenyekiti wa Kijiji cha Michenga
Bwana Iddi Kamila ameiambia
habarikwanza
kuwa kwa maelezo ya Kaka wa
Marehemu huyo, kuwa Marehemu amejinyonga
kwa
kinachosadikiwa kuwa ni kuwa na
madeni mengi aliyokuwa akidaiwa na watu mbalimbali.
Jeshi la polisi Wilayani Kilombero
limethibitisha kuwepo kwa taarifa za
mkazi huyo kujinyonga.
Wakati huo huo kijiji hicho cha
Michenga kinataraji kusoma mapato
na matumizi
ya kijiji mwishoni mwa wiki hii kwa
muujibu wa Mwenyekiti wa kijiji hocho Bwana
Idi Kamila.
Bwana Kamila ameuambia mtandaao
huu kuwa vikao vya ndani
vitakapokamilika
hiii leo taarifa itawekwa hadharani
siku ya kusoma mapato na matumizi
hayo.
KINANA KUONGEA NA WAKAZI WA IFAKARA KESHO
Katibu Mkuu wa Chama cha
Mapinduzi Taifa Bwana
Abdurahaman Kinana kesho
anataji kufanya ziara ya siku moja
Wilayani Kilombero na kuzungumza
na
Wananchi katika eneo la stendi ya
Kwa Makali.
Katibu wa siasa na uenezi CCM
Wilaya ya Kilombero Bwana
Pellegrine Kifyoga
ameiambia Habarikwanza kuwa
lengo la ziara hiyo ni
kuhamasisha ,kuangalia
utekelezaji wa ilani ya chama hicho
na kukagua uhai wa chama na
jumuiya
zake.
Bwana Kifyoga amesema kuwa
Bwana Kinana atafungua mashina ya
wakereketwa
na miradi ya kijamii na baada ya
hapo atazungumza na wananchi
pamoja na
wanachama wa CCM katika mkutano
wa hadhara utakaofanyika saa tisa
alasiri
katika Eneo la Stendi ya Kwa makali
Ifakara Mjini.
Katika Ziara ya Katibu huyo wa CCM
atambatana na Viongozi wa CCM
TAIFA, Katibu
wa NEC Itikadi na uenezi Bwana
Nape Nnauye na Katibu wa Nec
Oganaizesheni
Taifa Bwana Mohamed Seif Khatib.
Amewataka wanachama na wananchi
kwa ujumla kujitokeza kwa wingi
kuwasikiliza
viongozi hao na kupokea maelekezo
yatakayotolewa na viongozi hao
katika
mkutano huo ili waweze kuyafanyia
kazi zaidi
Friday, April 5, 2013
SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO
Sunday, March 17, 2013
TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI KUIWINDA MOROCCO
TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI KUIWINDA MOROCCO
MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/-
WAANGOLA KUCHEZESHA MECHI YA STARS
Saturday, March 16, 2013
WATOTO WALEMAVU WA KITUO CHA BETHELEHEMU WILAYANI KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA
Tuesday, March 12, 2013
WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU
WANAFUNZI WILAYANI KILOMBERO WAHIMIZWA KUONGEZA BIDII KATIKA MASOMO YAO KUEPUKA AIBU YA MATOKEO KATIKA MITIHANI YAO YA KUHITIMU
Monday, March 11, 2013
MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA MSAADA WA VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE
KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA MSAADA WA PIKIPIKI KWA JESHI LA POLIS WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75
Friday, March 8, 2013
WAKANDARASI WAASWA KUFANYA KAZI ZAO KATIKA KIWANGO KINACHOSTAHILI.
Thursday, March 7, 2013
MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO BI AZIMINA MBILINYI KUONGOZA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI HUMO.
SERIKALI YA KIJIJI CHA MCHOMBE YAHUSIKA NA UPOTEVU WA FEDHA JUMLA YA MILIONI 2.19
Wednesday, March 6, 2013
MAZISHI YA MWIGIZAJI ALIYEPOTEA MKOANI NJOMBE YAFANYIKA.
Akizungumza Mara Baada ya Kupatikana Kwa Mwili Huo Afisa Tarafa ya Njombe Mjini Bi Lilian Nyemele Ameishukuru Kampuni ya TANWAT Kwa Namna Ilivyoshiriki Katika Kusaidia Zoezi Hilo Pamoja na Wananchi Wote Walioshiriki.
Mwili wa Marehemu Ulipatikana Leo Majira ya Saa Nane Mchana Ikiwa ni Baada ya Jitihada za Muda Mrefu za Wananchi na Viongozi Kuweza Kuutafuta Mwili Huo Bila Mafanikio Kutokana na Ukosefu wa Vifaa Vya Uokozi.
Akizungumza Mara Baada ya Kuwasili Mkoani Njombe Mtaalam wa Uzamiaji Kutoka Jijini Dar Joseph Mapunda Anasema Kuna Haja Kwa Serikali ya Mkoa wa Njombe Kuanza Kutoa Mafunzo Kwa Wananchi na Wataalam Mbalimbali Ili Kuweza Kupata Wataalam wa Uzamiaji.
Marehemu Mexon Nyekelela Chota Alizama Kwenye Mabwawa Hayo Mnamo March Mosi Mwaka Huu Majira ya Saa Kumi na Moja Jioni Wakati Akiwa na Wenzake Mara Baada ya Kumaliza Shughuli Zao za Sanaa.
Monday, March 4, 2013
PONGEZI KWA AZAM FC KUSONGA MBELE
TIMU YA KIKAPU YA ST JOSEPH MOROGORO YACHAKAZWA 71-16
Tuesday, February 26, 2013
PICHA YA PAMOJA YA BAADHI YA STAFF WA CHUO CHA MTAKATIFU JOSEPH CHA MKOANI MOROGORO.
Friday, November 2, 2012
BAADA YA KIMYA KIREFU SASA JIANDAE KUPATA HABARI ZAIDI.
Saturday, October 1, 2011
SHULE YA SEKONDARI YAKOSA VYOO KWA MIAKA NANE.
Shule ya sekondari ya Mlabani iliyopo kata ya Ifakara wilayani Kilombero, inakabiliwa na uhaba wa vyoo kwa muda wa miaka minne sasa na kuwafanya wanafunzi wa shule hiyo kuwa katika hali ya hatari ya kukumbwa na magonjwa ya mlipuko.
Hayo yameelezwa katika taarifa ya shule hiyo iliyosomwa na makamu mkuu wa shule,hiyo mwalimu Idrissa Lyoko katika mahafali ya kwanza ya shule hiyo kwa mgeni rasmi, imeeleza kuwa shule hiyo ina choo chenye matundu manane tu, ikiwemo matundu sita yanayotumiwa na wanafunzi wa shule hiyo wapatao 635.
Taarifa hiyo imeeleza Kwa sasa shule hiyo inahitaji matundu 28 ya choo
na ina upungufu matundu 22 ya choo.
Risala hiyo imeeleza kati ya wanafunzi hao wavulana 350 na wasichana 285, pia walimu wako kumi, wanaume sita na wanawake wanne, shule ina mchepuo wa sayansi, biashara na sanaa.
Mgeni rasmi katika mahafali hayo ambayo ni ya kwanza katika shule hiyo meneja wa shirika la PLAN INTERNATIONAL Tawi la Ifakara, bwana HAIDARI MFINANGA amesema viongozi wa serikali za vitongoji vilivyopo katika vijiji vya Mlabani na Katindiuka na uongozi wa halmashauri wapange mikakati ya kuiendeleza shule hiyo kimajengo
Bwana Mfinanga amesema shirika lake la Plan halitasaidia tena katika ujenzi wa majengo bali kwa sasa inafadhili watoto wanaosoma, hivyo amewataka jamii na wazazi washirikiane kuleta maendeleo ya shule hiyo kwa njia ya michango.
Tuesday, September 27, 2011
RASIMU YA HESABU KATIKA HALMASHAULI YA WILAYA YA KILOMBERO
RASIMU YA HESABU WILAYA YA KILOMBERO
Jumla shilingi bilioni 15 milioni 690 laki 944,313.00 zimepitishwa na baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya kilombero katika kikao cha kupitisha rasimu ya kitabu cha hesabu za mwisho za halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha ulioisha juni 30 mwaka huu.
Fedha hizo zimepitishwa na baraza la madiwani hii leo katika kikao maalumu cha kupitisha Rasimu ya kitabu cha hesabu za mwisho za Halmashauri kwa mwaka wa fedha ulioisha 20110/2011kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya.
Rasimu hiyo imeonyesha kuwa kiasi hicho cha fedha ni majumuisho ya mali za kudumu ambazo zimefikia kiasi cha shilingi bilioni 10 milioni 499,16,346.00 na mali za muda mfupi shilingi bilioni 5 milioni 191 laki 927,967.00.
Aidha sehemu kubwa ya mali hizo zimetokana na fadha za ruzuku kutoka serikali kuu na michango ya wahisani kiasi cha shilingi bilioni 14 milioni 79 laki 763,492.00 na ziada ilyohifadhiwa ni shilingi bilioni 1 milioni 611 laki 180,821.00.
Friday, September 23, 2011
AFYA WA WANANCHI WA KILOSA HATARINI BAADA YA KUPASUKA KWA BOMBA LA MAFUTA,LIENDALO ZAMBIA.
Jumla ya ekari 1400 za mazao mbalimbali katika kata ya Malolo wilayani Kilosa Mkoani Morogoro,zimeharibiwa na mafuta machafu yanayovuja kutoka katika bomba kubwa linalosafirisha mafuta hayo kutoka Tanzania kwenda Zambia lililopita katika kata hiyo.
Afisa kilimo cha umwagiliaji wa kata hiyo, Bwana Mwelasi amesema bomba hilo la mafuta tangu lipasuke hadi sasa ni muda wa miezi miwili na limeharibu mfumo wa umwagiliaji wa mashamba jumla ya ekari 500 ya mazao ya vitunguu na mahindi.
Bwana Mwelasi ameyataja mazao yaliyoathirika kutokana na kupasuka kwa bomba hilo kuwa ni vitunguu na mahindi ambapo hata kiwango cha uzalishaji wa mazao hayo amesema kuwa kimeshuka.
Afisa kilimo huyo amesema mimea imekauka kutokana na mafuta yanayovuja kutoka katika bomba hilo na kuingia chini ya ardhi na kuathiri mazao na kusababisha kushuka kwa kiwango cha uzalishaji.
Akizungumzia uzalishaji wa mazao katika kata hiyo Amesema hapo awali kabla ya bomba hilo kupasuka ekari moja ilikuwa ikizalisha magunia 70 ya mazao, lakini sasa ekari moja inazalisha gunia 20 ya mazao kiwango ambacho amesema kimeshuka kwa kiasi kikubwa.
Hata hivyo amevitaja Vijiji vilivyoathirika na mafuta hayo kuwa ni Malolo "A", Malolo "B" na Mgogozi ambapo wananchi wanaoishi katika vijiji hivyo wamo hatarini kuharibu afya zao kutokana na maji wanayotumia kwa kunywa na shughuli zinigine.
Kutokana na athari hiyo kutokea Mbunge wa jimbo la Mikumi, bwana Abdulsalam Ameri tayari amekwisha peleka mtambo wake wa kuchimba visima vya maji katika kata hiyo na kila kijiji kati ya vijiji hivyo vitachimbiwa visima viwili na kufanya idadi ya visima sita katika kata hiyo ambavyo vitasaidia kuokoa maisha ya wananchi wa kata hiyo.
UKOSEFU WA WATAALAMU MBALI MBALI KATIKA SEKTA YA KILIMO CHA MIWA NI KIKWAZO KIKUBWA KWA WAKULIMA WA MIWA KILOMBERO
Ukosefu wa Wataalamu wa Uchumi , Mizani na Sheria ni baadhi ya changamoto zinazovikabili vyama vya Wakulima wa Miwa katika Bonde la Kilombero.
Akizungumza katika mahojiano na mwandishi wetu Katibu wa Chama Cha Wakulima wa Miwa cha Msolwa Ujamaa (MUCGA) Modestus Chitemi amesema ili kuwezesha ongezeko la bei kwa Wakulima kwa Uwiano kama ilivyo kwa Nchi Jirani Wataalamu zaidi wanahitajika.
Akitolea mfano wa Nchi ya Malawi, Bwana Chitemi amesema kuwa Wakulima wa Miwa waNchi hiyo wana uwiano wa kupata asilimia Sitini (60) wakati Viwanda vya Sukari vinapata asilimia Arobaini(40).
Ameongeza kuwa kutokuwepo kwa mgao na Ruzuku ya pembejeo kutoka Serikalini katika zao la Miwa ingawa Mahitaji ya mbolea na dawa za magugu ni makubwa sana ni changamoto nyingine inayoikabili vyama vya Wakulima wa Miwa katika Bonde la
Kilombero

Mfanyakazi katika shamba la miwa akiendelea na zoezi la ukataji miwa..(picha juu)
Changamoto nyingine ni ukosefu wa Mtaji kuanzisha na kuendeleza Kilimo cha bega kwa bega na Umwagiliaji na kukosa kasi kubwa ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara na mifereji mashambani.
Mbali ya changamoto hizo katibu huyo amesema kuwa Ajira kwa Wananchi, Idadi ya Wakulima na pato la Mkulima, limeongezeka baada ya ubinafsishaji wa Viwanda na matumizi ya mfumo Mauzo ya miwa kwa uwiano wa mapato.

Shamba la miwa wilayani kilombero..
KCY YATUMIA MILIONI TISINI KWA AJILI YA MISAADA.
Kampuni ya Kilimo Cha Yesu (KCY) iliyopo Mpanga Wilayani Kilombero imetumia jumla ya Shilingi Milioni Tisisni (90,000,000/=) katika Mwaka 2010 kwa ajili ya Misaada mbalimbali.
Akitoa maelezo kuhusu kazi ya Kampuni ya KCY kwenye siku ya Sekta Binafsi Tanazania, Mkurugenzi wa KCY Mpanga Bruno Wicki Bruno amesema wametumia Milioni Ishirini na Laki Tano (20,500,00/=)kwa ajili ya Kusomesha watoto ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha, Milioni Kumi na Saba na Laki Tano (17,500,000/=) misaada ya Dawa kwa walemavu na kusafirisha Wagonjwa na Milioni Kumi na Saba na Laki Tano (17,500,000/=) kusaidia Kanisa.
Shilingi Milioni Thelathini (30,000,000/=) walitumia kufidia hasara katika kampuni ya KCY na Milioni Nne na Laki sita (4,600,000/=)kwa misaada mbalimbali ya wasiojiweza.
Amesema kwa Msimu wa Kilimo uliopita walilima juml;a ya Ekari Elfu NNE mia sita(4600) na wamekopesha Shilingi Milioni Themanini (80,000,000/=) kwa Marejesho ya Riba ya Shilingi Elfu Tano(5,000) kwa Ekari kwa Vikundi kumi vyenye jumla ya Ekari elfu mbili (2000).
Kampuni ya KCY inayojishughulisha na maendeleo na kufundisha neono la Mungu kwa maneno na Matendo imeanzishwa mwaka 2004 kwa lengo la kusaidia Watanzania kuendelea katika shughuli za Kilimo.
TANZANIA KUNUFAIKA NA MSAADA WA EURO MILIONI 15 KUTOKA SERIKALI YA UHOLANZI
TANZANIA itafaidika na msaada wa Euro milioni 15 ambazo ni sawa na (zaidi ya Sh bilioni 30 za kitanzania ) kutoka Serikali ya Uholanzi kugharamia mradi wa Kujenga Uwezo kwa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini unaojulikana kwa jina la NICHE.
Meneja wa mradi huo, Ute Jansen ameyasema hayo alipotembelea Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro, kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao kwa Mzumbe, unatoa ufadhili kwa Shule ya Biashara na kuboresha mafunzo ya utawala wa Serikali za Mitaa.
Jansen amesema ana matumaini makubwa kuwa mradi huo utakapokamilika, utaboresha sekta
zilizoainishwa kwenye mradi huo ambazo ni kujenga uwezo katika kutoa elimu kuhusu afya, sekta binafsi na Serikali za Mitaa.
Kwa upande wake, Msimamizi wa mradi huo nchini kupitia Shirika la NUFFIC, Johanna Van Nieuwenhuizen, amesema Uholanzi imeridhishwa na jinsi Tanzania inavyoitumia misaada kutoka nchini mwake, hivyo kujihakikishia fursa zaidi za kusaidiwa katika miradi mbalimbali.
Naye Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa Mugishi Nkwabi Mgasa, aliyemwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo, ameishukuru Serikali ya Uholanzi kwa kufadhili mradi huo na kueleza kuwa ufadhili huo una maana kubwa kwa chuo hicho kwa sababu utapanua uwezo wa chuo hicho katika kutoa mafunzo ya biashara na utawala wa Serikali za Mitaa
Thursday, September 22, 2011
PAMBAZUKO FM RADIO 90.7 MHz IFAKARA YAZIDI KUONGEZA USIKIVU.
Kituo cha radio mjini Ifakara Mkoani Morogoro Panbazuko Fm sterio 90.7MHz, kwa sasa wameongeza usikivu wao kwa lengo la kuwafikia wananchi walio wengi katika sehemu mbali mbali.
Wakizungumza na mtandao huu kwa nyakati tofauti,mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho bi THERESIA MAKUNGU amesema kwa sasa wameweza kuwa na usikivu mzuri na kuwafikia wananchi walio wengi mara baada ya kumaliza kufunga mitambo yao mipya.
Bi Makungu amesema lengo kubwa la kituo chao ni kuwahabarisha wananchi yale yanayokuwa yakiendelea katika maeneo yao na duniani kwa ujumla.
Mafundi wakiimarisha mitambo ya radio pambazuko fm ifakara(picha juu)
Nae mwariri mkuu wa kituo hicho bwana ELIAS MAGANGA amesema kwa sasa wamekuwa katika wigo mpana katika kuwahabarisha wananchi wa maeneo mbali mbali ambako radio hiyo imekuwa ikirusha matangazo yake.
Maganga amesisitiza kuwa lengo kubwa la kutoa habari ni kuwajulisha wananchi yale yanayokuwa akiiendelea katika sehemu mbali mbali katika maeneo yao,na kuongeza kuwa siku zote chombo cha habari hakina ugomvi na yeyote bali vimekuwa vikitoa yale mazuri na maovu yanayofanywa katika jamii.
Wakati huo huo aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kilombero na mkuu mpya wa mkoa wa Mwanza mheshimiwa Evarist Ndikilo ameipongeza radio pambazuko kwa juhudi zake katika kuwaelimisha na kuwahabarisha wananchi wa wilaya ya kilombero.
Ndikilo ameyasema hayo katika taarifa yake fupi aliyoitoa moja kwa moja kupitia kituo hicho cha radio katika kipindi cha JIONI LEO siku ya alhamisi alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya ya kilombero katika kuwaaga kwake.
Radio Pambazuko fm kwa sasa inasikika katika mikoa ya Morogoro,Lindi ,Ruvuma na Iringa hususani katika wilaya mpya ya KILOLO
Sehemu ya antena mpya za pambazuko fm radio katika picha ya anga...
SEHEMU YA MIJI YETU INAVYOONEKANA KATIKA PICHA ZA ANGA.
Hii ni baadhi ya mitaa katika miji yetu hapa nchini Tanzania,sehemu hii inawakilisha maeneo mengi ambayo maisha ya mtanzania wa kawaida huyaendesha kila siku katika kujitafutia kipato chake cha siku..
Na hii ni kutoka katika mkoa mpya wa NJOMBE mooja ya mikoa mipya inayopatikana hapa nchini kwetu.
MKUU MPYA WA MKOA WA MWANZA AWAOMBA WAZEE KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WAPYA KILOMBERO
Ombi limetolewa kwa wazee kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkuu wa wilaya atakayekuja kuongoza katika wilaya ya kilombero pamoja na viongozi wengine wanaobaki kama walivyoshirikiana vizuri na mkuu wa wilaya aliyepita.
Ombi hilo limetolewa na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kilombero ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa mwanza mhandisi Evarist Ndikilo katika mkutano wa kuwaaga na kuwashukuru wazee wa wilaya ya kilombero uliyofanyika leo katika ukumbi wa jamosi mjini Ifakara.
Mhandisi ndikilo amewaeleza wazee, kuwa kwa kipindi cha miaka mitano aliyofanya kazi katika wilaya amefanikiwa kuleta maendeleo katika sekta ya elimu,kilimo,afya,miundombinu na mazingira,
Mbali na mafanikio hayo mhandisi ndikilo hakusita kuwaeleza wazee changamoto ambazo zinaikabili wilaya ya kilombero zikiwemo umaskini,migogoro ya Ardhi na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na mifugo na kilimo cha umwagiliaji.
Kwa upande wao wazee wamezitaja changamoto zinazowakabili ikiwemo kutibiwa bure na ajali za bodaboda zinazotokea mara kwa mara ,lakini pia wamemshukuru mhandisi Ndikilo kwa ushirikiano aliouonesha kwa wazee kwa kipindi cha miaka mitano aliyokuwa akifanya kazi wilayani hapa na kumtakia kazi njema huko aendako.
SHIRIKA LA MICHE LA ITALY LATOA KOMPYUTA KWA SHULE YA MSINGI MJINI IFAKARA
Shule ya msingi ya Madukani iliyopo kata ya Ifakara wilayani Kilombero, hivi karibuni imepokea Kompyuta kumi na Printer moja kutoka shirika la MICHE la Italia.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, bibi Ester Nuruva ameueleza mtandao huu kuwa kompyuta walizopata kutoka katika shirika hilo watazitumia kwaajili ya kuwafunza wanafunzi wa kuanzia darasa la tatu hadi darasa la saba.
Aidha mwalimu mkuu huyo amesema hapo awali shule hiyo ilikuwa inafundisha somo la TEHAMA ambapo ilikuwa inahusu kompyuta kwa nadharia, kutokana na kupata msaada huo wa kompyuta sasa somo hilo litafanywa kwa vitendo.
Bibi Nuruva amesema aliyekabidhi msaada huo kwa shule hiyo alikuwa Rais wa shirika hilo, bibi Eva Maria Bardeleben kutoka Italia.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Madukani, amelishukuru shirika hilo kwakuwa na moyo wa kujitolea kwa upande wa sekta ya elimu, hivyo ameyaomba mashirika mengine kuwa na moyo wa kutoa misaada hususani katika sekta ya elimu.
AFARIKI KWA AJALI YA PIKI PIKI WILAYANI KILOMBERO-IFAKARA
Mtu mmoja amekufa na wawili wamejeruhiwa kutokana na ajali ya gari iliyomgonga mwendesha pikpiki jana (20/9/011) eneo la kwa shungu kata ya Kibaoni wilayani Kilombero.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Adolfina Chialo ameieleza radio pambazuko kuwa ajali hiyo imetokea jana majira saa tisa na nusu alasiri baada ya gari hilo lenye usajili wa Na.T 184 AAC lilikuwa likiendeshwa na David Mtazama(39) mkazi wa kitongoji cha Mkuya na kumgonga mwendesha pikipiki Emanuel Amnungi(17) mkazi wa Mlabani aliyekuwa akiendesha pikipiki yenye usajili ya Na. T590 DRM ainaya TIBETA.
Aidha Chialo amemtaja aliyekufa katika ajali hiiyo ni Abdulazaki Mgoima(4) aliyekuwa amebebwa na mama yake Anna Sabu ambaye amejeruhiwa wakati wamebebwa katika pikipiki hiyo wakitokea mjini Ifakara kuelekea nyumbani kwao Kijiji cha Mbasa
Kamanda huyo amesema gari lililogonga pikipiki lilikuwa likitokea mjini Ifakara kuelekea Kibaoni na imegonga pikipiki kwa nyuma.
Amewataja majeruhi waliiojeruhiwa katika ajali hiyo ni Anna Sabu abiria wa pikipiki na dreva wa pikipiki Emanuel Mnungi ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mtakatifu Francis ya mjini Ifakara katika wodi ya wagonjwa mahututi.
Hata hivyo kamanda Chialo amesema dreva amejisalimisha polisi na tayari leo amekwisha fikishwa mahakamani kujibu mashitaka manne ya kusababisha kifo, kusababisha majeruhi wawili na uharibifu wa mali.
MBUNGE WA MIKUMI ACHANGIA SHILINGI MILIONI 27.3KWA MIRADI YA MAENDELEO
Mbunge wa jimbo la Mikumi kwa tiketi ya CCM, bwana Abdulsalam Ameri hadi sasa kwa muda wa miezi kumi akiwa mbunge, amekwisha tumia jumla ya shilingi milioni 27.3 kwa kuchangia miradi ya maendeleo ya kata.
Bwana Ameri amesema jimbo lake la mikumi lina jumla ya kata 14 na yuko katika ziara ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagu kuwa mbunge na kupita kata hadi kata.
Amesema hadi Septemba 20 mwaka huu amekwisha tembelea kata kumi kwa kufanya mikutano ya kuwashukuru na kupata kero kutoka kwa wananchi wa kata husika.
Hivyo amewataka wananchi wa jimbo hilo kuwa uchaguzi umekwisha mwaka 2010 na makundi yamekwisha sasa imebaki kufanyakazi ya kujenga uchumi wa nchi yetu na amewataka viongozi wa serikali za kata wafanye kazi isiyokuwa na jazba.
Aidha mbunge huyo amewaasa viongozi waache kufuata makundi, wafanye kazi waliyotumwa pia amewataka viongozi wa vijiji kuwasomea taarifa ya mapato na matumizi wananchi wa vijiiji vyao kwa kila kipindi cha miezi mitatu ili wananchi wawe na imani na viongozi wao na kuhamasika kujiletea maendeleo.
WANANCHI WA KIDODI WILAYANI KILOSA WACHANGA SHILINGI MILION TATU KWA AJILI YA MRADI WA MAJI.
Jumla ya shilingi mil.3 zimekusanywa kutokana na mchango wa wananchi wa kijiji cha lumango kata ya kidodi wilayani kilosa kwaajili ya mradi wa maji ya mtiririko.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na afisa mtendaji wa kijiji hicho sept 18 mwaka huu katika mkutano wa hadhara uliofanyika katia kata ya kidodi kwa mbunge wa jimbo la mikumi bwana Abdulsalam Amer,imeeleza kuwa kijiji hicho kimepangiwa kuchangia mradi huo kiasi cha shilingi mil 4 na laki 5.
Taarifa hiyo iliyowasilishwa kwa mbunge wa jimbo hilo imeeleza kuwa wananchi wa kijiji hicho hadi sasa wanadaiwa shilingi mil 1 na laki 5 kwa ajili ya mradi hou.
Diwani wa kata ya kidodi bwana Ibrahim Fatahaki amesema kuwa katika kata hiyo,kijiji cha lumando kinaongoza kwa mchango wa mradi wa maji katika kata ya kidodi.
Wakati huohuo wananchi wa kijijik hicho wamfyatua jumla ya matofali 20000 ya kuchoma kwa ajili ya ujenzi wa zahanati unaotarajia kuanza hivi karibuni.
Hata hivyo mbunge wa jimbo hilo bwana Amer ameahidi kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo kwa kutoa vifaa vya ujenzi.
