Monday, April 15, 2013

AJINYONGA KUEPUKA MADENI

MTU mmoja aliyejulikana kwa jina la
Karimu Kamwenda(41) mkazi wa
Kitongoji
cha Michenga A kijiji cha Michenga wilayani Kilombero
amejinyonga usiku wa kuamkia
leo kwa kile kinachodaiwa ni kukwepa madeni.

Kwa mujibu Mwenyekiti wa Kijiji cha Michenga
Bwana Iddi Kamila ameiambia
habarikwanza
kuwa kwa maelezo ya Kaka wa
Marehemu huyo, kuwa Marehemu amejinyonga
kwa
kinachosadikiwa kuwa ni kuwa na
madeni mengi aliyokuwa akidaiwa na watu mbalimbali.

Jeshi la polisi Wilayani Kilombero
limethibitisha kuwepo kwa taarifa za
mkazi huyo kujinyonga.

Wakati huo huo kijiji hicho cha
Michenga kinataraji kusoma mapato
na matumizi
ya kijiji mwishoni mwa wiki hii kwa
muujibu wa Mwenyekiti wa kijiji hocho Bwana
Idi Kamila.

Bwana Kamila ameuambia mtandaao
huu kuwa vikao vya ndani
vitakapokamilika
hiii leo taarifa itawekwa hadharani
siku ya kusoma mapato na matumizi
hayo.

No comments:

Post a Comment