Friday, April 5, 2013

SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO

SHILINGI BILIONI 3.3 KUTUMIKA KATIKA MLADI WA UMWAGILIAJI KILOMBERO .

JUMLA ya Fedha shilingi Bilioni 3 Milioni 396 na Laki 9 na Elfu 9 Mia 2 na Tano zitatumika kama Gharama ya Ujenzi wa  Skimu ya Umwagiliaji katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa Wilayani Kilombero.

Kwa muujibu wa Taarifa ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero juu ya Mradi wa Ujenzi wa  Banio na Mfereji wa Umwagiliaji imeeleza  kuwa fedha zilizopatikana mpaka sasa ni Milioni 510 Laki 2 na Elfu 61 Mia 3 na Sabini na Tano Huku fedha zinazohitajika kukamilisha Ujenzi wa Skimu zikiwa ni Bilioni 2 milioni mia 916 Laki 6 na Elfu Arobaini na Saba Mia 8 na Thelathini na Tatu.

Taarifa imefafanua kuwa kati ya fedha hizo shilingi Milioni 416 na Laki 4 Elfu Sitini na Saba na Mia 3 Sabini na moja zimetumika katika Ujenzi wa Miundombinu Mfereji Mkuu Mita 900, Mifereji ya Kati 3 Mita 925 na Maumbo mbalimbali 12.

 Sehemu ya ujenzi wa mladi wa umwagiliaji wilayani kilombero  
(picha na Henry Bernard Mwakifuna.)
Mradi huo utakaosaidia upatikanaji wa uhakika wa Chakula na ongezeko la Kipato kuondokana na Kilimo cha kutegemea Mvua utasaidia Kaya 1204.

Mradi huo wenye eneo la Ukubwa wa Hekta 675 umepitia hatua mbalimbali tangu  Mwaka 1975 ukiwa chini ya Wachina walioanzisha Kituo cha Mafunzo ya kilimo ukipitia hatua mbalimbali unataraji kukabidhiwa Mwishoni mwa Mwezi ujao.

No comments:

Post a Comment