Friday, September 19, 2014

MAHAFARI YA DARASA LA SABA KATIKA SHULE YA MSINGI KICHANGANI NA MKWATANI ZILIZOPO WILAYANI KILOSA

Wahitimu wa darasa la saba katika shule mbili za  msingi za mkwatani na kichangani zilizopo wilayani kilosa mkoani morogoro wametakiwa kuwa makini kwa kipindi hiki ambacho wamehitimu elimu ya msingi wakiwa wanasubili  wakiwa nyumbani kwa kungojea matokeo yao.

                             Waitimu wa darasa la saba wa shule zote mbili mkwatani na kichangani
Hayo yamesemwa na aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo  Faresi Makene alipokuwa akiwapa wosia wahitimu hao wa darasa la saba September 19 mwaka huu katika viwanja vya shule ya msingi kichangani ambapo katika shule ya msingi kichangani waliohitimu ni 72 na katika shule ya msingi mkwatani wanafunzi waliohitimu ni 22.
Mwalimu mkuu wa shule ya mkwatani aliyesimama akifuatiwa na mgeni Rasmi akifuatiwa na mwenyekiti wa shule ya msingi kichangani Swedy Sawasawa na wa mwisho ni  Mwalimu wa shule ya msingi kichangani Saidy Mkalimoto
                  Baadhi ya wazazi wakiwa wanawashuhudia watoto wao wakihitimu elimu ya msingi
                                      Wanafunzi wa darasa la sita wakiwa wanacheza muziki


Katika mahafari hayo pia Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mkwatani  Sophia Mkwemba amewataka wazazi na viongozi wa vijiji kuwapokea watoto hao huko majumbani na kuwa nao makini kwa kuedelea 



wanafunzi na wazazi waliokusanyika kuwaaga wahitimu wa darasa la saba katika viwanja vya shule ya msingi kichangani.
kuwapa na kuwafunza maadili yaliyo mema ili kuwaandaa na maisha ya baadae na kuwataka wazazi 
kujiandaa mapema pindi matokeo yanapotoka ili wawasomeshe vizuri watoto bila matatizo.

                                           Mzazi akifurahi na mwanaye mara baada ya sherehe
   kikundi cha ngoma cha wanafunzi wa darasa la nne wakitumbuiza katika sherehe hiyo ya mahafari ya darasa la saba 2014

No comments:

Post a Comment