Wednesday, September 3, 2014

WANANCHI WA WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WACHOSHWA NA UONGOZI ULIOPO MADARAKANI KWA KUSHINDWA KUTATUA KERO ZA WANANCHI



Wanakijiji wa ulaya mbuyuni  kata ya ulaya wilayani kilosa mkoani morogoro wameilalamikia serikali ya kijiji na Tarafa kwa kutowatatulia mgogoro wao uliopo unaowahusu wafugaji kuwavamia katika maeneo yao ya kilimo.
                                                    Mifugo ikiwa inashambulia zao la mbaazi

Wakitoa malalamiko yao kwa Jazba September 2 mwaka huu kwenye mkutano wa kijiji ulioitishwa na Afisa Tarafa Baadhi ya wakulima katika kijiji hicho cha ulaya mbuyuni Twist Twaha Kilabeba,Steven Mzuma na Omary Mbwana alimaarufu kwa jina la [Gulamali] wamesema kuwa wamechoshwa na uongozi uliopo madarakani hasa uongozi wa kijiji kwani umeonyesha dalili za kushindwa kutatua mgogoro wao kwa muda mrefu hali ambayo inawafanya kukosa amani katika mashamba yao na uhai wao kiujumla kwani wafugaji hao wa jamii ya kimasai huwatishia wakulima hao.
                    Baadhi ya mazao aina ya mbaazi ikiwa imeharibiwa na mifugo aina ya ng'ombe

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amesema kuwa wafugaji waliokuwa maeneo ya wafugaji wanapaswa kuondoka haraka sana kwani kisheria watakamatwa na kufunguliwa mashtaka na kuongeza kuwa amewaagiza maafisa tarafa kwa ajili ya utekelezaji wa kuwaondoa wafigaji hao na ameongeza kuwa wananchi hawapaswi kutoa maeneo yao kwa ajili ya kulisha mifugo na badala yake wakibainika watakamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani na kwa upande wa viongozi kama wakibainika kuwapokea wafugaji kinyemela watawajibishwa kinidhamu kufunguliwa mashtaka mahakamani pamoja na kuwaondoa madarakani.
Aidha Afisa tarafa wa Tarafa ya Ulaya Raphael Mvulungu amewaomba wananchi kutuliza jazba zao na kuwaomba kutoa ushilikiano wao kwa ajili ya kuwaondoa wafugaji hao wa jamii ya kimasai na kusema kuwa wafugaji hao hawawezi kuleta ubishi wa kuondoka ila kutakuwa na watu watakao kuwa wanawakingia kifua na kusema kuwa kuna baadhi ya wananchi wananufaika na wafugaji hao na baadhi yao walimwambia wafugaji hao wasiondoke walipoambiwa kuna mchakato wa kuwaondoa.
Aidha Mvulungu ameongeza kuwa katika zoezi la kuwaondoa wafugaji hao ataanza na wale ambao wametoa maeneo yao kwa ajili ya kuwapa wafugaji hao kwa ajili ya kujenga mazizi na wale wakulima ambao wanatoa maeneo yao kwa ajili ya kulishia mifugo na kuongeza msisitizo kuwa atahakikisha wafugaji hao wanaondoka katika kijiji hicho kikubwa amewaomba ushilikiano wananchi kwa ajili ya kuwaondoa wafugaji hao.

No comments:

Post a Comment