Wednesday, August 27, 2014

VIONGOZI WATAKIWA KUACHA KUJALI MASLAHI YAO BINAFSI

Viongozi wametakiwa kuacha kufanya kazi kwa maslahi yao binafsi badala yake wametakiwa kuwajibika kwa ajili ya maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
                                                Wanafunzi wa shule ya sekondari ukwiva
Hayo yamesemwa na Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvurungu august 26 mwaka huu na amewataka viongozi kusimamia miradi ya maendeleo katika maeneo yao ambapo amewataka viongozi wa Kata ulaya kusimamia miradi hiyo ya maedeleo iliyokuwa viporo vya muda mrefu katika maeneo yao hasa ujenzi wa nyumba za walimu ambao ni mradi wa muda mrefu lakini bado hauja kamilika.
              Baadhi ya majengo ya nyumba za walimu ambayo bado hayajamaliziwa katika ujezi wake

Aidha mkuu wa shule ya ukwiva Liberath Ngure ambapo ndipo kwenye ujenzi wa nyumba za walimu ambazo hazimaliziki kwa ujenzi wake amesema kuwa shule hiyo ya ukwiva inakabiliwa na changamoto nyingi lakini lakini changamoto hizo hazifanyiwi kazi na viongozi na kusema kuwa Mtendaji wa kata alishaahidi ahadi nyingi na hakutekeleza ahadi hizo na kusema kuwa alishamuandikia barua  tar 28/05/2014 kutoka katika kamati ya ujenzi inayohusiana na ujenzi wa nyumba tatu [3] za walimu ambapo ambayo barua hiyo ilikuwa ikimkumbusha kuhusu ujenzi wa nyumba hizo lakini kukawa hakuna taarifa yoyote ya utekelezaji.
                                                 Mkuu wa shule ya ukwiva Liberath Ngure
Naye mwenyekiti wa kamati ya ujenzi shuleni hapo Timotheo Mahembula amesema kuwa Halmashauri ilishatoa fedha kwa ajili ya umaliziaji wa nyumba hizo lakini fedha hizo zilitumika kwa shughuli nyingine jambo ambalo linaleta sitofahamu katika urudishaji wa fedha hizo za umaliziaji wa majengo hayo na kuongeza kuwa Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kilosa Amer Mubarack na alimwagiza mtendaji kutafuta njia ya upatikanaji wa fedha ya umaliziaji wa nyumba hizo lakini halmashauri ilishamaliza swala hilo la ujenzi wa nyumba.
                     Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa shule ya sekondari ukwiva Timotheo Mahembula

No comments:

Post a Comment