Saturday, April 22, 2017

WANAKIJIJI WA KIJIJI CHA MBWADE WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WAILALAMIKIA SERIKALI KWA KUTOKUWA NA VIONGOZI WA SERIKALI YA KIJIJI

Wakazi wa kijiji cha mbwade wilayani kilosa mkoani morogoro wailalamikia serikali kwa kutokuwa na wenyeviti wa vitongoji na kusababisha kushuka kwa maendeleo katika kijiji Chao kwa kukosa wawakilishi katika vikao vya halmashauri ya kijiji.
Mmoja kati ya wakazi hao aliyeomba jina lake Lihifadhiwe amesema kuwa chanzo cha kijiji hicho kutokuwa na wenyeviti wa vitongoji nikutokana uchaguzi wa mwaka 2014 wa ngazi ya serikali ya mitaa kudai kuwa kuvamiwa nawatu ambao si wakazi wa kijiji hicho ambao walipiga kura jambo ambalo liliwafanya wakazi wa eneo hilo kugomea uchaguzi kutokana na watu hao kuonekana kupiga kura kuchagua mgombea kwa maslahi yao binafsi.

Kwa upande wake kaimu mtendaji wa kijiji hicho Huruma Kandili amesema kijiji hicho kina jumla ya vitongoji vitano ambavyo ni madoto lunch, mkwajuni, kichangani, usagarani, na mtapenda kati ya vitongoji vyote vitano kimoja kina mwenyekiti wa kitongoji ambacho ni kitongoji cha madoto lunch kwa upande wake amesema kuwa kijiji chake hakina wenyeviti wa vitongoji nikutokana na wanakijiji kuvunja masanduku yakupigia kura wakidai kuwa Kuna watu waliovamia uchaguzi ambao si wakazi wa kijiji hicho jambo ambalo amelikanusha na ameeleza kuwa watu hao ni wakazi wa kijiji hicho ila kijiji hicho kina jamii mbili ya wakulima na wafugaji hivyo jamii ya wafugaji watu wakuhama hama wakitafuta malisho yamifugo yao hivyo Muda wa uchaguzi walirudi kwa ajili yakufanya uchaguzi katika kijiji Chao.

Alipotafutwa mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya kilosa Kesi Juma Mkambala kuelezea ukweli wa taarifa hii amesema kuwa yeye hana taarifa kuhusiana na tatizo hilo na ameahidi kulifuatilia.

No comments:

Post a Comment