Friday, February 14, 2014

MKURUGENZI MTENDAJI WA WILAYA YA KILOSA AMETAKIWA KUWAITA WALIMU ILI KUWAELEZA UKWELI WA MATATIZO YAO.


Mkurugenzi mtendaji  wa halmashauri ya wilaya ya kilosa masalu mayaya,ametakiwa kuwaita walimu wote wa wilaya ya kilosa ili kuweza kuwaeleza matatizo yao na kuyatafutia ufumbuzi.

Wito huo umetolewa Februari 13 mwaka huu na mwenyekiti wa halmashauri wa wilaya kilosa mheshimiwa Amer Mubarak katika kikao cha kamfed kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo wakati kamfed ilipokuwa ikikabidhi vitabu vya wanafunzi wa sekondari .
Mubarak emesema kuwa kufanya hivyo kutasaidia kujua matatizoyanayowakabili na kuyatafutia ufumbuzi,lengo likiwa ni kuongeza ufaulu mashuleni.
Pia amezitaka bodi za shule kuwa makini nakupa ulewa  wa matatizo yashule zao na kujaribu kutatua na ikishindikana wafike wilayanikuomba nsaada.
;
Aidha mwenyekiti wa halmashuri hiyo ametaka wananchi wahamasishwe kujenga nyumba za walimu karibu na shule ili kuwapa wepesi katika kufanya kazi yao ya kufundisha.

No comments:

Post a Comment