Friday, February 14, 2014

WILAYA YA KILOSA NA WILAYA MPYA YA GAIRO WAMEPOKEA MSAADA WA VITABU AROBAINI NA SABA ELFU NA THELATHINI


      Jumla ya vitabu arobaini na saba elfu na thelathini February 13 mwaka huu  vimetolewa kwa shule za sekondari  wa kumi na tisa wilayani kilosa na shule sita wilaya mpya ya Gairo.

      Vitabu hivyo vimetolewa na shirika la camfed ambalo linashughulikia kwa kuwasaidia watoto walio mashuleni wasio na uwezo licha ya kutoa vitabu na vifaa vingine mashuleni ,pia shirika hilo hutoa karo za shule na mavazi kwa wanafunzi hao.
        Akikabidhi vitabu hivyo kwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kilosa Amer  Mbaraka Afisa mradi wa kamfed ambaye pia ni mlezi wa kafed mkoani morogoro Deogratius john amesema kuwa kamfed imedhamilia  Nyanja ya elimu ili kufanikisha mpango wa serikali wa matokeo makubwa sasa  yaani [BRN].
         Kati ya vitabu vilivyotolewa ni pamoja na Dunia yangu bora,How to read English,English study guide,mathematical study guide na biology studyguide
Pia bwana Deogratius John amewataka walimu kupanga mkakati bora kwa kila mwanafunzi apate vitabu hivyo na kuvitumia ipasavyo.

No comments:

Post a Comment