Saturday, May 17, 2014

WANACHAMA WA DECI WAENDELEA KULALAMIKIA SERIKALI KUHUSU PESA WALIZOZULUMIWA



Waliokuwa  wanachama wa chama cha kupanda  na kuvuna DECI Wilayani Kilosa wameoiomba serikali iwarejeshee pesa zao kama ilivyowaahidi au itoe tamko lolote juu ya pesa zao ili wafahamu kinachoendelea.

Wakizungumza na HABARIKWANZA baadhi ya wanachama hao wamesema serikali  imekaa kimya kwa muda mrefu kitu ambacho kinawapa wasiwasi wa kurejeshewa pesa zao kama serikali ilivyowaahidi.

Mmoja wa wanachama hao Nassoro Machengo ambaye alipanda zaidi ya milioni moja amesema baada ya serikali kuthibitisha na kuifungia taasisi hiyo na kuipeleka mahakamani ili ahidi kurejesha pesa kwa wananchi waliopanda ambacho wanavielelezo mara tu kesi hiyo itakapokamilika .

Machengo amesema wanashangazwa na ukimya wa serikali wakati kesi imeshakamilika na serikali imeshindwa kufanya hivyo wanaomba serikali iwarudishie pesa kama ilivyo ahidi au itoe tamko lolote juu ya kinachoendelea kwa kukaa kwao kimya kinawapa wasiwasi na kuhisi kuwa hawatapata tena pesa hizo .

Takribani miaka 7 iliyopita kuiibuka taasisi ya kifedha ya DECI iliyokuwa ikijiendesha katika utaratibu wa kupanda na kuvuna pesa ambapo wananchi mbalimbali waliwekeza pesa kwa  lengo la kuvuna pesa zaidi , lakini taasisi hiyo ilikuwa ikiendeshwa kinyume na taratibu za kisheria hivyo serikali ilisimamisha kufanya shughuli hizo huku ikiwa imekusanya  mabilioni ya watanzania.

No comments:

Post a Comment