Thursday, September 22, 2011

AFARIKI KWA AJALI YA PIKI PIKI WILAYANI KILOMBERO-IFAKARA

AJALI YA PIKI PIKI WILAYANI KILOMBERO-IFAKARA

Mtu mmoja amekufa na wawili wamejeruhiwa kutokana na ajali ya gari iliyomgonga mwendesha pikpiki jana (20/9/011) eneo la kwa shungu kata ya Kibaoni wilayani Kilombero.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Adolfina Chialo ameieleza radio pambazuko kuwa ajali hiyo imetokea jana majira saa tisa na nusu alasiri baada ya gari hilo lenye usajili wa Na.T 184 AAC lilikuwa likiendeshwa na David Mtazama(39) mkazi wa kitongoji cha Mkuya na kumgonga mwendesha pikipiki Emanuel Amnungi(17) mkazi wa Mlabani aliyekuwa akiendesha pikipiki yenye usajili ya Na. T590 DRM ainaya TIBETA.

Aidha Chialo amemtaja aliyekufa katika ajali hiiyo ni Abdulazaki Mgoima(4) aliyekuwa amebebwa na mama yake Anna Sabu ambaye amejeruhiwa wakati wamebebwa katika pikipiki hiyo wakitokea mjini Ifakara kuelekea nyumbani kwao Kijiji cha Mbasa

Kamanda huyo amesema gari lililogonga pikipiki lilikuwa likitokea mjini Ifakara kuelekea Kibaoni na imegonga pikipiki kwa nyuma.

Amewataja majeruhi waliiojeruhiwa katika ajali hiyo ni Anna Sabu abiria wa pikipiki na dreva wa pikipiki Emanuel Mnungi ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mtakatifu Francis ya mjini Ifakara katika wodi ya wagonjwa mahututi.

Hata hivyo kamanda Chialo amesema dreva amejisalimisha polisi na tayari leo amekwisha fikishwa mahakamani kujibu mashitaka manne ya kusababisha kifo, kusababisha majeruhi wawili na uharibifu wa mali.

No comments:

Post a Comment