Friday, September 23, 2011

UKOSEFU WA WATAALAMU MBALI MBALI KATIKA SEKTA YA KILIMO CHA MIWA NI KIKWAZO KIKUBWA KWA WAKULIMA WA MIWA KILOMBERO

UKOSEFU WA WATAALAMU MBALI MBALI TATIZO KWA WAKULIMA WA MIWA KILOMBERO
Ukosefu wa Wataalamu wa Uchumi , Mizani na Sheria ni baadhi ya changamoto zinazovikabili vyama vya Wakulima wa Miwa katika Bonde la Kilombero.

Akizungumza katika mahojiano na mwandishi wetu Katibu wa Chama Cha Wakulima wa Miwa cha Msolwa Ujamaa (MUCGA) Modestus Chitemi amesema ili kuwezesha ongezeko la bei kwa Wakulima kwa Uwiano kama ilivyo kwa Nchi Jirani Wataalamu zaidi wanahitajika.

Akitolea mfano wa Nchi ya Malawi, Bwana Chitemi amesema kuwa Wakulima wa Miwa waNchi hiyo wana uwiano wa kupata asilimia Sitini (60) wakati Viwanda vya Sukari vinapata asilimia Arobaini(40).

Ameongeza kuwa kutokuwepo kwa mgao na Ruzuku ya pembejeo kutoka Serikalini katika zao la Miwa ingawa Mahitaji ya mbolea na dawa za magugu ni makubwa sana ni changamoto nyingine inayoikabili vyama vya Wakulima wa Miwa katika Bonde la
Kilombero

Mfanyakazi katika shamba la miwa akiendelea na zoezi la ukataji miwa..(picha juu)
Changamoto nyingine ni ukosefu wa Mtaji kuanzisha na kuendeleza Kilimo cha bega kwa bega na Umwagiliaji na kukosa kasi kubwa ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara na mifereji mashambani.

Mbali ya changamoto hizo katibu huyo amesema kuwa Ajira kwa Wananchi, Idadi ya Wakulima na pato la Mkulima, limeongezeka baada ya ubinafsishaji wa Viwanda na matumizi ya mfumo Mauzo ya miwa kwa uwiano wa mapato.

Shamba la miwa wilayani kilombero..

No comments:

Post a Comment