Friday, September 23, 2011

KCY YATUMIA MILIONI TISINI KWA AJILI YA MISAADA.

KCY YATUMIA MILIONI TISINI KWA AJILI YA MISAADA MBALI MBALI.

Kampuni ya Kilimo Cha Yesu (KCY) iliyopo Mpanga Wilayani Kilombero imetumia jumla ya Shilingi Milioni Tisisni (90,000,000/=) katika Mwaka 2010 kwa ajili ya Misaada mbalimbali.

Akitoa maelezo kuhusu kazi ya Kampuni ya KCY kwenye siku ya Sekta Binafsi Tanazania, Mkurugenzi wa KCY Mpanga Bruno Wicki Bruno amesema wametumia Milioni Ishirini na Laki Tano (20,500,00/=)kwa ajili ya Kusomesha watoto ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha, Milioni Kumi na Saba na Laki Tano (17,500,000/=) misaada ya Dawa kwa walemavu na kusafirisha Wagonjwa na Milioni Kumi na Saba na Laki Tano (17,500,000/=) kusaidia Kanisa.

Shilingi Milioni Thelathini (30,000,000/=) walitumia kufidia hasara katika kampuni ya KCY na Milioni Nne na Laki sita (4,600,000/=)kwa misaada mbalimbali ya wasiojiweza.

Amesema kwa Msimu wa Kilimo uliopita walilima juml;a ya Ekari Elfu NNE mia sita(4600) na wamekopesha Shilingi Milioni Themanini (80,000,000/=) kwa Marejesho ya Riba ya Shilingi Elfu Tano(5,000) kwa Ekari kwa Vikundi kumi vyenye jumla ya Ekari elfu mbili (2000).

Kampuni ya KCY inayojishughulisha na maendeleo na kufundisha neono la Mungu kwa maneno na Matendo imeanzishwa mwaka 2004 kwa lengo la kusaidia Watanzania kuendelea katika shughuli za Kilimo.

No comments:

Post a Comment