Thursday, September 22, 2011

SHIRIKA LA MICHE LA ITALY LATOA KOMPYUTA KWA SHULE YA MSINGI MJINI IFAKARA

SHIRIKA LA MICHE LA ITALY LATOA KOMPYUTA KWA SHULE YA MSINGI MJINI IFAKARA
Shule ya msingi ya Madukani iliyopo kata ya Ifakara wilayani Kilombero, hivi karibuni imepokea Kompyuta kumi na Printer moja kutoka shirika la MICHE la Italia.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo, bibi Ester Nuruva ameueleza mtandao huu kuwa kompyuta walizopata kutoka katika shirika hilo watazitumia kwaajili ya kuwafunza wanafunzi wa kuanzia darasa la tatu hadi darasa la saba.

Aidha mwalimu mkuu huyo amesema hapo awali shule hiyo ilikuwa inafundisha somo la TEHAMA ambapo ilikuwa inahusu kompyuta kwa nadharia, kutokana na kupata msaada huo wa kompyuta sasa somo hilo litafanywa kwa vitendo.

Bibi Nuruva amesema aliyekabidhi msaada huo kwa shule hiyo alikuwa Rais wa shirika hilo, bibi Eva Maria Bardeleben kutoka Italia.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Madukani, amelishukuru shirika hilo kwakuwa na moyo wa kujitolea kwa upande wa sekta ya elimu, hivyo ameyaomba mashirika mengine kuwa na moyo wa kutoa misaada hususani katika sekta ya elimu.

No comments:

Post a Comment