Thursday, September 22, 2011

MBUNGE WA MIKUMI ACHANGIA SHILINGI MILIONI 27.3KWA MIRADI YA MAENDELEO

MBUNGE WA MIKUMI ACHANGIA SHILINGI MILIONI

Mbunge wa jimbo la Mikumi kwa tiketi ya CCM, bwana Abdulsalam Ameri hadi sasa kwa muda wa miezi kumi akiwa mbunge, amekwisha tumia jumla ya shilingi milioni 27.3 kwa kuchangia miradi ya maendeleo ya kata.

Bwana Ameri amesema jimbo lake la mikumi lina jumla ya kata 14 na yuko katika ziara ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagu kuwa mbunge na kupita kata hadi kata.

Amesema hadi Septemba 20 mwaka huu amekwisha tembelea kata kumi kwa kufanya mikutano ya kuwashukuru na kupata kero kutoka kwa wananchi wa kata husika.

Hivyo amewataka wananchi wa jimbo hilo kuwa uchaguzi umekwisha mwaka 2010 na makundi yamekwisha sasa imebaki kufanyakazi ya kujenga uchumi wa nchi yetu na amewataka viongozi wa serikali za kata wafanye kazi isiyokuwa na jazba.

Aidha mbunge huyo amewaasa viongozi waache kufuata makundi, wafanye kazi waliyotumwa pia amewataka viongozi wa vijiji kuwasomea taarifa ya mapato na matumizi wananchi wa vijiiji vyao kwa kila kipindi cha miezi mitatu ili wananchi wawe na imani na viongozi wao na kuhamasika kujiletea maendeleo.

No comments:

Post a Comment