Thursday, September 22, 2011

WANANCHI WA KIDODI WILAYANI KILOSA WACHANGA SHILINGI MILION TATU KWA AJILI YA MRADI WA MAJI.

SHILINGI MILION TATU KWA AJILI YA MRADI WA MAJI.

Jumla ya shilingi mil.3 zimekusanywa kutokana na mchango wa wananchi wa kijiji cha lumango kata ya kidodi wilayani kilosa kwaajili ya mradi wa maji ya mtiririko.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na afisa mtendaji wa kijiji hicho sept 18 mwaka huu katika mkutano wa hadhara uliofanyika katia kata ya kidodi kwa mbunge wa jimbo la mikumi bwana Abdulsalam Amer,imeeleza kuwa kijiji hicho kimepangiwa kuchangia mradi huo kiasi cha shilingi mil 4 na laki 5.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa kwa mbunge wa jimbo hilo imeeleza kuwa wananchi wa kijiji hicho hadi sasa wanadaiwa shilingi mil 1 na laki 5 kwa ajili ya mradi hou.

Diwani wa kata ya kidodi bwana Ibrahim Fatahaki amesema kuwa katika kata hiyo,kijiji cha lumando kinaongoza kwa mchango wa mradi wa maji katika kata ya kidodi.

Wakati huohuo wananchi wa kijijik hicho wamfyatua jumla ya matofali 20000 ya kuchoma kwa ajili ya ujenzi wa zahanati unaotarajia kuanza hivi karibuni.


Hata hivyo mbunge wa jimbo hilo bwana Amer ameahidi kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo kwa kutoa vifaa vya ujenzi.

No comments:

Post a Comment