Tuesday, September 27, 2011

RASIMU YA HESABU KATIKA HALMASHAULI YA WILAYA YA KILOMBERO


RASIMU YA HESABU WILAYA YA KILOMBERO


Jumla shilingi bilioni 15 milioni 690 laki 944,313.00 zimepitishwa na baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya kilombero katika kikao cha kupitisha rasimu ya kitabu cha hesabu za mwisho za halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha ulioisha juni 30 mwaka huu.

Fedha hizo zimepitishwa na baraza la madiwani hii leo katika kikao maalumu cha kupitisha Rasimu ya kitabu cha hesabu za mwisho za Halmashauri kwa mwaka wa fedha ulioisha 20110/2011kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya.

Rasimu hiyo imeonyesha kuwa kiasi hicho cha fedha ni majumuisho ya mali za kudumu ambazo zimefikia kiasi cha shilingi bilioni 10 milioni 499,16,346.00 na mali za muda mfupi shilingi bilioni 5 milioni 191 laki 927,967.00.

Aidha sehemu kubwa ya mali hizo zimetokana na fadha za ruzuku kutoka serikali kuu na michango ya wahisani kiasi cha shilingi bilioni 14 milioni 79 laki 763,492.00 na ziada ilyohifadhiwa ni shilingi bilioni 1 milioni 611 laki 180,821.00.

No comments:

Post a Comment