Thursday, September 22, 2011

PAMBAZUKO FM RADIO 90.7 MHz IFAKARA YAZIDI KUONGEZA USIKIVU.

PAMBAZUKO FM RADIO 90.7 MHz YAZIDI KUONGEZA USIKIVU

Kituo cha radio mjini Ifakara Mkoani Morogoro Panbazuko Fm sterio 90.7MHz, kwa sasa wameongeza usikivu wao kwa lengo la kuwafikia wananchi walio wengi katika sehemu mbali mbali.

Wakizungumza na mtandao huu kwa nyakati tofauti,mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho bi THERESIA MAKUNGU amesema kwa sasa wameweza kuwa na usikivu mzuri na kuwafikia wananchi walio wengi mara baada ya kumaliza kufunga mitambo yao mipya.

Bi Makungu amesema lengo kubwa la kituo chao ni kuwahabarisha wananchi yale yanayokuwa yakiendelea katika maeneo yao na duniani kwa ujumla.

Mafundi wakiimarisha mitambo ya radio pambazuko fm ifakara(picha juu)

Nae mwariri mkuu wa kituo hicho bwana ELIAS MAGANGA amesema kwa sasa wamekuwa katika wigo mpana katika kuwahabarisha wananchi wa maeneo mbali mbali ambako radio hiyo imekuwa ikirusha matangazo yake.

Maganga amesisitiza kuwa lengo kubwa la kutoa habari ni kuwajulisha wananchi yale yanayokuwa akiiendelea katika sehemu mbali mbali katika maeneo yao,na kuongeza kuwa siku zote chombo cha habari hakina ugomvi na yeyote bali vimekuwa vikitoa yale mazuri na maovu yanayofanywa katika jamii.

Wakati huo huo aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kilombero na mkuu mpya wa mkoa wa Mwanza mheshimiwa Evarist Ndikilo ameipongeza radio pambazuko kwa juhudi zake katika kuwaelimisha na kuwahabarisha wananchi wa wilaya ya kilombero.

Ndikilo ameyasema hayo katika taarifa yake fupi aliyoitoa moja kwa moja kupitia kituo hicho cha radio katika kipindi cha JIONI LEO siku ya alhamisi alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya ya kilombero katika kuwaaga kwake.

Radio Pambazuko fm kwa sasa inasikika katika mikoa ya Morogoro,Lindi ,Ruvuma na Iringa hususani katika wilaya mpya ya KILOLO

Sehemu ya antena mpya za pambazuko fm radio katika picha ya anga...

1 comment:

  1. Baraza la watoto mkoan Arusha limeiomba serkal kuingilia Kati adhabu zinazotolewa Na walimu Na baadhi ya walez kwa watoto kwani zinazorotesha hali ya kusoma,kujenga na kunasababisha wanafunz weng kufanya vbaya katika masomo Yao.
    Akizungumza Na waandishi WA habari jijini Arusha mwenyekiti WA watoto mkoani humo bwana Hassan kimaro amesema watoto wanafanyiwa vtendo vng vya kikatili hivyo serikal ameiomba kuingolia kati.
    Aidha ameiunga mkono jitihada za raisi john magufuri katoka siku 100 yangu alipoingia madarakani Na kuomba kianziahwe chama chama cha wanafunz WA shule ya msingi Na sekondar cha kuelezea matatizo Yao hasa yanayohusu elimu.

    ReplyDelete