Monday, August 11, 2014

KIKWETE AFANYA KWELI KWENYE MASOMO YA SAYANSI KWA SHULE ZA SEKONDARI NCHINI TANZANIA



Afisa Tarafa wa tarafa ya Ulaya Raphael Mvulungu amewataka wananchi kuendelea kuchangia ujenzi  wa  Maabara tatu katika shule za sekondari.
                                   Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvulungu

Ameyasema hayo August 10 mwaka huu wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari  utakayogharimu kiasi cha fedha cha shilingi milioni 84 ambapo kwa sasa wameanza kuchangisha fedha hizo  kwa wananchi kiasi cha shilingi 5000 kwa kila mwananchi ambapo katika Tarafa hiyo kuna nguvu  kazi 5000 ambao wanatakiwa kutoa mchango huo ambapo hilo ni  agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Jakaya Kikwete ambapo amehitaji  kila shule sekondari  iwe na maabara tatu za Sayansi , Bailojia , Kemia na Fizikia na amehitaji maabara hizo kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
                  Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Ukwiva Liberath Patrick Ngure

Kwa upande wake mkuu wa shule ya Sekondari ya Ukwiva Liberath ngure amesema kuwa mpango huo utasaidia kukuza kiwango cha ufaulu kwa upande wa masomo ya sayansi na kusema kuwa changamoto iliyopo ni baadhi ya wazazi kushindwa kujua umuhimu wa maabara na aamewaomba wananchi kwa ujumla kuwa na moyo wa kuendelea kuchangia ili kukamilisha ujenzi wa maabara hizo.                                                                                                                                                        
     wanafunzi wa shule ya sekondari ukwiva wakiwa katika jengo lililojengwa na TANAPA Shuleni hapo                                                                                                                              

No comments:

Post a Comment