Tuesday, August 12, 2014

MIFUGO YAWA TISHIO WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WAKULIMA WAHANGAIKA WASIJUE PAKWENDA



Mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amewataka viongozi  wa vijiji kutowapokea wafugaji  wanaotoka maeneo ya vijiji vya  jirani na kuvamia katika maeneo ya wakulima.
                                            Baadhi ya mifugo iliyopo kijiji cha ulaya mbuyuni

Ameyasema hayo agost  11 mwaka huu wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na wafugaji kuvamia maeneo ya wakulima wilayani kilosa mkoani morogoro na kusema kuwa katika wilaya yake kuna wafugaji wengi hivyo hahitaji tena wafugaji kutokana na wilaya hiyo kuwa na wafugaji wengi na kukwamisha shughuli nyingine za kimaendeleo. 
                       mazao aina ya mbaazi yakiwa yameharibiwa na mifugo katika kijiji cha ulaya mbuyuni

Ameongeza kwa kusema kuwa viongozi waliopo vijijini wanawakaribisha wafugaji hao kwa kupewa rushwa na wanapoona mambo yanawashinda  huchukua hatua ya kuwafukuza na na kushindwa kutokana na rushwa ambayo wameshaipokea.
Pia amesema kuwa pindi atakapo baini kuwa kiongozi yeyote amepokea rushwa kwa ajili  ya kumkalibisha mfugaji katika eneo lake basi atakuwa amepoteza sifa ya kuwa kiongozi. 
                                   mifugo aina ya ng'ombe ikiendelea kula mazao aina ya mbaazi

Aidha ametoa wito kwa wakazi wa kilosa kuwa na matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya wakulima na wafugaji kwa ajili ya kulinda ardhi na pia kuondoa migogoro.
Kwa upande wake katibu tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvurungu amesema kuwa katika kata yake ni kweli mifugo ipo lakini hajui wafugaji hao wameingia vipi kutokana na wenyeviti wa viji kuwatetea wafugaji hao kuwa wanawatambua uwepo wao hivyo kushindwa kuwachukulia hatua za kisheria wafugaji hao
                                    Mwenyekiti wa kijiji cha ulaya mbuyuni Rashid Mjomba

Naye mwenyekiti wa kijiji cha ulaya mbuyuni Rashidi Mjomba amesema kuwa katika kijiji chake kuna wafugaji wamevamia kijiji hicho na hajui wametoka wapi na hatua za kuwaondoa wafugaji hao zinachukuliwa na ameeleza kuwa  kuna changamoto inayowakumba kwa sasa ni kwa baadhi ya wananchi kudai kuwa endapo wafugaji hao wa jamii ya kimasai wataondoka uchumi utashuka kijijini hapo kutokana na wafugaji hao kiuwa wateja wazuri kiatika biashara zao.

No comments:

Post a Comment