Tuesday, August 5, 2014

WANANCHI WILAYANI KILOSA MKOANI MOROGORO WALALAMIKA KUCHAKACHULIWA FEDHA ZAO



Wananchi wa wilayani kilosa mkoani morogoro wameilalamikia serikali kwa matumizi mabaya ya fedha zao za kodi ambazo zipo kwa ajili ya maendeleo ya nchi yao na badala yake baadhi ya viongozi kutumia fedha hizo kwa manufaa yao binafsi.
                            Wananchi wakiwa katika barabara iliyofunguliwa na mh:waziri wa nchi ofisi ya waziri  mkuu tawala za mikoa TAMISEMI Hawa Ghasia

Baadhi ya wananchi hao khamisi juma na Bi,Aisha Salehe wamesema kuwa barabara hiyo yenye kiwango cha lami imetengenezwa bila ubora wowote kwani haijachukua muda tangu kukamilika kwake lakini kuna baadhi ya vipande vimeshaanza kubanduka.
Aidha wamesema kuwa baada ya ufunguzi wa barabara hiyo yenye kiwango cha lami yenye urefu wa km 0.9 inayokadiliwa kuwa imetumia kiasi cha shilingi milioni mia tatu 300 za kitanzania ambapo barabara hiyo imefunguliwa na julai 18 mwaka huu na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Hawa Ghasia. 
                                   Wananchi wakishuhudia barabara ikifunguliwa rasmi

Akijibu malalamiko hayo mkuu wa wilaya ya kilosa Elias Tarimo amesema kuwa wananchi wasiwe na wasiwasi kuhusiana na ujenzi huo wa barabara kwa kusema kuwa watakuja wataalamu kwa ajili ya kuja kupima kiwango kilichojengwa katika barabara hiyo na kusema kuwa barabara hiyo imejengwa kwa kiwango cha kati na kuhusiana na ubora amewaambia wananchi kusubiri wakaguzi watakapo kuja kwa ajili ya kutoa majibu ya ujenzi wa barabara hiyo na ameongeza kuwa mpango huo wa ujenzi wa barabara ni mpango wa kuboresha mji wa kilosa kuwa katika muonekano mzuri  na ameongeza kuwa huo na mpango mwendelezo wa kuboresha barabara za mji huo wa kilosa.

No comments:

Post a Comment