Tuesday, August 12, 2014

WANANCHI WA KIJIJI CHA ULYA MBUYUNI WILAYANI KILOSA WANUFAIKA NA MRADI MKAA ENDELEVU NA UVUNAJI WA HEWA SAFI KWA KUJENGEWA OFISI YA KIJIJI NA SHIRIKA LA MKUHUMI



Wananchi wa kijiji cha Ulaya mbuyuni wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamelishukuru shirika TFLG na Mjumita kwa kuwajengea ofisi ya kijiji kijijini hapo.
                         Maandalizi ya ujenzi wa ofisi ya kijiji katika kijiji cha mbuyuni wilayani kilosa mkoano morogoro

Afisa Tarafa wa Tarafa hiyo ya Ulaya Raphael Mvulungu amesema kuwa wanalishikuru shirika hilo kwani wamenufaika nalo kwa kiasi kikubwa kutokana na mpango ulioanzishwa kijijini hapo wa matumizi bora ya ardhi ambapo unahusishwa na uvunaji wa hewa ukaa na kuongeza kuwa hadi sasa kijiji kimejipatia fedha nyingi kupitia mradi huo. 
                                             Afisa tarafa wa tarafa ya ulaya Raphael Mvulungu

Naye mwenyekiti wa kijiji hicho cha Ulaya Mbuyuni Khamisi Mjomba amesema kuwa kupitia shirika hilo kijiji kina fedha zaidi ya shilingi milioni 41 kwenye benki ya CRDB na fedha hizo zitatumika katika shughuli za kimaendeleo.
                                       Mwenyekiti wa kijiji cha ulaya mbuyuni Rashid Mjomba

Na ameongeza kuwa katika ujenzi huo wa ofisi ya kijiji gharama zote zitakuwa ni za shirika na siyo zile fedha ambazo zimeshakusanywa.
                                             Ujenzi wa ofisi ya kijiji ukiwa unaendelea

Naye Mwanakamati katika ujenzi huo wa ofisi ya kijiji Comledy Robert amesema kuwa wanashukuru shirika hilo kwani katika kijiji chao hakuna ofisi ya kijiji na  ofisi inayojengwa sasa itakuwa na ukumbi wa mikutano , mahabusu na ofisi yenyewe na amesema kuwa ujenzi huo unatarajiwa kuanza hivi karibuni na kukamilika mwishoni mwa mwezi wa tisa.

No comments:

Post a Comment