Monday, March 11, 2013

KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA MSAADA WA PIKIPIKI KWA JESHI LA POLIS WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75

KILOMBERO PLANTATION LIMITED YATOA  PIKIPIKI KWA JESHI LA POLISI WILAYANI KILOMBERO YENYE THAMANI YA TSH M 1.75 
 
Kituo Kidogo cha Polisi cha Mngeta kilichopo wilayani Kilombero kimepatiwa msaada wa pikipipiki moja aina ya bajaji Boxer yenye thamani ya shilingi 1,750,000 kutoka kampuni ya Kilombero Plantation Limited KPL.

Meneja Rasilimali watu wa kampuni hiyo Bwana David Lukindo amesema kuwa msaada huo umekabidhiwa hivi karibuni na mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bwana Cater Coleman.

Bwana Lukindo amesema kuwa kampuni imetoa msaada huo baada ya kutambua kituo hicho kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa usafiri na msaada huo na anaamini kwa kiasi kidogo watakuwa wamesaidia katika kuimarisha ulinzi katika tarafa ya mngeta.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa msaada wa pikipiki hiyo Mkuu wa kituo hicho Mkaguzi msaidizi wa Polisi Joseph Elias,ameishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na anawaomba wadau wengine kuiga mfano wa KPL.

Bwana Elias amesema kuwa jeshi la polisi linakabiliwa na changamoto nyingi hususan usafiri hali inayowafanya kushindwa kuwafikia wananchi katika maeneo mengi hivyo kupatikana kwa  usafiri huo utasaidia jeshi hilo kupambana na wahalifu kwa kuwafikia wananchi wengi ,ili kupunguza vitendo vya uhalifu katika tarafa ya mngeta.
 

No comments:

Post a Comment