Monday, March 4, 2013

TIMU YA KIKAPU YA ST JOSEPH MOROGORO YACHAKAZWA 71-16

TIMU YA KIKAPU YA ST JOSEPH MOROGORO YACHAKAZWA 71-16.


Mchezaji wa timu ya Mt.Joseph Andrew,akijaribu kuokoa mpira katika mchezo uliofanyika juzi katika uwanja wa Polster Club dhidi ya Kihonda Hits(Picha na Mussa Enock)

Timu ya kikapu ya chuo cha Mtakatifu Joseph kilichopo kihonda barabara mpya Mkoani morogoro imechakazwa vibaya kwa jumla ya point/alama  71-16 dhidi ya timu ya Kihonda Hits katika mchezo wa kirafiki uliofanyika siku ya jumamosi ya tarehe 02 mwezi 03 mwaka huu.

Mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Polister Club  uliopo Kihonda Maghorofani ulimalizika  kwa timu ya chuo cha Mtakatifu Joseph kwa kucharazwa jumla ya point/alama 71 kwa 16 dhidi ya wapinzani wao Kihonda Hits.

Mchezo huo ulioanza kwa kasi na kuwafanya timu ya Kihonda Hits kuanza kupata point/alama 6 mfululizo na katika dakika ya 8 ya mchezo mchezaji hatari wa  st joseph maarufu kwa jina la Kulwa aliweza kuwainua mashabiki wa timu ya Chuo cha Mtakatifu Joseph kwa kufunga point zililochochea kasi ya mchezo kuongezeka kwa timu hiyo.

Hata hivyo jitihada hizo hazikuleta matumaini ya kutosha kwa upande wa timu ya chuo cha  Makatifu Joseph kwani hadi timu zinaenda mapumziko matokeo yalikua ni 37-12,Matokeo ambayo yalianza kuwavunja moyo wachezaji na mashabiki wa timu hiyo.

No comments:

Post a Comment