Saturday, March 16, 2013

WATOTO WALEMAVU WA KITUO CHA BETHELEHEMU WILAYANI KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA

WATOTO WA KITUO CHA BETHELEHEMU KILOMBERO WAPATIWA ZAWADI YA SIKUKU YA PASAKA.

Wanawake wa kata ya Kibaoni Wilayani Kilombero wametoa msaada wa mbuzi wawili kwa ajili ya sikukuu ya pasaka kwa watoto walemavu wa akili wa kituo cha bethelehemu unaogharimu jumla ya shilingi 180,000.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo Mratibu wa kamati ya sherehe ya siku ya mwanamke duniani Bi Sophia Msiku amesema kuwa msaaada huo umepatikana baada ya wanawake hao kufanya harambee katika sherehe ya siku ya wanawake duniani.

Bi Msiku amesema kuwa katika kusherekea siku ya mwanamke duniani walipanga kushiriki na watoto hao lakini kutokana na mambo kuingiliana walishindwa kufanya hivyo na badala yake walipanga siku ya kupeleka msaada huo.

Akizungumza wakati akipokea msaada huo mlezi mkuu wa kituo hicho Sister Maria Dorothea Lyimo amewashukuru akina mama hao na amewataka watu wengine kuiga mfano huo kwa kutoa msaada huo kwa watoto hao .

No comments:

Post a Comment