Thursday, March 7, 2013

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO BI AZIMINA MBILINYI KUONGOZA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI HUMO.



SIKU YA MWANAMKE DUNIANI


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Bi Azimina Mbilinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani ambayo yataadhimishwa na wanawake wa  kata ya Kibaoni katika viwanja vya soko la Kibaoni.

Mratibu wa kamati ya maandalizi ya maadhimisho hayo Bi Sophia Msiku ambae ni Afisa Mtendaji wa kata hiyo amesema kuwa kata ya kibaoni imejipanga vizuri katika maadhimisho hayo .

Bi Msiku  amesema kuwa maadhimisho hayo yataanza kwa maandamano kuanzia maendeeleo na maandamano hayo yatapokelewa na Mgeni rasmi katika viwanja hivyo.

Amesema katika maadhimisho hayo kutakuwa na maonyesho ya sanaa,michezo mbalimbali,na pia wanawake watatoa ushuhuda mbalimbali.

Ameongeza kuwa Mbali na kutoa ushuhuda mbalimbali pia  elimu ya watu kujua haki zao katika kupambana na rushwa itatolewa
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema kuwa uelewa wa masuala ya jinsia katika jamii,ongeza kasi.




No comments:

Post a Comment