Monday, March 11, 2013

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA MSAADA WA VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO MH.ABDUL MTEKETA ATOA  VITABU 200 VYA MASOMO MBALIMBALI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KIYONGWILE

MBUNGE wa Jimbo la Kilombero Mheshimikwa Abdul Mteketa ametoa msaada wa Vitabu 200 vya Masomo mbalimbali kwa Shule ya Sekondari ya Kiyongwile iliyopo Kata ya Ifakara.

Akizungumza na Wanafunzi na Walimu wa Shule  hiyo Wakati akikabidhi msaada huo Mheshimiwa Mteketa amewaeleza kuwa  Lengo  la msaada huo ni kuinua Taaluma na kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi  wa shule hiyo na pia ni moja ya kutekeleza ahadi ya kuboresha Elimu kwa shule za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Kilombero.

Amewataka Wanafunzi na Walimu kuvitunza Vitabu hivyo ili Viwasaidie wanafunzi waliopo kwa sasa na watakaokuja baadaye.
Msaada uliotolewa ni Vitabu vya Masomo ya Fizikia, Kemia, Jiografia, Baiolojia na Hisabati.

Mbali na Msaada huo Mbunge huyo ametoa Msaada wa Kalamu za Wino na Mkaa zenye Thamani ya Shilingi Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000/=)kwa shule ya Msingi ya Lipangalala huku akiwaahidi kujenga Vyoo na kuweka Maji katika Shule hiyo.

Mheshimiwa Mteketa ametoa ahadi hiyo baada ya uongozi wa shule hiyo kumweleza matatizo hayo likiwemo  na tatizo la Ukosefu wa Umeme shuleni hapo.










No comments:

Post a Comment