Wednesday, March 6, 2013

MAZISHI YA MWIGIZAJI ALIYEPOTEA MKOANI NJOMBE YAFANYIKA.

Mazishi ya Mkazi Mmoja wa Kibena Mjini Njombe bwana Mexon Nyekelela Chota Yamefanyika Katika Makaburi ya Kibena,Ikiwa ni Baada ya Kupatikana Kwa Mwili wa Marehemu Uliokuwa Amezama Kwa Siku ya Tano Katika Mabwawa ya Kampuni ya TANWAT Mjini Njombe.

Akizungumza Mara Baada ya Kupatikana Kwa Mwili Huo Afisa Tarafa ya Njombe Mjini Bi Lilian Nyemele Ameishukuru Kampuni ya TANWAT Kwa Namna Ilivyoshiriki Katika Kusaidia Zoezi Hilo Pamoja na Wananchi Wote Walioshiriki.





Mwili wa Marehemu Ulipatikana Leo Majira ya Saa Nane Mchana Ikiwa ni Baada ya Jitihada za Muda Mrefu za Wananchi na Viongozi Kuweza Kuutafuta Mwili Huo Bila Mafanikio Kutokana na Ukosefu wa Vifaa Vya Uokozi.

Akizungumza Mara Baada ya Kuwasili Mkoani Njombe Mtaalam wa Uzamiaji Kutoka Jijini Dar Joseph Mapunda Anasema Kuna Haja Kwa Serikali ya Mkoa wa Njombe Kuanza Kutoa Mafunzo Kwa Wananchi na Wataalam Mbalimbali Ili Kuweza Kupata Wataalam wa Uzamiaji.

Marehemu Mexon Nyekelela Chota Alizama Kwenye Mabwawa Hayo Mnamo March Mosi Mwaka Huu Majira ya Saa Kumi na Moja Jioni Wakati Akiwa na Wenzake Mara Baada ya Kumaliza Shughuli Zao za Sanaa.

No comments:

Post a Comment