Tuesday, March 12, 2013

WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU

WAKULIMA WILAYANI KILOMBERO WALALAMIKIA UCHELEWESHWAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU .

Wakulima wa vitongoji vya lipangalala,lihami,kwa mkuya na kiyongwile kata ya Ifakara Wilayani Kilombero wamelalamikia kucheleweshwa mbolea ya ruzuku  ambayo ilitakiwa kufika tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana.

Wakizungumza na Mtandao huu wa habarikwanza Baadhi ya wakulima wamesema kuwa pembejeo katika maeneo hayo zimechelewa kufika hali ambayo imewafanya wakulima hao kushindwa kuzitumia hasa zile za kupandia kutokana na muda kupita.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya kugawa vocha za pembejeo katika maeneo hayo Bwana Paulo Magehema amekiri malalamiko ya wakulima hao ambapo amesema kuwa mbolea hiyo ilitakiwa ifike mwaka jana lakini imefika mwezi machi mwaka huu  huku  mimea ikiwa imeshaota na kukua hivyo kwa upande wa mbolea ya kupandia haitafanya kazi yoyote.

Hata hivyo amesema pamoja na kucheleweshwa kwa mbolea hizo wakulima 300 watanufaika na mbolea hizo ambazo zimefika  chache ambazo hazitakidhi idadi ya wakulima waliotuma maombi ya kupatiwa mbolea hizo




No comments:

Post a Comment