Friday, March 8, 2013

WAKANDARASI WAASWA KUFANYA KAZI ZAO KATIKA KIWANGO KINACHOSTAHILI.

WAKANDARASI WAASWA WILAYANI KILOMBERO

WAKANDARASI wa Ujenzi Nchini wametakiwa kufanya Kazi  zao kwa kuzingatia Sheria, ubora na Kiwango cha Hali ya Juu.

Akiongea mara baada ya kukagua maandalizi ya Awali ya Ujenzi wa Daraja la Mto Kilombero Mkoani Morogoro, Naibu Waziri wa Ujenzi Injinia Greyson Lwenge amesema kuwa ubora wa hali ya juu unahitajika katika ujenzi unaofanyika na makandarasi wakabidhi Daraja likiwa katika kiwango cha juu.

Amesema kuwa jumla ya fedha Shilingi Bilioni 53 zitatumika katika kukamilisha Ujenzi wa Daraja hilo litakalokamilika Januari 2015.

Tayari shilingi Bilioni 8 zimekwishatolewa kwa ajili ya Mandalizi ya Awali ya Ujenzi wa Daraja hilo linalounganisha Wilaya ya Kilombero na Ulanga.
 Kivuko katika mto kilombero kikitumika kuvusha abiria,wakati wakazi wake wakisubiri    kumalizika kwa daraja mwaka 2015. (picha na Henry Bernard Mwakifuna.)


Awali Injinia Mkuu wa Kampuni ya China Railways Group wanaojenga Daraja hilo Liang Yan Ping amesema kuwa watajenga Daraja hilo kwa Kiwango kwa kuwa wanauzoefu wa Ujenzi wa madaraja.

Liang amesema kuwa Muda wa Miezi 24 uliowekwa utatumika kukamilisha ujenzi huo, ingawa wako Nyuma katika Miezi Mitatu waliopewa kwa ajili ya Maandalizi ya Ujenzi huo.

Wakati huo huo Naibu Waziri wa Ujenzi Injinia Greyson Lwenge amesema kuwa Barabara ya Mikumi, Ifakara, Lupiro hadi Lumecha Mkoani Ruvuma ipo kwenye mchakato wa kupata Wakandarasi watakaoiwekea Lami.

Amesema kuwa Barabara hiyo yenye Urefu wa Kilomita 512 ni muhimu kwa Mkoa wa Morogoro na Taifa kwa Ujumla inataraji kuwa katika Kiwango kizuri ifikapo Mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment