Tuesday, April 15, 2014

AFARIKI DUNIA AKIJARIBU KUVUKA MTO WILAYANI MVOMERO MKOANI MOROGORO.



Mkazi  wa kijiji cha manembo kitongoji cha Mng’ongo wilaya mvomero mkoani Morogoro Theresia Herry mwenye umri wa miaka 80 amefariki baada ya kusombwa na maji katika mto mseleleko mwishoni mwa wiki hii.

Akizungumzia mazingira ya kifo hicho mtoto wa marehemu Martin Cosmas amesema kuwa mama yake alienda shamba siku ya ijumaa akiwa ameongozana na Dada yake Serapia Cosmas na baadaye walipokuwa wanarudi walipofika mtoni Bi, Theresia alipokuwa anajaribu kuvuka  alisombwa na maji hayo na mwanaye aliyekuwa naye alipojaribu kumuokoa alishindwa kutokana na maji hayo kuwa na nguvu na ndipo marehemu alipokutwa na umauti huo.

Aidha mmoja wa  shuhuda wa tukio hilo Charles Golaga amesema kuwa wameshtushwa na kusikitishwa  sana na msiba huo kwa kusema kuwa marehemu alikuwa hajaumwa na alikuwa anatoka shamba ndipo akakutwa na umauti huo.

 Naye mwenyekiti wa kijiji cha mng’ongo amethibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mto huu ni mara ya kwanza kusababisha tukio hilo na kuongeza kwa  kusema  kuwa anawataka wananchi kuwa makini  na maji yanayotiririka mtoni na kuacha tabia kujaribu kuvuka maji yenye kina kirefu na yenye kasi.
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoani Morogoro Faustine Shilogile amesema kuwa tukio hilo bado halijawafikia na kuahidi kulifuatilia.

No comments:

Post a Comment