Monday, April 14, 2014

UPATIKANAJI WA MAFUTA YA TAA WILAYANI KILOSA YALETA GUMZO



Wakazi wa wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wanakabiliwa na uhaba wa mafuta ya taa takribani wiki tatu kutokana na upatikanaji wa mafuta hayo kuwa mgumu.

Akiongea na Clouds fm mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo Kilosa Ally Malingo amesema kuwa amethibitisha kwa kusema kuwa upatikanaji wa mafuta ya taa umekuwa mgumu na kuongeza kwa kusema kuwa ameongea na mmiliki wa sheli ya  ya mafuta Hemedi Bakhamisi na kusema kuwa mafuta hayo ya taa yatapatikana wiki hii.

Naye mmiliki wa sheli hiyo ya mafuta ya taa bakhamisi amesema kuwa upatikanaji wa mafuta umekuwa mgumu kutokana na baadhi ya makampuni yanayoagiza  mafuta nje ya nchi kuacha kuagiza mafuta hayo na kuongeza kuwa mafuta yatapatikana mapema wiki hii na kusema kuwa wanahofia kuchelewa endapo daraja la Ruvu (Kibaha) halitakuwa tayali .

Aidha mfanyabiashara wa mafuta hayo   aliyejitambulisha kwa jina moja la Alex amesema kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara wamepandisha bei ya mafuta kwa kuuza shilingi mia tatu kwa koroboi moja badala ya shilingi mia na hamsini na kuongeza kuwa wameamua kufanya hivyo kutokana na upatikanaji wa mafuta hayo kuwa mgumu.

Pia Bi Mwanaisha Mundo ambaye ni mkazi wa Kilosa amesema kuwa upatikanaji wa mafuta kuwa mgumu umewafanya wao kulala giza , pia ameongeza kwa kusema kuwa mafuta yanayopatikana madukani yanapatikana kwa gharama kubwa na kusema kuwa licha ya gharama kuwa kubwa lakini upatikanaji wa mafuta hayo bado ni mgumu

No comments:

Post a Comment